Tumlaumu Nyoka au Adam na Eva?

Tumlaumu Nyoka au Adam na Eva?

Da Vinci XV

JF-Expert Member
Joined
Dec 7, 2019
Posts
3,862
Reaction score
6,438
Wasalaam,

Katika wale wote tunaofuata Iman ya Mungu mmoja ama mafundisho yanayofanana na kutofautiana katika sehemu chache
Haswa katika dini kuu Uislam ,Ukristo na Uyahudi.

Katika pande zote hizo tunaamini jambo moja juu ya huyu mungu wetu ya kwamba yeye ndiye mjuzi wa yote yaliyotekea na yajayo.

Na kuna ule msemo maarufu sana wa wazee wetu wa zamani eti "MOLA NDIYE MPANGAJI"
Sidhani kama walikosea wanadamu wote asilimia 100% waaminio uwepo na muongozo wa huyu mungu wanaamini kuwa mola ndiye anayepanga mambo yote yanatokea katika dunia.

Wametutoka vigogo kadhaa msimu huu, Maalim Seif , Mzee Pombe Magufuli na kauli kama "YOTE NI MIPANGO YA MUNGU" zilishamiri sana katika vinywa vya wanaadamu vivyo hivyo hili ni jambo Endelevu na Desturi yetu kwamba likitokea jambo lolote liwe tata au la kawaida, kubwa au dogo basi Heshma ya Utendaji yote inabaki kwa Mungu huyu mungu mkuu
kwamba yeye ndiye mpangaji wa yote

Tunaamini
Kila Jambo hupangwa na Mungu mwenyewe.

Tukirejelea nyuma kidogo katika tukio moja , ambalo kidogo litanifanya niingie katika kundi la mapungufu kiuandishi baada ya kutumia kiambatanishi kimoja yaani kisa kutoka Upande mmoja wa dini ('Islam') hii ni kutokana na kukosa masimulizi ya kisa hiki katika upande wa dini zingine(ukristo) tofauti na Uislamu. Lakini hii haipangui lengo la Mada yetu kuu, inalenga pale pale katika kung'amua sintofahamu hii. katika pande zote. Si tunaamini Mungu ndiye mpangaji wa Yote.

Hii ni Hadithi ya mtume Muhammad (S.A.W) akielezea jinsi Nabii Musa yule aliyesumbuana na Farao kule Misri alivyokutana na Nabii Adam baba wa kizazi cha Wanaadamu Ulimwenguni.

Inasimuliwa

Nabii Muhammad (ﷺ) alisema,

"Adam na Musa walibishana wao kwa wao.

Musa akamwambia Adam.

" Ewe Adam! Wewe ni kipi kilikufanya ufukuzwe katika bustani ya Mwenyezi Mungu, kwanini ulivunja miadi ya mwenyezimungu (ukala tunda na mkeo ukafukuzwa peponi)"

Adam akamjibu

"Mwenyezimungu alikuwa ameiandika katika hatima yangu miaka kabla ya kuumbwa kwangu.

Mtume Muhammad anaelezea ya kuwa Adamu alimjibu Musa huku akimcheka ya kwamba kila kitu kilikuwa kimeshaandikwa kabla ya yeye kuumbwa.

Masimulizi haya yanaeleza namna Nabii Mussa alivyomuomba Mola wake amkutanishe na Nabii Adamu ili apate kumuuliza kilichomsibu ikafikia hatua ya yeye, kumuasi mola wake wake kwa kumfuata Ibilisi naye Adamu akajikuta yu Uchi kufuatia kula tunda.
Inaelezwa Mussa alipokutanishwa tu na Adamu alianza kumshushia lawama yakwamba kwanini alikula tunda mpaka akafukuzwa kule Eden akasababisha Wanaadamu waje kuishi mahali na sehemu zenye shida nyingi Duniani

Nabii adamu anamjibu nabii Musa ya kuwa "Hilo lilishaandikwa katika hatma za nabii Adam ya kwamba lazima litatokea.

Kama ni hivyo Kauli ya kusema Mola ni mpangaji wa yote haina Kipingamizi mara nyingi

Na hapa inatuonyesha yakwamba yote ilikuwa mipango ya Mungu ili mwanadamu apate kumcha/kumtii yeye, na wala asifate kwingineko.

SWALI.

