Tunajua Unalazimisha huku Kujipendekeza Kwake ili mwakani uwe Mwandamizi katika Kuzunguka nae nchi nzima wakati wa Kampeni

Tunajua Unalazimisha huku Kujipendekeza Kwake ili mwakani uwe Mwandamizi katika Kuzunguka nae nchi nzima wakati wa Kampeni

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
DAR ES SALAAM; Msanii wa muziki wa kizazi kipya Faustina Charles ‘Nandy’, ameibuka kwenye mkutano na wanahabari akiwa ametinga vazi analosema ni kama mtindo wa nguo za Rais Samia Suluhu Hassan.

Nandy aliyekuja kuzungumzia tamasha lake litakalofanyika Mwanza kesho, alikuwa amevaa ushungi mweusi na vazi la suti nyekundu aina ya Kaunda.

Baada ya kuulizwa kuhusu uvaaji wa vazi hilo ikiwa ni mara yake ya kwanza akiwa katika muonekano huo, amesema anavutiwa sana na uvaaji huo wa Rais Samia, kiasi cha yeye kuamua kuiga akisema ni vazi zuri kwa wanawake.

“Rais ametupa vazi letu la kipekee ambalo ni zuri na wanawake kwa sasa wanavaa, nikaona na mimi niwakilishe. Nitaenda kwenye tamasha la Nandy kisamia,”amesema. Mwingine aliyevaa vazi kama hilo ni Yasirun Yasin ‘Yammi’

Ametaja baadhi ya wasanii watakaotumbuiza kwenye tamasha hilo ni Maya Christinah Xichavo ‘Sho Madjozi’ kutoka Afrika Kusini, William Lyimo ‘Billnas’, Saraphina Michael ‘Saraphina’, Stamina Sharobwenzi ‘Stamina’, Young Lunya na Yasirun Yasin ‘Yammi’

Amesema katika tamasha hilo litakalofanyika kwenye viwanja vya Elevante atatambulisha msanii mwingine wa kimataifa kama ‘surprise’.

Kwa upande wake William Lyimo ‘Billnas’, amesema amejipanga vizuri kufanya kazi sio kama mume bali msanii mwenye mkataba kama wengine na atahakikisha anaimba na bendi.

Chanzo: habarileotz

Ameanza Kuvaa tokea alipokuwa Makamu wa Rais mbona huko nyuma hatutukuona Ukijipendekeza Kwake na Kumsifia juu ya Uvaaji wake?

Hovyoo na ndiyo maana Unaishi kwa Matumaini.
 
Acheni wasanii wapambanie ugali wao, wenyewe ni binadamu kama sisi tunavyopambania kazi za maboss zetu na kutafuta madili ili kuongeza kipato,
Unataka wajifanye chadema biashara zao zianze kufungiwa wakati mkiambiwa mnunue wimbo mmoja kwa jero hamna atakayefanya hivo
 
Acheni wasanii wapambanie ugali wao, wenyewe ni binadamu kama sisi tunavyopambania kazi za maboss zetu na kutafuta madili ili kuongeza kipato,
Unataka wajifanye chadema biashara zao zianze kufungiwa wakati mkiambiwa mnunue wimbo mmoja kwa jero hamna atakayefanya hivo
Kuna muda kama naona ni muda sasa kila raia ajitafute kimpango wake hii ukitaka kuibadilisha watu wanakubadilsha jina
 
Ila Nandy inaonekana ni mkatili na ana masimango mno.

Nina hakika huyu Yammy anavumilia mengi mno.

Hii video ya jinsi anavyomuangalia msanii wake kwa dharau imeniaminisha kuwa hata yule dada wake wa kazi anapitia manyanyaso mengi toka kwa huyu Nandy. Ana husda ya dhahiri.
 
Ila Nandy inaonekana ni mkatili na ana masimango mno.

Nina hakika huyu Yammy anavumilia mengi mno.

Hii video ya jinsi anavyomuangalia msanii wake kwa dharau imeniaminisha kuwa hata yule dada wake wa kazi anapitia manyanyaso mengi toka kwa huyu Nandy. Ana husda ya dhahiri.
View attachment 3095046
Anaonekana ni mchoyo, mroho na bahili sana, na kina nyodo na mashavu yake kama paka wa ikulu
 
Anaonekana ni mchoyo, mroho na bahili sana, na kina nyodo na mashavu yake kama paka wa ikulu
Basi inatosha Bibiee,,, Punguza kisukari hicho kitakumaliza mapema kama unadili na mambo madogomadogo kama hayo.
 
Back
Top Bottom