sonofobia
JF-Expert Member
- Jun 21, 2015
- 1,171
- 4,295
Ee mwumba wetu, umewaunganisha watu katika ndoa takatifu nami natumaini kupokea Sakramenti hiyo na kushirikiana na mwenzangu wa ndoa maisha yangu yote.
Kwa hiyo nakuomba ee Bwana unisaidie kuchagua kwa hekima, nipate mchumba mwema, safi na mwaminifu, nifuate zaidi uzuri wa roho kuliko wa uso, zaidi tabia njema kuliko umaridadi.
Mioyo yetu iwe ya kulingana, na nia zetu zipatane, tupate kuishi pamoja na amani na kulea jamaa zetu kwa kukuheshimu wewe na baraka zako Amina.
Kwa hiyo nakuomba ee Bwana unisaidie kuchagua kwa hekima, nipate mchumba mwema, safi na mwaminifu, nifuate zaidi uzuri wa roho kuliko wa uso, zaidi tabia njema kuliko umaridadi.
Mioyo yetu iwe ya kulingana, na nia zetu zipatane, tupate kuishi pamoja na amani na kulea jamaa zetu kwa kukuheshimu wewe na baraka zako Amina.
>>> Fanya hii Sala asubuhi na jioni, baada ya muda utayaona majibu.