Tumeshindwa kumlinda Asimwe

Tumeshindwa kumlinda Asimwe

View attachment 3020022

Taarifa za kifo cha huyu mtoto zimeumiza mioyo yetu,mtoto wa miaka miwili kufanyiwa ukatili huu si jambo la kulifumbia macho na ilipaswa tupaze sauti tangu alipokamatwa tarehe 30/05/2024.

Uhai wa Asimwe umedhulumiwa na watu wabaya kwa sababu zao wanazozijua wenyewe lakini kama Taifa tumeshindwa kumlinda mtoto mdogo kwa hapa inabidi tujitafakari.

Ingependeza kama kungetolewa onyo kali kutoka ngazi za juu ili kukomesha mauaji haya ambayo yalipotea kwa muda isaidie kuzuia kasi yake isije ikarudi kama zamani.

Mwisho kabisa watanzania tubadilike na kuachana na hizi dhana wa kuamini mambo ya wasgizani na tumuogope Mungu ambae ndie muumba wa vyote.

Pumzika Asimwe
"alipokamatwa" tarehe 30/05/2024. Mtoto huyu hakukamatwa alitekwa na wakora.
 
Rais hakuonekana kuumizwa hata kidogo na huyu mtoto ndo maana hamjasikia kauli yoyote kutoka kwake.
Angekuwa kaumizwa angeitisha press conference ya ghafla na kisha kufunga mipaka yote kwa muda,na kisha kumpa IGP na Mkurugenzi Mkuu wa Usalama wa Taifa siku 14 wawe wamewapata wauaji wakiwa hai au wamekufa,na ikibidi kuomba msaada Scotland Yard na FBI,huwa nasema siye hatuna Serikali tuna genge la wahuni tu walioshika Bunduki.
Kiroboto Lucas Mwashambwa njoo hapa umtetee mama.
 
Serikali na Bunge zipo bize na Mpina
Aisee unaweza kuhisi labda sisi tuna planet yetu yani kila uchao ni vituko fikirishi kiasi cha kujiuliza hivi tuna serikali?kila kona ni mapambio lakini huwez kusikia makemeo kutoka ngazi za juu kwenye mambo yanayodisturb jamii inaumiza sana kwa kweli
 
Ilitakiwa siku mtoto anapotea Jeshi, polisi, usalama na kila chombo cha dola waingie Kagera. Baa zifungwe, wauza bangi, waganga wa kienyeji, watiliwa mashaka wote ndani. Kila kijiji kila nyumba oparesheni. Hata asipopatikana lakini siku nyingine mtu akimuona albino awe kama ameona msafara wa Rais. Kila raia anakuwa mlinzi. Kanda ya ziwa wamezidi ujinga.
Umenena vema mzee na ni ishu inayowezekana kabisa lakini huwezi kusikia mpango kazi kama huo cha msingi wakikamatwa wauwawe mbona vibaka tunawaua daily kitaa huku?
 
2024 hii bado kuna watu wanaamini watafanikiwa kuputia ushirikina? Tuna safari ndefu sana...hivi viimani vya kishenzi shenzi vinatupotezea muda sana. Ule usiku mama alipoporwa mtoto palitakiwa pachimbike, asingelala mtu mpaka apatikane.

Rest in peace little angel
 
Nimetokwa machozi Kwa ajili ya huyu mtoto. Napendekeza waziri wa mambo ya ndani, Mkuu wa mkoa na WA wilaya RPC, DSO husika wafukuzwe kazi, mara Moja!
Hivi Toka ametekwa Kwa mama yake serikali walikuwa wanashindwa kumpata akiwa Hai ameuawa ndiyo Wahangaike kutafuta wauaji! Basi mifumo ya nchi yetu itakuwa bado sana. Hawa ni usalama wa taifa au usalama wa viongozi wanasiasa?
 
100 % correct na kwa kufanya hivyo huyo mtoto angeweza kupatikana akiwa hai maana katoroshwa tangu 30/05/2024 kakutwa amefariki 17/06/2024
Ina mana wauaji walikuwa wanaskilizia kwanza.....walipoona kimya kumepoa nadhan ndo wakatekeleza unyama wao.....dah! so painful.
 
Hizi ni mambo za kiboya sana na zipo huko kanda ya ziwa
Inafaa sasa alibino waamishwe huko waamishiwe mikoa salama kama Arusha ambapo alibino wanaishi kwa amani
 
Mwenyezi Mungu, ailaze mahala pema, peponi roho ya mtoto mzuri Asimwe.
Hawa watu wenye imani potofu hawa, walaanike. Unaanzaje kuuwa Malaika asiye na kosa lolote?

