Tunamkumbuka Edward Sokoine - Mtu wa Watu

Mwanakijiji na wengine,

Mnaonaje tukimuenzi Marehemu Sokoine mwaka huu kwa vitendo kama JF?
 


........Mkuu Kyoma uko wapi ndugu?....heri ya mwaka Mpya.....

Salute
 
Mwanakijiji na wengine,

Mnaonaje tukimuenzi Marehemu Sokoine mwaka huu kwa vitendo kama JF?
Yeah, hata sisi tulio machimboni tutarudi mjini. Huyu bwana ingawa nilikuwa kijana mdogo sana wakati akifariki, namkumbuka kama shujaa wa kweli na mtu aliyekuwa anaijua dawa ya matatizo ya uongozi Tanzania.

Kama tungeliendelea kupambana na shida zile, tungezalisha wafanyakazi makini na wagunduzi wa kweli kwa maelfu. Alipokufa waliomfuatia ndo hao ruksa mpaka na ufisadi hadi ukatinga Ikulu.
 
Kwa kumkosa huyu mpambanaji wa rushwa , magendo na wizi wa fedha za uma tumeona mengi. Machache tuliyoshuhudia ni epa, kagoda, tics, kiwira na buzwagi. Shujaa huyu asingekubali ushenzi huu.

Amekosekana aliye vaaa viatu vyake. Hongezeni mapungufu mengine.mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi.
 
Huyu mzee alijkitahidi kweli but mdogo wake dah. Namaanisha yule morani mwingine!
 
Lakini morani mwingine pamoja na mapungufu yake alikua mchapa kazi, alitolewa kafara on behalf of vigogoz, cause kama kwey tuhuma za ufisadi zingekua kwa kiwango hicho wakisemacho why hajafikishwa kisutu au wanaogopa maumbuo maana Deep Green, Kagoda na Maremeta sio morani wahusika tunawajua lkn mhhh walijisemea ndugu zangu kina Soda Nitakutapika " Kumkoma nyani Giladi" tumebaki kumuhukumu morani na Richmond.

Mhhh I think its diversion of attention tu tusahau Kagoda, Deep Green, Maremete, Kiwanda cha Kusafisha Dhahabu Vingunguti aka Mwananchi Gold Ref...... na mengi tu ya mashenzini. anyways ...............
 
Tunamuenzi vipi marehemu Edward Sokoine?

ANAYESTAHILI pongezi hana budi kupongezwa. Wengi wetu tunapenda sana kufanya kumbukumbu ya mambo yanayofurahisha, lakini mambo ambayo yanasuta dhamiri zetu huwa si ya kukumbukwa sana, maana mambo hayo hutukosesha raha.

Mojawapo ya mambo ambayo yanakosesha raha, viongozi wa Tanzania wa leo kuyakumbuka, ni kuhusu kifo cha aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania wakati wa utawala wa awamu ya kwanza, Edward Moringe Sokoine, na ndio maana hata kumbukumbu yake haipewi mkazo na viongozi wa chama tawala na serikali yetu.

Je ni kweli kwamba Edward Moringe Sokoine si wa thamani sana kiasi cha kubezwa kukumbukwa kwa heshima na chama au na serikali ya chama chake enzi za uhai wake?

Edward Moringe Sokoine alizaliwa mwaka 1938 na kuaga dunia Aprili 12, 1984. Alikuwa Waziri Mkuu mara mbili, Februari 13, 1977 hadi Novemba 7, 1980, na tena Februari 24, 1983 hadi kifo chake kilichosababishwa na ajali ya gari eneo la Dakawa mkoani Morogoro akitokea bungeni Dodoma. [/SIZE]
Uongozi wa Sokoine ulionekana kuwa wa mfano kwa uadilifu na kufuatilia utendaji kazi huku akikemea ulaji rushwa na ubadhirifu wa mali za umma. Huenda hii ikawa ni mojawapo ya sababu kubwa ya uongozi wa nchi yetu kususia kumfanyia kumbukumbu ya heshima, kwani uadilifu aliokuwa nao Sokoine haupo hata chembe katika CCM na serikali yetu ya sasa.

Sokoine alikuwa ni mpenzi wa wananchi wote; alikuwa mzalendo mwaminifu, mwenye vitendo vingi, lakini pia maneno machache.

Je, hali halisi katika uongozi wa serikali yetu ikoje? Maneno mengi, lakini vitendo kidogo au hakuna kabisa.

Watanzania wa sasa wamekuwa wakiahidiwa vitu vingi na serikali yao; vitu ambavyo haviwezekani hata kwa wenye imani ya kuhamisha milima, je, uadilifu uko wapi?

Sokoine aliendesha yeye mwenyewe Operesheni Wahujumu Uchumi, mafisadi walitupa barabarani pesa walizokuwa wamezikwapua kwa njia haramu ili kujisalimisha.

Vipi vigogo wetu wa sasa walivyo na uswahiba na wahujumu uchumi. Viongozi wetu wa sasa, akiwemo rais, mawaziri na makatibu wakuu na wakuu wa mikoa na wilaya; wanahusudu zaidi urafiki na wahujumu uchumi, wanaowahujumu Watanzania huku walalahoi wakiendelea kusota katika njaa na lindi la umaskini.

Unategemea wahusudu mafisadi hawa wanaweza kukumbuka kuandaa kwa heshima kumbukumbu ya mzalendo huyu ambaye matendo yake yanachefua hawa waliopo sasa?

Viongozi wetu wa sasa ndio marafiki wakubwa wa mafisadi, Sokoine alitafsiri kauli zake kwa vitendo na bila woga.

