Zanzibar 2020 Tunakubaliana na maridhiano, lakini Maalimu Seif na ACT Wazalendo lazima muwajibu Watanzania haya

Zanzibar 2020 Tunakubaliana na maridhiano, lakini Maalimu Seif na ACT Wazalendo lazima muwajibu Watanzania haya

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2010
Posts
17,005
Reaction score
20,425
Naomba nichangie kidogo kwa hatua iliyofikiwa leo kwa Maalim Seif kuingia katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Kwanza niseme mimi ni muumini wa maridhiano na ninaunga mkono "dhana" ya maridhiano iliyofikiwa leo pale Zanzibar.

Lakini ninapinga maridhiano haya yasiyo weka wazi msingi wa Maridhiano. Ninasema haya kwakuwa hadi sasa ACT na CCM hawajatueleza msingi wa maridhiano haya ni nini na hawajatuambia matunda yamaridhiano ya nyuma nini na kitendo cha leo kuweko maridhiano tena ni tafsiri ya kuwa maridhiano ya nyuma hayakuzaa matunda.

Nimesikiliza hotuba ya Maalim Seif leo, ni nzuri lakini haijajibu hoja za msingi za sisi tunaohoji msingi wa maridhiano haya. Imekuwa ni hotuba ya jumla zaidi inayo tulazimisha tufute machozi bila kutueleza kuwa kesho hatutalia kwasababu ya hili na lile.

Moja ya kichaka cha hoja wanachojificha wanaotetea ACT kujiunga na CCM ni hiki kinachoitwa "Siasa za Zanzibar zina namna yake". Hivyo hata tukihoji kwamba sababu zilizofanya 2015 wagomee zimetatuliwa ndipo wameingia tena au laaa? Wao wanatuziba kwa kujificha kwenye kichaka kinachoitwa historia ya siasa za Zanzibar.

Tumehoji hapa kwamba ni makubaliano gani ambayo ACT na CCM wameyaweka mezani hadi kufikiwa maridhiano ya leo ili kesho yasijirudie haya? Bado hatujibiwi tunarudishwa kwenye kichaka kanakwamba sisi hatujui historia ya Zanzibar.

Mfano Chadema imeweka mezani msingi wa maridhiano ya kitaifa kati yake na CCM ambayo ni 1. Kutambua kuwa uchaguzi ulikuwa batili, 2. Kuundwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi, 3. Mchakato wa Katiba Mpya ya Warioba kuendelea

Pengine kuna wanachoshindwa kusema wazi kuwa maslahi ya Maalim na Wenzake yamezingatiwa kuliko malengo ya Wazanzibar ya kupata nchi yao ambao ndio msingi ulioasisiwa na CUF ya Maalim. Nani leo mtetezi wa Wazanzibar??

Jibu liko Pemba na Unguja!

_______________

Nakukumbusha, ni mwezi wa Sikukuu, Watu watano watapata ZAWADI ya kitabu cha Ujasusi kwa 20,000 tu popote ulipo badala ya 80,000.

Lipia 20,000/= kwa

TigoPesa 0715865544
M-Pesa 0755865544
Airtel Money 0788887887
HaloPesa 0624452045
(Yericko Nyerere)

Tuma majina yako na ulipo

(Dar ni free delivery)

Nje ya Dar nauli 8,000/=

Instagram Follow @yerickonyerere

IMG-20201208-WA0237.jpg
 
Msingi wa uanzishwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa ilikuwa ni nini?

CCM na ACT-Wazalendo walichofanya ni kutimiza takwa la Katiba ya Zanzibar 1984.

Kama ndani ya katiba kuna maridhiano basi walichofanya ni kutekeleza kilichoko ndani ya katiba.

Inanishangaza ulipoandika ''Mfano Chadema imeweka mezani msingi wa maridhiano ya kitaifa kati yake na CCM ambayo ni 1. Kutambua kuwa uchaguzi ulikuwa batili, 2. Kuundwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi, 3. Mchakato wa Katiba Mpya ya Warioba kuendelea''

CHADEMA mnataka maridhiano na nani? Kwa lipi? Kwa msingi wa katiba ipi?
Katiba ya Tanzania inasema, the winner takes all. Kwa Tanzania bara uchaguzi umeisha!

CHADEMA wanatakiwa waishi na wakati na sio matamanio hewa!

