Tumeshamaliza Sensa ya 'Mibichwa' yetu, na sasa Sensa hizi zinafuata ili Watanzania tuanze kuwekewa Tozo mpaka ya huu Upumuaji Wetu

Tumeshamaliza Sensa ya 'Mibichwa' yetu, na sasa Sensa hizi zinafuata ili Watanzania tuanze kuwekewa Tozo mpaka ya huu Upumuaji Wetu

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
Ya Watu ( Mibichwa ) yetu inamalizika rasmi ( Kikanuni ) leo na leo hii hii tena inaanza ya Nyumba zetu ( zenu ) na baada ya hapo jiandaeni kwa Sensa za haya yafuatayo.....

1. Sensa ya Walio na Akili na Wasionazo

2. Sensa ya Wanaotumia Condoms na Sisi Wazee wa Kugongesha Besela ( Tulioapa Kutokuvaa Condoms ) hadi Umauti Wetu.

3. Sensa ya Wanaoshindia Maharage, Tembele, Kuku na Nyama.

4. Sensa ya Watumiaji wa Mitandao na wale Wakesha JamiiForums Kuikosoa Mamlaka na Bi. Chifu

5. Sensa ya Wabobezi wa Kugombania DalaDala, Waomba sana Lifti na Wamiliki wa Gari zao Binafsi

6. Sensa ya Wanaolala Sebuleni katika Makochi yaliyoliwa na Panya kwa Mashemeji zao ila Wakiamka Asubuhi wanajifanya Kuchangamka kuliko waliolala Vyumbani katika Vitanda vyenye Magodoro mazuri.

7. Sensa ya Wanaoenda Haja Kubwa sana na Wanakaa huko muda mrefu hadi Kuwatesa Wenzao ambao nao wanataka kuingia huko huko ili Kushusha Mizigo yao Michafu ya Kibaikolojia.

Nyie mlidhani zile Meseji mlizokuwa mnatumiwa Kiungwana na Kudekezwa na Bi. Chifu kuwa Msensabike alikuwa akimaamisha?

Kudadadeki Mazoezi yote haya ya Sensa yakimaliza tutaanza Kulipishwa Mitozo ya kila aina kwani namba Mbili wa Bi. Chifu ambaye Kitaaluma ni Mchumi kwa Kushirikiana na Mpuuzi Mmoja wa Wizara ya i Fedha anayesajili tu Watu wa Amerika ya Kusini kuchezea Wanyiramba Kubwa Nyota FC yake Wamemdanganya Bi. Chifu kuwa ili aweze Kuongoza vyema na asikose Pesa atuwekee Mitozo kwenye Kila Kitu na Huduma mpaka tukome na ikiwezekana tuhamie nchini Burundi.
 
Kwamba Burundi hakutajaa ? Ile nchi ni kama mkoa mmoja tu wa Tanzania
 
Back
Top Bottom