Kiongozi mkuu2020
JF-Expert Member
- Aug 8, 2020
- 1,748
- 998
Baaada ya wapinzaniii kuishiwa hoja, kwa sasa tumebakiwa na vyama vya ubishi na wanachama wote, mumebakiwa na ubishi tu.Mkuu katiba iliweka utaratibu baada ya maridhiano sio kabla.
Utaratubu wa kikatiba sio maridhiano bali ni sheria...
Tupo wengi sana kwa hili halikubaliki kabisa,lkn siku zote nimekuwa nikisema kuwa upinzani wa Zitto unatia mashaka sana hapa Tanzania.Mimi siungi mkono maridhiano hayo na wala sitayaunga mkono hata nikiwekewa bunduki kichwani .
Liwalo na liwe
Walichokifanya ACT hakina tofauti na walichofanya kina Mdee na kundi lakeMkuu katiba iliweka utaratibu baada ya maridhiano sio kabla.
Utaratubu wa kikatiba sio maridhiano bali ni sheria....
Aliye mtosa mwenzake ni yupi kati ya Mdee na CDM? Cdm ni taasisi kubwa kuliko hao wachumia matumbo yao kina Mdee na tushawafukuza na kuwavua uanachama.Chadema na siasa zenu kali mtaishia mitandaoni, wanasiasa makini hutanguliza maslahi mapana ya nchi.Kwa akili zenu hizi mtakosa vyote.Ndiyo maana HAlima & co wamewatosa
Akili za kimbulura utazijua tuChadema mnakera sana, Hongera Halima & co kwa kujitambua na kutanguliza tanzania [emoji1241] kwanza
Wewe ni sawa na kiroboto tu kwa Yeriko.Who is yeriko by the way??[emoji848][emoji848] hayupo wakukujibu maswali yako mkuu, cha msingi poleni wahanga
Hongera sana kwa comment yenye uzito unaojitoshelezaMkiambiwa CCM hamna akili mkubali sio tusi ndivyo mlivyo
Hivi wewe unaweza kukutana tu na mtu barabarani mkariadhiana kwenda kula chakula cha mchana pamoja?
Bila ya kuwa na sababu ya msingi itayo pelekea kwenda kula chakula pamoja ?
Jibu ni kuwa lazima kutakuwa na jambo fulani litakalo pelekea tukio hilo na huo ndio msingi wa maridhiano ...
Unaposema neno maridhiano lazima lije swali mmeridhiana nini au maridhiano ya nini? Jibu lake ndio litakua msingi wa maridhiano hayo
Hivyo basi ili maridhiano yawepo lazima viwepo vitu mtakavyo ridhiana kwa pande zote husika na lazima vitu hivyo viwepo kabla ya maridhiano yenyewe
Bogus ndio mana kutwa mnaletewa wapinzani kushika uongozi CCM ninmapimbi kwelikweli
Wewe una nini?kuanzia hapa dsm hadi kwenu mwandiga una nini cha kujivunia?Kwani we Nani kwanza Unalipi hasa
Yaani Hata Nyuma ya Mtaa wenu hawakufahamu
Mnajipa Ujiko tu kumbe Makopo Matupu
Nivizuri sasa watanzania ndiyo watamjua vema Zitto kuwa yeye anatanguliza tumbo lake mbele na maslahi ya watanzania ni baada ya yeye kushiba.Zitto Kabwe , Maalim Seif na Act Wazalendo hata uwape miaka mitano hawana majibu ya haya maswali na walichokifanya zaidi ya usaliti .
Hauna ujuwalo wewe zaidi ya kupalilia mrija wako usizibweCHADEMA mnazidi kupotea, mnazidi kupoteza uhalali na kukubalika kisiasa. Watu huwa hawaishi kwa uhasama miaka yote ingawa uhasama wenu ni wa kimaslahi pia.
Wazanzibari wameona hawawezi kuishi kwa kununiana wakati wanaweza kuunganisha nguvu na kujenga nchi yenye kufanya shughuli za kimaendeleo zenye kupiga hatua haraka.
CHADEMA mnayo changamoto ya kupata uongozi mpya wenye maono mapya kabisa, huu wa sasa umeshapoteza muelekeo.
Mbowe hatoki cdm mkitaka nendeni mkanywe sumu maana hamna faida kwa taifa hili.Maalim ni mzee wa miaka 77 mnataka aendelee kuishi kwa uhasama mpaka lini?.
Tafuteni kiongozi mpya Mbowe keshashindwa mazima.
Naona sasa mkuu nawe umeligundua hilo ingawa ulikuwa upande huoHakuna maridhiano pale kuna compliance ya ACT kwa matakwa ya CCM
Unaota sana baada ya kulewa mbandule wakati huo msosi wenyewe haupoCHADEMA wasipokuwa makini ndio biashara yao imekwisha. Yale yale ya kina TLP na NCCR Mageuzi.
we endelea tu kulamba miguu tu ta wanaume😂😂 mshahara wake unaufaham lakn ??Wewe ni sawa na kiroboto tu kwa Yeriko.