Kwanini tunamlaumu Adamu na Shetani Ilhali ilikuwa ni mipango ya Mwenyezimungu?

i stand to be corrected
Na mwenyezimungu Mjuzi wa Yote

DaVinci XV
 
I am sorry and I beg to be corrected if there will be any conflict and misunderstanding in term of religious wing.
 
Hapo kuna ishu ya Yuda Iskarioti (Japo iko kwenye Ukristo tu). Kwa maelezo ya Yesu, ilikuwa tayari imepangwa asalitiwe ili afe. Lakini Petro katika matendo ya mitume anamlaumu Yuda vikali kwa kumsaliti na kugawa nafasi yake kwa mtu mwingine. Kwa mantiki hiyo Yuda anaonewa.
Aiseee hivi ,vitu vinafikirisha sana, kwahiyo hapa tunang'amua nini????
 
Mungu alipaswa kuadhibiwa adhabu kali sana
Aisee mkuu ,hapa anaadhibiwaje..... wakati yeye ndiye bingwa wa kuadhibu. kama anavyoahidi kumuadhibu huyo nyoka..na mkarimu wa kusamehe kama alivyowahurumia Adamu na Mkewe

Hapa kwa Mujibu wa Vitabu vyake
 
Aisee mkuu ,hapa anaadhibiwaje..... wakati yeye ndiye bingwa wa kuadhibu. kama anavyoahidi kumuadhibu huyo nyoka..na mkarimu wa kusamehe kama alivyowahurumia Adamu na Mkewe

Hapa kwa Mujibu wa Vitabu vyake

Ukiangalia masimulizi yake ameonekana akitumia silaha ya upanga kupambana na maadui, Kama angekuwepo hata bom lingemtosha
 
Uzi wa WAPAGANI naona mmeitana.

endeleeni kujadili ujinga wenu

Zab 53:1 SUV​

Mpumbavu amesema moyoni, Hakuna Mungu; Wametenda uovu wa ufisadi na kuchukiza, Hakuna atendaye mema.

Mt 11:25-26 SUV​

Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako.
 
Kwa mm mkristo naamini kwenye kitu kiitwacho "Mpango wa Uokovu"...(Plan of salvation).
Ambao unaanzia kule mbinguni kabla misingi ya ulimwengu bado haijawekwa.
Ambao wote tulikua kule na MUNGU lakini tulikua kwenye mfumo wa roho.(hatukua na miili).

Binadamu wote ambao wamezaliwa,walizaliwa na watakaozaliwa walikuwepo katika mfumo huo tajwa na moja ya roho zilizokuwepo ni Adam,mussa,lucifer,Yesu,mm,ww ndugu msomaji na kila mtu ambae ana mwili wa nyama na mifupa kwa sasa.

Ndo mana ilikua Rahisi kwa MUNGU kusema Jeremia utakua Nabii, fulani utakua hivi ni sababu tulikua nae na tulikua tunajifunza na kila mtu alikua ana potential zake.

Sio coincidence leo mtu anazaliwa anakua muimbaji mfano jide, rubi etc,au mtu anakua soccer player kama samatta na wengine wengi wenye vipaji tofauti tofauti.

To cut the long story short ni kwamba kwenye huu mpango kila kitu tulikubaliana na kilipangwa mfano Adam kukengeuka,yesu kusalitiwa,shetani kuasi, etc.

So MUNGU anajua kila kitu....sisi baada ya kuzaliwa tumepita kwenye kitu kiitwacho "Veil"..ambacho kime erase kumbukumbu zetu zote za kilichotokea kabla hatujazaliwa.
 
Kila mtu kulinganana na imani yake anaweza kutoa maoni mbali mbali.
Nami kwa imani yangu hio hadithi ya Musa kukutana na Adam sio hadithi halisi Bali ni tungo tu ambazo unazisoma ili kujifunza jambo fulani, sio lazima kisa hiko kiwe kimetokea moja kwa moja.

Ni kama hadithi na mifano ya Yesu sio yote vingine vilikua ni ngano tu.

Na hata kwenye biblia kuna hadithi ya sauli kukutana na samweli amba alikua amekwisha fariki zamani.
Hio hadithi wachambuzi wanasema haikua tukio la kweli Bali kiini macho.

Ni sawa na huo mfano wa Musa na Adam kunaweza kusiwe na uhalisia wowote ila kinapatikana funzo ya kwamba mungu anayajua yote yajayo yaliopo na yaliopita kutoka kwa viumbe wake wote.


