Tunakosea tunaposema mazuri aliyofanya hayati Julius Nyerere huku hatusemi mabaya aliyofanya na yametugharimu kama taifa

Tunakosea tunaposema mazuri aliyofanya hayati Julius Nyerere huku hatusemi mabaya aliyofanya na yametugharimu kama taifa

Kweli alipambana akasomesha wananchi wake na akahakikisha kuwa taifa linakuwa na umoja na mshikano.

Lakini ukweli kuwa aliharibu uchumi wa taifa na kuliacha masikini huwa hauwekwi wazi.

Hayati Nyerere alisahau kupambania uchumi wa taifa lake. Akabaki kupigana vita kuzikomboa Uganda, Zimbabwe na Mosambiqui bila kusahau Afrika kusini.

Vita vya ukombozi alivyoshiriki vilisababisha taifa kubakia kuwa masikini mpaka leo hii.
Mada nyingine ni za ajabu kweli: Kushiriki katika ukombozi limekuwa kosa? Kama nchi imeshindwa kutumia turufu ya ushiriki huo kunufaika, hilo kosa la Mwalimu Nyerere?

Na huo uchumi unaosema aliuharibu, ilikuwa lini ulipokuwa mzuri hadi uharibiwe. Nchi zipi zilizokuwa zinafanana na Tanzania ambazo unaweza kutolea kama mfano wa uchumi ambao haukuharibiwa?
 
Mkuu huna data sahihi wewe, wasema hakukuwa na viwanda wala chuo kikuu???
Hebu tuwekee "data sahihi" ulizonazo wewe, mkuu Allency!

Yaani hata kujuwa Chuo Kikuu inakuwa shida?
 
Biblia inasema mpende jirani yako. Tumemsaheme alitenda vema kuliko kuiba na kunemeesha familia yake.

Hata kukataa kuitwa mh. Nyerere bali Mwalimu ni sadaka yakini.
 
Nyerere aliacha viwanda je marais waliofuata waliviendeleza? Zaidi ya kuuza mashirika ya umma na ufisadi wa kutisha wakafanya kina mkapa.
 
Kweli alipambana akasomesha wananchi wake na akahakikisha kuwa taifa linakuwa na umoja na mshikano.

Lakini ukweli kuwa aliharibu uchumi wa taifa na kuliacha masikini huwa hauwekwi wazi.

Hayati Nyerere alisahau kupambania uchumi wa taifa lake. Akabaki kupigana vita kuzikomboa Uganda, Zimbabwe na Mosambiqui bila kusahau Afrika kusini.

Vita vya ukombozi alivyoshiriki vilisababisha taifa kubakia kuwa masikini mpaka leo hii.
Yeye alifanya kwa nafasi yake katika harakati za ukombozi wa nchi za Afrika akaondoka, je sisi tuliobaki tumelifanyia nini Taifa liweze kuendelea kama siyo kufikiria kuiba tu
 
Kweli alipambana akasomesha wananchi wake na akahakikisha kuwa taifa linakuwa na umoja na mshikano.

Lakini ukweli kuwa aliharibu uchumi wa taifa na kuliacha masikini huwa hauwekwi wazi.

Hayati Nyerere alisahau kupambania uchumi wa taifa lake. Akabaki kupigana vita kuzikomboa Uganda, Zimbabwe na Mosambiqui bila kusahau Afrika kusini.

Vita vya ukombozi alivyoshiriki vilisababisha taifa kubakia kuwa masikini mpaka leo hii.
Nyerere ni marehemu anayeogopwa hadi leo..

Ingawa kwa mazingira ya wakati huo si blame chochote alijitahidi sana. Sema alikosa washauri wazuri zaidizadi alizungukwa na machawa..
 
Wakati Mwalimu alikaa hadi foleni na Marais wengine wanakalia viti vya kanisani kwa adabu, kuna Paka special linasafirisha na kukalia kiti maalum👇🐒🐒🐒
ApfOS.png
AAq4U0.jpeg
ADPZA.png
YAMVHzi.jpeg
 
Na tukishasema hayo mabaya yatatuvusha hapa tulipo kwenda nchi ya ahadi?
Tuwe na Utamaduni wa kusema mazuri na mabaya ya mtu mwanadamu sio kumlamba makalio tu kwa nyimbo na ngonjera.
 
Kabla ya kusema Nyerere aliharibu uchumi jiuluze wewe binafsi, baba na babu yako wamechangiaje kukuza uchumi wa nchi hii? Ungechambua kwanza data halafu data hizo zikuonyeshe kuwa uchumi aliharibu.

Wakati Nyerere anachukua nchi hii haikuwa na chuo kikuu, haikuwa na madaktari wala mainjinia, haikuwa na viwanda lakini yeye alijenga vitu hivyo na vingine vingi. Nyerere alisomesha watoto bure hadi university tena wakati ambapo wazazi wengi walikuwa hawataki watoto wao wasome. Alijenga vyanzo vya umeme na alitu.mia pesa za mazao tu, madini alisema tusichimbe kwanza hadi watu wetu wasome ili tuyasimamie vizuri halafu wewe unaibuka unasemq aliharibu ucbumi kwa sababu pengine unataka dezo. Nyerere ameondoka madarakani miaka 38 iliyopita lakini failure zenu una.mtupia yeye. Wakati wa Nyerere hakuna mtu aliyetaka ardhi ya kulima akakosa lakini leo hii kuna mamilioni ya wakulima wadogo hawana ardhii ya kulima kwa kunyang'anywa.

Chuo kikuu kilianza kama sehemu ya College of London mwaka 1961. Nyerere alikikuta hicho chuo kikuu

 
Back
Top Bottom