Tumekutana Instagram, amenitumia nauli niende kisiwa cha Malta tuonane

Tumekutana Instagram, amenitumia nauli niende kisiwa cha Malta tuonane

Jamaa ananikumbusha ile movie ya get out,demu anajitongozesha kwa wahuni wa kiafrica kisha anawaalika kwenda kwao ambako kuna mjumba wa kifahari.

Kisha ukifika huko watu wanapanda dau ukiwa hapo hapo na wewe huelewi,kisha baada ya hapo unaanza kujua hujui
Ile movie noma.
Amecheza Daniel Kaluuya kama sijakosea.
Hizo mambo zilikua sana miaka fulani hivi nyuma. Blacks walifanyiwa sana unyama.
Wanajua tuna kitu inaitwa 'jungle fever'.
 
Mzee tafuta ethical hackers, recruit akusaidie kusaka taarifa zote kuhusu binti. Kisha fanya analysis na ulinganyifu wa taarifa. Lazima ufanye risk assessment. Dunia imeharibika, lazima kujiridhisha sana kabla ya kufanya maamuzi.
 
Wadau kuna binti tumefahamiana kupitia mtandao wa kijamii Instagram ,ana miaka 17 yupo kisiwa cha Malta, tulianzisha mahusiano kupitia huo mtandao na hatimaye tukabadilishana namba za sim tukawa tunachat WhatsApp na kupigiana video call

Ni mwanafunzi wa chuo na wazazi wake ni wafanyabiashara
Binti alishanitambulisha kwa Dada yake ambaye yupo UK ni mwandishi wa habari na shangazi yake ambaye wapo naye chuoni na wananitaka niende

Hivi vihela vidogo vidogo binti na shangazi yake huwa wananitumia na nikiwauliza hela wanatoa wapi na wapo chuo wanasema wazazi wao wanawapa pocket money

Na wananipenda hatari

Tumefahamiana kama miezi 5 imepita juzi kanitumia dola 2720 niende kumtembelea nchini kwake kisiwa cha Malta.

Naomba nisaidiwe yafuatayo

Nauli kwenda Malta ni dola ngapi?

Vipi kuna usalama hapo? Na vipi maisha ya Malta yakoje anayejua

Vipi sheria za Malta kudate na miaka 17
Au nimzime hii hela na niblock

Updates

Nashukuru kwa michango yenu,wengi mmeshauri nisiende ila wengine wanasema niende

Kwa ujumla naheshimu mawazo yenu ila naomba niungane na wale wa kukubali niende ,nimeanza kuandaa harakati za kwenda huko

Nimewasiliana na mamlaka ya vissa Malta wamenipa utaratibu lakini kwa kipindi hiki cha mlipuko wameshauri kwamba nisubiri kidogo kwa sasa wameweka masharti magumu kidogo ya kuingia nchini kwao

Vissa yao wanashughulikia ndani ya mwezi mmoja ,muda huo nifanye maombi ya vissa nikisubiria hali ya covid inaendaje huko ila wakanitahadharisha nisije nikafanye booking ya ndege mpaka wao waje kuniambia

Pia nitakuwa na tahadhari nikifika Malta na kuna mdau mmoja alinishauri nifikie kwenye kanisa ili niangalie hali ipoje ndo niendelee na mambo mengine ila Watanzania mniombee
Figo zako zipo salama wajina?
 
Maake hapo kwanza ncheke.....

Huyu mwana yu hai kweli???
 
Back
Top Bottom