Teh teh teh 🤣 kwani mkuu hata usipounga mkono kwani ni tatizo kwao?Mimi siungi mkono maridhiano hayo na wala sitayaunga mkono hata nikiwekewa bunduki kichwani .
Liwalo na liwe
Kila chama kina aina yake ya maridhiano, hayo maridhiano ambayo nyie chadema mnayataka hayawezi kutokea until Jesus comes backNaomba nichangie kidogo kwa hatua iliyofikiwa leo kwa Maalim Seif kuingia katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Kwanza niseme mimi ni muumini wa maridhiano na ninaunga mkono "dhana" ya maridhiano iliyofikiwa leo pale Zanzibar.
Lakini ninapinga maridhiano haya yasiyo weka wazi msingi wa Maridhiano. Ninasema haya kwakuwa hadi sasa ACT na CCM hawajatueleza msingi wa maridhiano haya ni nini na hawajatuambia matunda yamaridhiano ya nyuma nini na kitendo cha leo kuweko maridhiano tena ni tafsiri ya kuwa maridhiano ya nyuma hayakuzaa matunda.
Nimesikiliza hotuba ya Maalim Seif leo, ni nzuri lakini haijajibu hoja za msingi za sisi tunaohoji msingi wa maridhiano haya. Imekuwa ni hotuba ya jumla zaidi inayo tulazimisha tufute machozi bila kutueleza kuwa kesho hatutalia kwasababu ya hili na lile.
Moja ya kichaka cha hoja wanachojificha wanaotetea ACT kujiunga na CCM ni hiki kinachoitwa "Siasa za Zanzibar zina namna yake". Hivyo hata tukihoji kwamba sababu zilizofanya 2015 wagomee zimetatuliwa ndipo wameingia tena au laaa? Wao wanatuziba kwa kujificha kwenye kichaka kinachoitwa historia ya siasa za Zanzibar.
Tumehoji hapa kwamba ni makubaliano gani ambayo ACT na CCM wameyaweka mezani hadi kufikiwa maridhiano ya leo ili kesho yasijirudie haya? Bado hatujibiwi tunarudishwa kwenye kichaka kanakwamba sisi hatujui historia ya Zanzibar.
Mfano Chadema imeweka mezani msingi wa maridhiano ya kitaifa kati yake na CCM ambayo ni 1. Kutambua kuwa uchaguzi ulikuwa batili, 2. Kuundwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi, 3. Mchakato wa Katiba Mpya ya Warioba kuendelea
Pengine kuna wanachoshindwa kusema wazi kuwa maslahi ya Maalim na Wenzake yamezingatiwa kuliko malengo ya Wazanzibar ya kupata nchi yao ambao ndio msingi ulioasisiwa na CUF ya Maalim. Nani leo mtetezi wa Wazanzibar??
Jibu liko Pemba na Unguja!
_______________
Nakukumbusha, ni mwezi wa Sikukuu, Watu watano watapata ZAWADI ya kitabu cha Ujasusi kwa 20,000 tu popote ulipo badala ya 80,000.
Lipia 20,000/= kwa
TigoPesa 0715865544
M-Pesa 0755865544
Airtel Money 0788887887
HaloPesa 0624452045
(Yericko Nyerere)
Tuma majina yako na ulipo
(Dar ni free delivery)
Nje ya Dar nauli 8,000/=
Instagram Follow @yerickonyerere
View attachment 1644809
Hakuna mtu anakulazimisha ww endelea kubakia kwenye kususa fcMimi siungi mkono maridhiano hayo na wala sitayaunga mkono hata nikiwekewa bunduki kichwani .
Liwalo na liwe
Ruzuku tayari wameshapokeaMsingi wa uanzishwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa ilikuwa ni nini?
CCM na ACT-Wazalendo walichofanya ni kutimiza takwa la Katiba ya Zanzibar 1984.
Kama ndani ya katiba kuna maridhiano basi walichofanya ni kutekeleza kilichoko ndani ya katiba.
Inanishangaza ulipoandika ''Mfano Chadema imeweka mezani msingi wa maridhiano ya kitaifa kati yake na CCM ambayo ni 1. Kutambua kuwa uchaguzi ulikuwa batili, 2. Kuundwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi, 3. Mchakato wa Katiba Mpya ya Warioba kuendelea''
CHADEMA mnataka maridhiano na nani? Kwa lipi? Kwa msingi wa katiba ipi?
Katiba ya Tanzania inasema, the winner takes all. Kwa Tanzania bara uchaguzi umeisha!
Ninajua baada ya muda CHADEMA wataanza kupokea ruzuku za serikali lakini pia watapeleka wabunge wa viti maalum bungeni hata kama sio kina Mdee na kundi lake!