Tunaipokea treni ya mchongoko kwa shingo upande, ni kama ile ya zamani imechongwa kimchongo

Tunaipokea treni ya mchongoko kwa shingo upande, ni kama ile ya zamani imechongwa kimchongo

Usanifu ni sanaa ya ubunifu!

Na ubunifu ni sayansi yenye vipimo ili kupata muonekano unaovutia. Katika hatua za utengenezaji huanza na michoro na mpangilio wa ndani (interior design)

Hii treni tuliyopokea tukiambiwa ni ya mchongoko. Ukitafuta ile curve ilivyo chongwa unaona kabisa ni mchongo ambao ni modified! Yaani ili niekeweke kirahisi natoa mfano huu.

Ili upate muonekano wa saloon car (mfano sura toyota crown) ni lazima usanifu kuanzia kwenye chassis (uchanja wa chini) ili ubalansi kimo cha siti, uonaji wa mbele, n.k haya yote huamua ufunge viti gani, boneti iwe saizi gani, injini ikae mkao gani n.k)

Lakini ukiichukua Noah au Hiace uichonge kupata muonekano wa Saloon car huwezi kuipata Lazima itagoma tu. Lazima igome kwasababu mgangilio wa awali wa viti na sakafu uko juu, hivyo jitihada za kuifyeka Hiace au Noah utabakia kwenye paa (Roof)

Ukiitazama treni yetu ni dhahili mboleshaji kaweka curve kuzunguka kichwa cha dereva, kale kadirisha ka ubavuni akamega kona moja ya juu!

Ukiendelea kuchunguza alivyoishusha ikamgomea maana kule mbele kabisa angepata engo kali kama mshale! Hivyo akaforce kibox na kuweka show kama toyota alphad new!

Wakati treni ya mchongoko Original kule mbele ile slope humalizikia kama YAI au ndege ndogo! Na ile shepu huwa inapatikana kwa kucurve juu na curve nyingine lazima itafutiwe chini zikutane kutokana na usanifu original!

Hii treni yetu mpya ukiitazama hata kama kipofu anaona kabisa haiko kama inavyotakiwa!

Lile umbo la Yai kule mbele ukiachilia kuongeza muonekano lakini hurahisisha penetration ya kuukata upepo hata matumizi ya Umeme/mafuta nguvu hupungua. Ndiyo maana ndege nazo ziko hivyo ili ziwe fasta.

Wamejitahidi kucurve kule chini wakaambulia sura ya alphad. Angalau linatembea wacha tulipokee tutapanda hivyohivyo kwa shingo upande. Huenda pesa yetu haitoshi kupata yale Original.

Hii ndiyo ile kwenye mechi wanaita unapigwa "home and away"
tatizo hamridhiki na chochote
 
Umenikumbusha zamani Tanga kulikuwa na basi likiitwa SHAKILA lilikuwa na umbo la mkate wa boflo
 
Kwa hii CCM usiamini kila kitu, watakuwa wamewaambia wachina waichoronge mbele ili kuridhisha watanzania, huku wakijua fika ndio tunachotaka kuona, ila specifics zinabaki pale pale, 80kph...

Nchi ngumu hii under CCM!!
Hatari sana

CCM ni wapigaji sana

Cc; Lucas Mwashambwa
 
Achakupotosha,

Chuma iyooapo, km hauelewi nenda youtube
ITX%20train.jpg
ITX..jpg
 
Siwezi kuunganisha koment yangu ya zamani kwenye uzi huu lakini nilikomenti walipoleta vile vichwa vya kwanza nikawashauri TRC wasihangaike na maneno ya Watanzania, kwa kuwa baadhi yao wanapenda kufuata mkumbo.

Nikasema dawa ni TRC kurudi kiwandani na kumodify vile vichwa na kuwa mchongoko kwa sababu watu wengine wamekaririshwa vichwa mchongoko na siyo kuangalia ni kwa namna gani treni ina kasi

Kwahiyo, hapo dawa imepatikana, vichwa mchongoko ndiyo hivyo, kazi imeisha. Tuseme lingine sasa!

Yote kwa yote, kama ambavyo ni ngumu kwa Watanzania kununua magari zero kilomita ya miaka ya karibuni, nahisi ndivyo ilivyo kwa serikali za nchi zinazoendelea mfano Tanzania kushindwa kununua treni toleo jipya, zero kilomita. Ni gharama sana.

Mbona watu wananunua magari ya mitumba na yakifika bongo yanatembea tu na ndani ni mazuri, iweje tushangae treni ya mtumba?
 
Siwezi kuunganisha koment yangu ya zamani kwenye uzi huu lakini nilikomenti walipoleta vile vichwa vya kwanza nikawashauri TRC wasihangaike na maneno ya Watanzania, kwa kuwa baadhi yao wanapenda kufuata mkumbo.

Nikasema dawa ni TRC kurudi kiwandani na kumodify vile vichwa na kuwa mchongoko kwa sababu watu wengine wamekaririshwa vichwa mchongoko na siyo kuangalia ni kwa namna gani treni ina kasi

Kwahiyo, hapo dawa imepatikana, vichwa mchongoko ndiyo hivyo, kazi imeisha. Tuseme lingine sasa!

Yote kwa yote, kama ambavyo ni ngumu kwa Watanzania kununua magari zero kilomita ya miaka ya karibuni, nahisi ndivyo ilivyo kwa serikali za nchi zinazoendelea mfano Tanzania kushindwa kununua treni toleo jipya, zero kilomita. Ni gharama sana.

Mbona watu wananunua magari ya mitumba na yakifika bongo yanatembea tu na ndani ni mazuri, iweje tushangae treni ya mtumba?
Umepita mule mule komredi! Hongera
 
Kichwa kizima kimekaa kimchongo mchongo hivi. Ni kama kiliungwa ungwa na kupigwa rangi kisanii sanii.
 
Ni ngongongo iliyochangamka
Wewe utakuwa unaishi/umeishi maeneo yenye reli ya TAZARA bila shaka. Maana lile treni la mizigo huitwa kwa jina hili na wenyeji wanaoishi kando ya hiyo reli.
 
Back
Top Bottom