Ninajua baada ya muda CHADEMA wataanza kupokea ruzuku za serikali lakini pia watapeleka wabunge wa viti maalum bungeni hata kama sio kina Mdee na kundi lake!
 
Msingi wa uanzishwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa ilikuwa ni nini?

CCM na ACT-Wazalendo walichofanya ni kutimiza takwa la Katiba ya Zanzibar 1984...
Mkuu katiba iliweka utaratibu baada ya maridhiano sio kabla.

Utaratubu wa kikatiba sio maridhiano bali ni sheria.

Msingi wa hoja hapa ni maridhiano bada ya kuvurugwa uchaguzi ambako ACT waliitangazia dunia. Na hoja ya msingi hapa ni je wanaingia katika takwa la kisheria kwa msingi upi ambao hautaleta manung'uniko tena 2025?

Zingatia takwa la kikatiba ni mshindi wa pili kuingia katika serikali.. yaani ACT wangetangazwa washindi baada ya kishinda, Mwinyi angekuwa Makamu wa Rais.

Katiba haijasema Maalim awe makamu tu, bali mshindi wa pili. Haya ndo maswali ya msingi, watwambie walifanya analysis ya mafanikio ya SUK ya mwaka 2010 na changamoto zake?
 
Chadema na siasa zenu kali mtaishia mitandaoni, wanasiasa makini hutanguliza maslahi mapana ya nchi. Kwa akili zenu hizi mtakosa vyote.Ndiyo maana HAlima & co wamewatosa
 
Chadema mnakera sana, Hongera Halima & co kwa kujitambua na kutanguliza tanzania [emoji1241] kwanza
 
Who is yeriko by the way??🤔🤔 hayupo wakukujibu maswali yako mkuu, cha msingi poleni wahanga
 
Kumekuwa na mapenzi makubwa ya Katiba kipindi hiki. Wanaowatetea wabunge wa COVID19 wananukuu katiba, wanaomtetea Maalim Seifu nao wananukuu katiba.

Je mapenzi haya ya Katiba yataendelea kwa vifungu vyote kwa mfano uwepo wa vyama vingi, haki ya kuandamana, haki ya kupewa dhamana kwa mshtakiwa et cetera et cetera!
 
Msingi wa uanzishwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa ilikuwa ni nini?

CCM na ACT-Wazalendo walichofanya ni kutimiza takwa la Katiba ya Zanzibar 1984...
Mkiambiwa CCM hamna akili mkubali sio tusi ndivyo mlivyo

Hivi wewe unaweza kukutana tu na mtu barabarani mkariadhiana kwenda kula chakula cha mchana pamoja?

Bila ya kuwa na sababu ya msingi itayo pelekea kwenda kula chakula pamoja?

Jibu ni kuwa lazima kutakuwa na jambo fulani litakalo pelekea tukio hilo na huo ndio msingi wa maridhiano ...

Unaposema neno maridhiano lazima lije swali mmeridhiana nini au maridhiano ya nini? Jibu lake ndio litakua msingi wa maridhiano hayo.

Hivyo basi ili maridhiano yawepo lazima viwepo vitu mtakavyo ridhiana kwa pande zote husika na lazima vitu hivyo viwepo kabla ya maridhiano yenyewe

Bogus ndio mana kutwa mnaletewa wapinzani kushika uongozi CCM ninmapimbi kwelikweli
 
CHADEMA mnazidi kupotea, mnazidi kupoteza uhalali na kukubalika kisiasa. Watu huwa hawaishi kwa uhasama miaka yote ingawa uhasama wenu ni wa kimaslahi pia.

Wazanzibari wameona hawawezi kuishi kwa kununiana wakati wanaweza kuunganisha nguvu na kujenga nchi yenye kufanya shughuli za kimaendeleo zenye kupiga hatua haraka.

CHADEMA mnayo changamoto ya kupata uongozi mpya wenye maono mapya kabisa, huu wa sasa umeshapoteza muelekeo.
 
Mkiambiwa CCM hamna akili mkubali sio tusi ndivyo mlivyo

Hivi wewe unaweza kukutana tu na mtu barabarani mkariadhiana kwenda kula chakula cha mchana pamoja?.....
Maalim ni mzee wa miaka 77 mnataka aendelee kuishi kwa uhasama mpaka lini?.

Tafuteni kiongozi mpya Mbowe keshashindwa mazima.
 
Back
Top Bottom