Tumenasa saini ya Paul Godfrey kutoka Yanga, atakuwa nasi kwa miaka miwili

Tumenasa saini ya Paul Godfrey kutoka Yanga, atakuwa nasi kwa miaka miwili

Hussein Massanza

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
1,016
Reaction score
2,195
IMG_20220702_121603_251.jpg


Watu wa Soka,

Tunaendelea na taarifa kuhusu usajili tulioufanya na maboresho yanayoendelea kwenye benchi la ufundi na kikosi chetu kuelekea msimu ujao wa Ligi Kuu.

Baada ya mshambuliaji Habib Kyombo na kiungo Aziz Andabwile, sasa tumefanikiwa kuinasa saini ya beki wa klabu ya Yanga Paul Godfrey "Boxer" ambaye kuanzia sasa ataitumikia timu yetu kwa miaka miwili.

Tutaendelea na utambulisho wa vifaa vipya mpaka pale dirisha la usajili litakapofungwa.

#TukutaneLigiKuu
#TukutaneMsimuUjao
 
Sasa uyu wa nini si kafeli uyu tafuteni wachezaji wa mahana
 
Hongereni! Yasingekuwa majeraha yaliyo msumbua kwa muda mrefu, muda huu tungekuwa tunaongea mengine kuhusu Paul Godfrey.
Mnajitahidi sana kwenye usajili.

Ikiwapendeza mumfuatilie yule mshambuliaji wa pembeni wa Mbeya Kwanza mfupi na mwenye nguvu na kasi ya ajabu. Alikuwa ndiyo mfungaji bora wakati timu inapanda ligi kuu. Ila kwa bahati mbaya alikuwa hapati nafasi ya kucheza. Badala yake mwalimu wa timi alikuwa akimchezesha zaidi Eliuta Mpepo.


NB; Simfahamu, hanifahamu. Ila ana kipaji kikubwa.
 
chukueni na wengine mjenge timu imara kina Yusuph Athumani, Ninja, Kaseke , Mauya nk ni wazuri ila hawapati game time Yanga
 
Mchukueni na ‘mwaisa, mtu mbaya’ akawavurugieni washambuliaji wenu kwa misumari
 
Back
Top Bottom