Tumeshindwa kumlinda Asimwe

Tumeshindwa kumlinda Asimwe

fukunyuku1234

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2024
Posts
243
Reaction score
494
Screenshot_20240618_151402_Instagram.jpg


Taarifa za kifo cha huyu mtoto zimeumiza mioyo yetu, mtoto wa miaka miwili kufanyiwa ukatili huu si jambo la kulifumbia macho na ilipaswa tupaze sauti tangu alipokamatwa tarehe 30/05/2024.

Uhai wa Asimwe umedhulumiwa na watu wabaya kwa sababu zao wanazozijua wenyewe lakini kama Taifa tumeshindwa kumlinda mtoto mdogo kwa hapa inabidi tujitafakari.

Ingependeza kama kungetolewa onyo kali kutoka ngazi za juu ili kukomesha mauaji haya ambayo yalipotea kwa muda isaidie kuzuia kasi yake isije ikarudi kama zamani.

Mwisho kabisa watanzania tubadilike na kuachana na hizi dhana wa kuamini mambo ya gizani na tumuogope Mungu ambae ndie muumba wa vyote.

Pumzika Asimwe

Pia soma:
- Kagera: Kisa cha Mtoto mwenye Ualibino kudaiwa kuibiwa, RPC Makungu asema tayari wameanza uchunguzi

- Kufuta mauaji ya albino, ni kutokomeza kabisa Waganga wapiga ramli

- Update: Mwili wa Mtoto Albino (Asimwe) wakutwa hauna baadhi ya viungo
 
Kiasi nimeumia juu ya huyu mtoto siwezi kueleza. Washukiwa wa huu unyama wakikamatwa polisi wafanye press tuwaone na kesi yao hadi hukumu viendeshwe kwa uwazi na liwe funzo.

Kwanza tunatakiwa kuwaona katika press wakiwa hoi kwa kipigo, unyama walioufanya hawana haki yoyote ya kiubinadamu.
 
Kiasi nimeumia juu ya huyu mtoto siwezi kueleza. Washukiwa wa huu unyama wakikamatwa polisi wafanye press tuwaone na kesi yao hadi hukumu viendeshwe kwa uwazi na liwe funzo.

Kwanza tunatakiwa kuwaona katika press wakiwa hoi kwa kipigo, unyama walioufanya hawana haki yoyote ya kiubinadamu.
Kabisa 2 yrs old kid kwelii
 
View attachment 3020022

Taarifa za kifo cha huyu mtoto zimeumiza mioyo yetu,mtoto wa miaka miwili kufanyiwa ukatili huu si jambo la kulifumbia macho na ilipaswa tupaze sauti tangu alipokamatwa tarehe 30/05/2024.

Uhai wa Asimwe umedhulumiwa na watu wabaya kwa sababu zao wanazozijua wenyewe lakini kama Taifa tumeshindwa kumlinda mtoto mdogo kwa hapa inabidi tujitafakari.

Ingependeza kama kungetolewa onyo kali kutoka ngazi za juu ili kukomesha mauaji haya ambayo yalipotea kwa muda isaidie kuzuia kasi yake isije ikarudi kama zamani.

Mwisho kabisa watanzania tubadilike na kuachana na hizi dhana wa kuamini mambo ya gizani na tumuogope Mungu ambae ndie muumba wa vyote.

Pumzika Asimwe
Serikali na Bunge zipo bize na Mpina
 
Serikali na Bunge zipo bize na Mpina
Yani kama Taifa tuna tatizo kubwa la viongozi,Mpina kawashika pabaya macho akili na masikio yote yako kwake

Tangu litokee hili la kupotea kwa huyu mtoto mpaka kifo chake hakuna karipia lolote lililotoka kutoka kwa viongozi si Rais wala Waziri Mkuu

Inasikitisha sana
 
Mwenyezi Mungu, ailaze mahala pema, peponi roho ya mtoto mzuri Asimwe.
Hawa watu wenye imani potofu hawa, walaanike. Unaanzaje kuuwa Malaika asiye na kosa lolote?

Tuanze kampeni ya kuwalinda Albino, Serikali muamke sasa, kuwalinda na kuwapa Elimu, jamii inayoishi nao wasishiriki, watoe taarifa mtu akigusia hilo.
 
View attachment 3020022

Taarifa za kifo cha huyu mtoto zimeumiza mioyo yetu,mtoto wa miaka miwili kufanyiwa ukatili huu si jambo la kulifumbia macho na ilipaswa tupaze sauti tangu alipokamatwa tarehe 30/05/2024.

Uhai wa Asimwe umedhulumiwa na watu wabaya kwa sababu zao wanazozijua wenyewe lakini kama Taifa tumeshindwa kumlinda mtoto mdogo kwa hapa inabidi tujitafakari.

Ingependeza kama kungetolewa onyo kali kutoka ngazi za juu ili kukomesha mauaji haya ambayo yalipotea kwa muda isaidie kuzuia kasi yake isije ikarudi kama zamani.

Mwisho kabisa watanzania tubadilike na kuachana na hizi dhana wa kuamini mambo ya gizani na tumuogope Mungu ambae ndie muumba wa vyote.

Pumzika Asimwe
Daah inasikitisha sana.
 
Rais hakuonekana kuumizwa hata kidogo na huyu mtoto ndo maana hamjasikia kauli yoyote kutoka kwake.

Angekuwa kaumizwa angeitisha press conference ya ghafla na kisha kufunga mipaka yote kwa muda na kisha kumpa IGP na Mkurugenzi Mkuu wa Usalama wa Taifa siku 14 wawe wamewapata wauaji wakiwa hai au wamekufa na ikibidi kuomba msaada Scotland Yard na FBI,huwa nasema siye hatuna Serikali tuna genge la wahuni tu walioshika Bunduki.
 
Back
Top Bottom