Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,843
- 31,057
Siku ya Jumanne ya terehe 23/06/2020 Wananchi nchini Malawi, walipiga kura katika uchaguzi wa marudio, baada ya yale ya awali yaliyompa ushindi Rais aliyeko madarakani, Peter Mutharika, kutenguliwa na Mahakama ya kikatiba nchini humo.
Tukumbuke kuwa Peter Mutharika alitangazwa na Tume ya Taifa nchini humo kuwa alipata ushindi mwembamba, katika uchaguzi mkuu uliofanyika nchini humo, mwezi Mei mwaka 2019, kwa kumshinda mpinzani wake mkubwa, Lazarus Chakwera, wa muungano wa upinzani, wa kupata ushindi wa asilimia 38.
Baada ya matokeo hayo kutangazwa na Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi ya nchi hiyo, Jane Mansah, kuliibuka maandamano ya wananchi wa nchi nzima, wakidai kuwa Tume ya Taifa ya uchaguzi, ilifanya udanganyifu kwa kumtangaza Rais aliyeko madarakani, Peter Mutharika, kuwa ndiye aliyeshinda uchaguzi huo.
Hata hivyo Muungano wa Upinzani nchini humo ulifungua kesi katika mahakama ya kikatiba kupinga ushindi huo uliotangazwa wa Peter Mutharika.
Hatimaye mwezi Februari ya mwaka huu, mahakama hiyo ya kikatiba, ilifanya uamuzi wa kihistoria, kwa kutengua matokeo hayo ya uchaguzi na kuamuru kuwa uchaguzi huo urudiwe, tena kwa kutumia sheria mpya ya uchaguzi huo kwa mgombea wa kiti cha Urais, ni lazima apate ushindi wa zaidi ya asilimia 50, kinyume na sheria ya hapo kabla ambayo ilikuwa ikimtaka mgombea wa kiti cha Rais, atangazwe mshindi, kwa ushindi wowote, hata ule wa (simple majority) ambayo ni chini ya asilimia 50 ya wapiga kura nchini huko.
Hata hivyo kwa matokeo ambayo yanaendelea kutangazwa na vyombo vya habari vya serikali ya Malawi, ni kuwa hadi hivi sasa mgombea wa upinzani, Mchungaji Lazarus Chakwera, anaongoza kwa kupata kura asilimia 59 ya kura zote zilizohesabiwa hadi hivi sasa, akifuatiwa kwa mbali sana na Peter Mutharika, ambaye ndiye Rais aliyoko madarakani hadi hivi sasa, ameambulia kura asilimia 38 pekee!
Kama Taifa la Tanzania tunajifunza nini kwa matokeo hayo ya uchaguzi mkuu wa Malawi?
1. Ni lazima kiwepo kipengele kwenye Katiba ya nchi, ambapo matokeo ya Urais yanaweza kupingwa mahakamani
2. Kuwepo hapa nchini kwa mahakama ya kikatiba, ambayo itaweza kusikiliza kesi za kupinga matokeo ya Urais kwenye uchaguzi mkuu, iwapo yatajitokeza
3. Ni lazima tuwe na Tume huru ya uchaguzi wa Taifa na ionekane katika muundo wake kuwa ni huru kweli kweli
4. Kuwepo na Muungano ya vyama vya upinzani usiokuwa na masharti magumu kama yalivyo nchini kwetu
Ninaamini yakifanyika marekebisho hayo muhimu katika Katiba ya nchi yetu na katika mifumo ya chaguzi zetu, ndipo tutakapojidai kweli tuna demokrasia iliyokomaa nchini mwetu na itatuepushia nchi yetu isiingie kwenye machafuko yanayoweza kuhatarisha maisha ya wananchi wetu.
Mungu ibariki Tanzania
Tukumbuke kuwa Peter Mutharika alitangazwa na Tume ya Taifa nchini humo kuwa alipata ushindi mwembamba, katika uchaguzi mkuu uliofanyika nchini humo, mwezi Mei mwaka 2019, kwa kumshinda mpinzani wake mkubwa, Lazarus Chakwera, wa muungano wa upinzani, wa kupata ushindi wa asilimia 38.
Baada ya matokeo hayo kutangazwa na Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi ya nchi hiyo, Jane Mansah, kuliibuka maandamano ya wananchi wa nchi nzima, wakidai kuwa Tume ya Taifa ya uchaguzi, ilifanya udanganyifu kwa kumtangaza Rais aliyeko madarakani, Peter Mutharika, kuwa ndiye aliyeshinda uchaguzi huo.
Hata hivyo Muungano wa Upinzani nchini humo ulifungua kesi katika mahakama ya kikatiba kupinga ushindi huo uliotangazwa wa Peter Mutharika.
Hatimaye mwezi Februari ya mwaka huu, mahakama hiyo ya kikatiba, ilifanya uamuzi wa kihistoria, kwa kutengua matokeo hayo ya uchaguzi na kuamuru kuwa uchaguzi huo urudiwe, tena kwa kutumia sheria mpya ya uchaguzi huo kwa mgombea wa kiti cha Urais, ni lazima apate ushindi wa zaidi ya asilimia 50, kinyume na sheria ya hapo kabla ambayo ilikuwa ikimtaka mgombea wa kiti cha Rais, atangazwe mshindi, kwa ushindi wowote, hata ule wa (simple majority) ambayo ni chini ya asilimia 50 ya wapiga kura nchini huko.
Hata hivyo kwa matokeo ambayo yanaendelea kutangazwa na vyombo vya habari vya serikali ya Malawi, ni kuwa hadi hivi sasa mgombea wa upinzani, Mchungaji Lazarus Chakwera, anaongoza kwa kupata kura asilimia 59 ya kura zote zilizohesabiwa hadi hivi sasa, akifuatiwa kwa mbali sana na Peter Mutharika, ambaye ndiye Rais aliyoko madarakani hadi hivi sasa, ameambulia kura asilimia 38 pekee!
Kama Taifa la Tanzania tunajifunza nini kwa matokeo hayo ya uchaguzi mkuu wa Malawi?
1. Ni lazima kiwepo kipengele kwenye Katiba ya nchi, ambapo matokeo ya Urais yanaweza kupingwa mahakamani
2. Kuwepo hapa nchini kwa mahakama ya kikatiba, ambayo itaweza kusikiliza kesi za kupinga matokeo ya Urais kwenye uchaguzi mkuu, iwapo yatajitokeza
3. Ni lazima tuwe na Tume huru ya uchaguzi wa Taifa na ionekane katika muundo wake kuwa ni huru kweli kweli
4. Kuwepo na Muungano ya vyama vya upinzani usiokuwa na masharti magumu kama yalivyo nchini kwetu
Ninaamini yakifanyika marekebisho hayo muhimu katika Katiba ya nchi yetu na katika mifumo ya chaguzi zetu, ndipo tutakapojidai kweli tuna demokrasia iliyokomaa nchini mwetu na itatuepushia nchi yetu isiingie kwenye machafuko yanayoweza kuhatarisha maisha ya wananchi wetu.
Mungu ibariki Tanzania