Etugrul Bey
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 6,514
- 15,247
Hakika binadamu ameshughulishwa Sana na wingi WA kutafuta Mali mpaka amesahau kesho itakuwaje,amesahau hakika hapa duniani yeye ni Msafiri na Mda wowote ataondoka.
Mwenyezi Mungu anatutaka tutafute dunia yetu na Akhera yetu pia,Kwa maana tupambane tupate ridhiki ya halali tupate Kula vya halali na kuvaa vya halali na kuwa na Maisha Bora kabisa.
Lakini
Wakati huo huo anatutaka tujiwekee hazina Bora ambayo itakuja kutufaa huko mbele ya safari baada ya kuondoka hapa duniani,kwani mwisho wa siku tutaenda katika maisha mengine nje ya dunia hii.
Kuna ujumbe mmoja wa utani unasemwa na watu lakini umebeba ujumbe mkubwa Sana Kwa mtu mwenye kufikiri hatima yake unasema hivi;
Je kama sadaka ndio hela ya Matumizi yako huko Akhera unadhani ingekuwezesha kuishi kwa mda gani?
Ni utani lakini kuna ujumbe Fulani, ebu jitafakari wewe binafsi unafikir kwa sadaka yako uliyotoa ungetoboa miaka mingapi au miezi mingapi?
Hakika wengi wetu kama tungekufa Leo basi tungekuja kuwa ombamba huko mbinguni kwani naamini kabisa hizo sadaka tulizo toa ni hafifu mno kutuwezesha kufikisha miezi mitatu.
Tuwekeze katika maisha yajayo ambayo wengi wetu tunaamini yapo kwa mujibu wa imani zetu na Dini zetu.
Mwenyezi Mungu anasema hakika mwanadamu amekula hasara mpaka anaingia Makaburini hakuna kheri yoyote aliyoitanguliza ambayo itakuja kumfaa huko Akhera.
Kwahiyo ndugu zangu fanya utakavyo fanya na tafuta Maisha utakavyo lakini mwisho wa siku Sisi ni mavumbi na tutarudi mavumbini Tu kwahiyo hatuna budi kujitayarishia hazina ambayo itakuja kutufaa huko mbele ya safari.
Walio tangulia wameshajua hatima Yao na laiti wangeweza kutupenyezea ujumbe basi wangetuambia:
Jamani Yale tulivyo ambiwa katika vitabu ni kweli na tumeyakuta huku msimdharau hata jambo moja!
Bahati mbaya wanashindwa kuwasiliana na Sisi na wanabakia kusema laiti walio bakia duniani wangejua hakika wangefanya Yale yanayo mpendeza Mwenyezi Mungu.
Kazi kwetu kufanya yale ambayo yatakuja kutufaa huko mbele ya safari.
Ni hayo Tu!
baby zu
Kazakh destroyer
adriz
Nurain
Akhi
Mwenyezi Mungu anatutaka tutafute dunia yetu na Akhera yetu pia,Kwa maana tupambane tupate ridhiki ya halali tupate Kula vya halali na kuvaa vya halali na kuwa na Maisha Bora kabisa.
Lakini
Wakati huo huo anatutaka tujiwekee hazina Bora ambayo itakuja kutufaa huko mbele ya safari baada ya kuondoka hapa duniani,kwani mwisho wa siku tutaenda katika maisha mengine nje ya dunia hii.
Kuna ujumbe mmoja wa utani unasemwa na watu lakini umebeba ujumbe mkubwa Sana Kwa mtu mwenye kufikiri hatima yake unasema hivi;
Je kama sadaka ndio hela ya Matumizi yako huko Akhera unadhani ingekuwezesha kuishi kwa mda gani?
Ni utani lakini kuna ujumbe Fulani, ebu jitafakari wewe binafsi unafikir kwa sadaka yako uliyotoa ungetoboa miaka mingapi au miezi mingapi?
Hakika wengi wetu kama tungekufa Leo basi tungekuja kuwa ombamba huko mbinguni kwani naamini kabisa hizo sadaka tulizo toa ni hafifu mno kutuwezesha kufikisha miezi mitatu.
Tuwekeze katika maisha yajayo ambayo wengi wetu tunaamini yapo kwa mujibu wa imani zetu na Dini zetu.
Mwenyezi Mungu anasema hakika mwanadamu amekula hasara mpaka anaingia Makaburini hakuna kheri yoyote aliyoitanguliza ambayo itakuja kumfaa huko Akhera.
Kwahiyo ndugu zangu fanya utakavyo fanya na tafuta Maisha utakavyo lakini mwisho wa siku Sisi ni mavumbi na tutarudi mavumbini Tu kwahiyo hatuna budi kujitayarishia hazina ambayo itakuja kutufaa huko mbele ya safari.
Walio tangulia wameshajua hatima Yao na laiti wangeweza kutupenyezea ujumbe basi wangetuambia:
Jamani Yale tulivyo ambiwa katika vitabu ni kweli na tumeyakuta huku msimdharau hata jambo moja!
Bahati mbaya wanashindwa kuwasiliana na Sisi na wanabakia kusema laiti walio bakia duniani wangejua hakika wangefanya Yale yanayo mpendeza Mwenyezi Mungu.
Kazi kwetu kufanya yale ambayo yatakuja kutufaa huko mbele ya safari.
Ni hayo Tu!
baby zu
Kazakh destroyer
adriz
Nurain
Akhi