Tumejifunza nini kama Taifa kuhusiana na uzushi kuhusu afya ya Rais Magufuli?

Uko sahihi kabisa mkuu.Hata mimi karibu nichukuliwe na huo uzushi,lakini nika stabilize baada ya kumuona Rais Ikulu akiendelea na shuhuli za kuapisha viongozi mbali mbali.Mkuu watu ni lazima wajue kwamba wapinzani na waathirika wa utawala wa Magufuli hawampendi,kwa hiyo wanatumia kila mbinu chafu kum-discredit kwa kusambaza uzushi ambao kwa njia moja au nyingine una nia ya ku-prove kwamba Rais anachukiwa na wananchi.Kwa hiyo ni kweli watu wanapaswa kuwa makini sana.

Kwa wapinzani issue ile,ambayo kama ilikuwa photoshopping sijui,lakini kwa ujinga wao walidhani kwamba ile ilikuwa opportune time ya wao kuonyesha kwamba Rais kweli anachukiwa sana na wananchi,jambo ambalo si kweli.
 
Hizi habari za kusema wapinzani ni waathirika wa utawala huu sijui mnazitoa wapi.

Hivi wakulima nao ni wapinzani?
 
Mazwazwa bado hawajaamini kama chuma kipo hai wanasema eti yule ni magufuli yule comedian wa iringa
 
Alafu ile hotuba yake ndani ya dakika 13 tuu kamaliza
Chuma ni mgonjwa

Aliongea kigonjwa sana ile siku anaapisha kitu ambacho si kawaida yake

Kwanza angekua mzima angejibu mapigo mpenda sifa yule
 
Nenda YouTube leo wakati anaapisha viongozi uone live chart zaidi ya 10k walichangia positively ni record ya mwaka! Usihangaike na hawa wa tweeter na JF mawakala wa mafisadi.
Hahhahahaha unakimbia sehemu ya watu wanaojielewa,
 
Mkuu;
Kumbuka nchi yetu bado ni changa kwenye masuala ya mitandao na kwa sababu hiyo wanachi wengi wanaamini kila wanachokisoma kwenye mitandao.

Weka sawa kwanza,

je, hapakutokea sintofahamu yoyote kule Rwangwa?

Ile video inayoonesha watu wakisukumwa na wanausalama wa rais ni ya kweli au ya uongo?
 
Kiukweli tuache utani rais bdo hajawa katika hali yake ya kawaida.tumuombee watanzania...
Nadhani hii ziara ilikuwa ndefu Sana nadhani wandaaji wamejifunza kitu Kwa binadamu yeyote kusafiri Kwa muda wote huo lazima mwili uchoke ongezea na hotuba za chuma kwenye maeneo aliyopita lazima angechoka tu, nadhani kilichotokea ni uchovu wa safari ndefu ya ziara
 
Tusijisahau kwamba sisi ni wanadamu akiwamo Mheshimiwa Rais, kwamba kama walivyo wanadamu wote huamka hufanya shughuli zote za kila siku, na mwisho wa siku huhitaji kupumzika na kulala. Na huenda ikatokea simu moja au siku kadhaa mtu (Akiwemo Rais) akaumwa, akapata matibabu, akapona na maisha yakaendelea kama kawaida. Hakukuwa na dhambi yoyote kwa wananchi kujulishwa kwamba Mheshimiwa Rais 'hajisikii vizuri' hivyo leo au siku mbili hizi ameshauriwa kupata mapumziko ya kutosha, ni jambo la kawaida kabisa.
 
" Mwisho kabisa nimejifunza kuwa inatakiwa kwanza kuchukua muda kabla ya kuamini kile ambacho kimeandikwa kwenye mitandao ya kijamii kwa sababu ukweli hukawia kufika."

[emoji122][emoji122][emoji122]
 
Kiukweli tuache utani rais bdo hajawa katika hali yake ya kawaida.tumuombee watanzania...
Usitupe kazi bwana, muombee wewe pekee yako, sisi tuna watu wengi sana wenye mahitaji kama watoto yatima, wajane, waliodhuliwa na uongozi huu wa awamu ya tano, waliodhulumiwa, waliohukumiwa bila makosa, wagonjwa wa kweli, walionyang'anywa haki zao, waliobambikwa makesi.
 


NDIYO NINI HIYO?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…