Tuanze kampeni ya kuwalinda Albino, Serikali muamke sasa, kuwalinda na kuwapa Elimu, jamii inayoishi nao wasishiriki, watoe taarifa mtu akigusia hilo.
Huyu mtoto ni peponi moja kwa moja
 
Hizi ni mambo za kiboya sana na zipo huko kanda ya ziwa
Inafaa sasa alibino waamishwe huko waamishiwe mikoa salama kama Arusha ambapo alibino wanaishi kwa amani
Arusha
Njombe
Moshi
Iringa
Geita

Hii mikoa inaongoza kwa mauwaji ya watu, hiyo salama sijui inatoka wapi. Ni bora ukasema Dar, tanga na pwani yote kwa ujumla
 
Halafu eti Tanzania ni nchi ya amani 😄 amani, hii nchi imejaa watu makatili sana, hawana tofauti na mayahudi yaliyolaaniwa
 
Kiasi nimeumia juu ya huyu mtoto siwezi kueleza. Washukiwa wa huu unyama wakikamatwa polisi wafanye press tuwaone na kesi yao hadi hukumu viendeshwe kwa uwazi na liwe funzo.

Kwanza tunatakiwa kuwaona katika press wakiwa hoi kwa kipigo, unyama walioufanya hawana haki yoyote ya kiubinadamu.
Nasikitika kukujurisha kwamba haitakua vile unatamani.
 
Arusha
Njombe
Moshi
Iringa
Geita

Hii mikoa inaongoza kwa mauwaji ya watu, hiyo salama sijui inatoka wapi. Ni bora ukasema Dar, tanga na pwani yote kwa ujumla
Nikumbushe lini albino aliuwawa au kukatwa viungo huko Arusha

Arusha ni sehemu albino wanaishi kwa amani na furaha wanatembea kwa uhuru bila hofu ya kutekwa na kuuwawa.
 
Hili jambo kutokea ni lazima serikali ilaumiwe yote na vyombo vyake … haya mambo yalikwisha kabisa naona yamerudi tena……

Lazima Rais awe mkali zaidi alitakiwa aanze kula kichwa cha RPC
 
View attachment 3020022

Taarifa za kifo cha huyu mtoto zimeumiza mioyo yetu,mtoto wa miaka miwili kufanyiwa ukatili huu si jambo la kulifumbia macho na ilipaswa tupaze sauti tangu alipokamatwa tarehe 30/05/2024.

Uhai wa Asimwe umedhulumiwa na watu wabaya kwa sababu zao wanazozijua wenyewe lakini kama Taifa tumeshindwa kumlinda mtoto mdogo kwa hapa inabidi tujitafakari.

Ingependeza kama kungetolewa onyo kali kutoka ngazi za juu ili kukomesha mauaji haya ambayo yalipotea kwa muda isaidie kuzuia kasi yake isije ikarudi kama zamani.

Mwisho kabisa watanzania tubadilike na kuachana na hizi dhana wa kuamini mambo ya gizani na tumuogope Mungu ambae ndie muumba wa vyote.

Pumzika Asimwe
Mkuu jiulize why kikikaribia kipindi cha uchaguzi haya mauaji yanatokea sana!!!yaani ningekua RAIS mm, ningekamata waganga wote na kupiga risasi hadharani!!
 
Nikumbushe lini albino aliuwawa au kukatwa viungo huko Arusha

Arusha ni sehemu albino wanaishi kwa amani na furaha wanatembea kwa uhuru bila hofu ya kutekwa na kuuwawa.

Nikweli kwa kaskazini sijawahi kusikia hilo, ila kwa mauwaji mengine tofauti na hilo aaaagh mmetisha+Iringa, njombe, geita na hata tarime japo kwa siku hizi yamepungua
 
Taifa lisipofundisha watu wake namba Bora zakujipatia kipato basi shetani hujiinua na kudanganya wajinga hao Kwa pesa za mazingaombwe!
Nchi inafeli Kwa kutoka elimu mbaya Kwa maisha ya Leo na Dunia ya Leo.
Jiulize kijana aliyemaliza chuo Leo anajua kilimo Bora,ufugaji Bora,ubunifu na kuanzisha viwanda vidogovidogo? Ikiwa ndiyo sekta inayoweza kubeba vijana wengi.
Vijana wetu wanajua zaidi udalali,kamari na kutafuta pesa za kishirikina!!
Hii ni Aibu kubwa kwa taifa lolote linalojipambanua kuwa na watu wazima wanaojiita wasomi,viongozi na wacha Mungu
 
Back
Top Bottom