Hawa wenye hizi kampuni za khamari wanatengeneza hela sana. Juzi tu hapa Sweden ilikua inazungumziwa hili suala la hawa jamaa na kopato chao pammoja na watu wanavyo poteza hela zao hadi kuingia kwenye madeni.
Ebu angalia hapa Tanzania kuna watu zaidi ya 50 milions, tuseme wenye uwezo wa kucheza ni watu milioni mmoja, kila mtu alipe 1000 kwenye mchezo, 1000 000×1000=1000 000 000 hizo hela zigawe kwenye kampuni 10 tofauti zinazo chezesha inakua 100 000 000 just imagine hapo ni kampuni mmoja tu inaweza kuingiza milioni mia au zaidi kwa wiki.
Nchini Sweden kuna kampuni ya kuchezesha hizi khamari SVENSKASPEL lakini wao hawapo kwa ajili ya faida ya mtu binafsi, wao faida inawarudia vijana.
Mfanao mchezo mmoja unaoitwa eurotips wanaweza wakainiza 10 000 000 krons sawa na 1000000 dola au ziadi kidogo, na wakatoa hela kwa washindi around 500 000 dolars, cha ziada ni hela zitakazo jenga viwanja vya aina mbali mbali mitaani, wanaangalia pale panapo hitajika, ni mkoa bani, walaya gani, kijiji gani kinahitaji kutengenezewa viwanja, na hapo sio tu eurotips pekee, kuna michezo tofauti zaidi ya 50, kila mmoja inaingiza dola milioni mmoja. Na uzuri wao hawa hua wanaandikaga kiasi kilichopatikana kila siku.
Serikali ya Tanzania nao wangeanzisha kitu kama hicho ili kuboresha michezo