Pamoja na hayo yoote lakini uwepo wa mwenyezi Mungu hakuna namna tunaweza kuukwepa, yanaweza kuwepo makosa mengi ya kiundishi , kitafsiti, kimapokeo nk , lakini Mungu yupo.
Bahati mbaya hivyo vitabu vyenye kuelezea uwepo wa Mungu vimejifunga havitaki kukosolewa Wala havitaki kurekebishwa, happy ndipo kwenye changamoto.

Maana akili ya miaka 1000 ilipota ilikuwepo kwa binadamu ni tofauti kubwa Sana na akiii ya leo.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Suala la Adam na Eva ni suala la hatma nusu ambayo inahitaji utendaji nusu ikamilike kuwa jinai.....Yani Adam na Eva walizaliwa na hiyo hatma lakini walipewa uwezo wa kuishinda hatma yao na wao wakashindwa kuishinda hatma ya kumsaliti Muumba wao.....

Maisha yetu wote yapo hivyo tunaumbwa na hatma zetu ziwe nzuri au mbaya.....mfano mtu anaumbwa na hatma ya kuwa kiongozi bora na baadae anakuwa kiongozi, lakini katika uongozi wake anakuwa muuaji na kinyume cha maadili ya uongozi na maandiko huyu mtu atakufa kifo kibaya au ataenda mahali pabaya sababu ameruhusu hatma mbaya nusu ishinde hatma yake nzuri nusu....

Hatma zetu ni saa na chungwa nusu, iwe kwa ubaya au uzuri na tunaishi kuitafuta nusu nzuri au nusu mhaya inayoweza kutuokoa au kutumaliza kabisa na hatna mbaya
 
Suala la Adam na Eva ni suala la hatma nusu ambayo inahitaji utendaji nusu ikamilike kuwa jinai.....Yani Adam na Eva walizaliwa na hiyo hatma lakini walipewa uwezo wa kuishinda hatma yao na wao wakashindwa kuishinda hatma ya kumsaliti Muumba wao.....

Maisha yetu wote yapo hivyo tunaumbwa na hatma zetu ziwe nzuri au mbaya.....mfano mtu anaumbwa na hatma ya kuwa kiongozi bora na baadae anakuwa kiongozi, lakini katika uongozi wake anakuwa muuaji na kinyume cha maadili ya uongozi na maandiko huyu mtu atakufa kifo kibaya au ataenda mahali pabaya sababu ameruhusu hatma mbaya nusu ishinde hatma yake nzuri nusu....

Hatma zetu ni saa na chungwa nusu, iwe kwa ubaya au uzuri na tunaishi kuitafuta nusu nzuri au nusu mhaya inayoweza kutuokoa au kutumaliza kabisa na hatna mbaya
Aisee sawah , mahitimisho yetu ni hatma iwe mbaya au njema

Tumekupata
 
Kila mtu kulinganana na imani yake anaweza kutoa maoni mbali mbali.
Nami kwa imani yangu hio hadithi ya Musa kukutana na Adam sio hadithi halisi Bali ni tungo tu ambazo unazisoma ili kujifunza jambo fulani, sio lazima kisa hiko kiwe kimetokea moja kwa moja.

Ni kama hadithi na mifano ya Yesu sio yote vingine vilikua ni ngano tu.

Na hata kwenye biblia kuna hadithi ya sauli kukutana na samweli amba alikua amekwisha fariki zamani.
Hio hadithi wachambuzi wanasema haikua tukio la kweli Bali kiini macho.

Ni sawa na huo mfano wa Musa na Adam kunaweza kusiwe na uhalisia wowote ila kinapatikana funzo ya kwamba mungu anayajua yote yajayo yaliopo na yaliopita kutoka kwa viumbe wake wote.


Pamoja na hayo yoote lakini uwepo wa mwenyezi Mungu hakuna namna tunaweza kuukwepa, yanaweza kuwepo makosa mengi ya kiundishi , kitafsiti, kimapokeo nk , lakini Mungu yupo.
Bahati mbaya hivyo vitabu vyenye kuelezea uwepo wa Mungu vimejifunga havitaki kukosolewa Wala havitaki kurekebishwa, happy ndipo kwenye changamoto.

Maana akili ya miaka 1000 ilipota ilikuwepo kwa binadamu ni tofauti kubwa Sana na akiii ya leo.



Sent using Jamii Forums mobile app
sawa
 
Back
Top Bottom