Enzi za Sokoine, kama kulikuwa na viongozi wala rushwa na mafisadi, basi Sokoine alikuwa chanzo cha hofu kubwa ya wala rushwa na mafisadi hao; alikuwa akifanya ziara za ghafla sehemu za kazi na kisha akapata maelezo na ushahidi wa ufisadi wa viongozi husika. Hicho ni sawa na kiyama.

Viongozi wetu wa sasa wanakaa na Mafisadi, wanakula nao, na kufanya mikutano pamoja kupanga namna ya kuwahujumu Watanzania, hata wale wanaotuhumiwa waziwazi, wanateteana. Turejee kauli ya Waziri Mkuu wa sasa Mizengo Pinda, aliposema mmoja wa watuhumiwa wa ufisadi ahukumiwe kwa kazi alizofanya na si majungu ya bungeni.

Enzi za Sokoine yeye mwenyewe alisimama kidete kupambana na wahujumu uchumi ambao baadhi walilazimika kukimbia nchi na wengine kutelekeza biashara zao.

Je, viongozi mafisadi waliopo sasa wanaweza kweli kumkumbuka mtu ambaye alikuwa tishio kwa maisha yao?

Sokoine alionekana kama tishio la majambazi, lakini wakati huu wa utawala hasa wa awamu ya nne, majambazi na vibaka wanapapasa hadi Ikulu. Kibaka aliingia Ikulu akaiba maua, majambazi yakavunja hata ofisi ya Rais mstaafu Benjamini William Mkapa wakaiba kompyuta; kama majambazi yanapapasa hadi sehemu nyeti kama hizo, sijui huku mitaani walalahoi tunalindwa na nani? Huenda ndio maana wananchi wanazidi kujichukulia sheria mikononi.

Sokoine alikuwa mfano wa kuigwa. Alishi kama alivyohubiri. Siyo tu hakujilimbikizia mali, bali alipunguza hata mali zake ili apate nafasi zaidi ya kututumikia Watanzania.

Jamii ya viongozi tulionao sasa, ambao hata kutaja mali zao wanaogopa, watu wasiotumia muda mwingi kukaa ofisini, watu wanaotumia muda mwingi kukaa katika biashara na starehe zao, wanaweza kuwa na lipi la kuigwa?

Wanaweza kukumbuka kweli kumuiga Sokoine? Na watamuiga kwa lipi? Watafanya hivyo hadharani au sirini ili wasisutwe na Watanzania maskini ambao hawategemei hata chembe ya huruma kutoka viongozi hao?

Pamoja na kiwango cha maendeleo kilichokuwepo wakati huo, Sokoine na Nyerere hawakuwachangisha Watanzania katika suala la elimu; madawati yalitosha na waalimu walienda shuleni kufundisha. Kwa sasa ni tofauti, madawati hayatoshi, madarasa hayatoshi, na walimu wanatangaza waziwazi kuwa wamechoshwa na ufisadi wa serikali isiyowajali, hivyo wataendelea kufundisha wanavyojisikia.

Bahati mbaya walimu wamezira kuwafundisha watoto wa maskini, na watoto wa vigogo hawapo nchini katika shule za kata, ndio maana hata tishio la walimu haliwagusi vigogo.

Sokoine aliutambua ukweli, kuwa katika nchi yetu, mahitaji ya wachache wenye nacho ni makubwa mno na kamwe hawaridhiki na walichonacho na wapatacho, lakini la msingi wanalohitaji wanyonge wa nchi hii ni moja tu: kutokandamizwa.

Lakini ukandamizaji uliopo katika nchi yetu kwa sasa ni mkubwa, watu wamefukuzwa katika nyumba zao kwa sababu ya kulazimishwa kuchangia michango ya sekondari hata kama hawana, kina mama wamejifungulia katika ofisi za watendaji kwa kukosa michango, wanaotaka kuandamana wanatishwa na wasipotishika huambulia kipigo, je ndani ya jamii hii iliyochafuka vile tungeweza kumkumbuka mtu msafi?

Enzi za Sokoine, wananchi waliwapenda viongozi wao, walijipanga barabarani kuwaimbia viongozi wao, kwa kuwasifu walipowafukuza wahujumu uchumi, walivyokosa uswahiba na wafanyabiashara, tofauti na sasa, hata msafara wa rais unapigwa mawe, mabango kibao kila anapokuwa na ziara katika nchi!

Wananchi wanalalamika kila siku, ufisadi, ujambazi, wizi, maadili ya kazi hakuna, lakini rais aliyepo na chama chake wameendelea kuwaingiza wananchi mjini, kwa kuwaahidia maisha bora kwa kila Mtanzania, ambayo labda yanapatikana katika Tanzania ambayo sio hii tunayoiona.

Je, tunamuenzi Sokoine, au tuache kabisa kuliko kuchafua jina safi kwa sifa za kijinga!? Tutafakari. [Kifo cha Waziri Mkuu Edward Moringe Sokoine kilileta majonzi makubwa kwa Watanzania wa kawaida ambao walikuwa wanamtegemea Sokoine kuwatetea wanyonge na kuinua kiwango chao cha maisha.

Mwili wa Edward Moringe Sokoine ulizikwa nyumbani kwao Monduli, mkoani Arusha. Pamoja na maadili mazuri aliyoonyesha, viongozi waliomfuata katika uongozi hata jimbo alilotoka wamekuwa wakituhumiwa sana kwa Ufisadi.

Kuna kila sababu ya Watanzania kutofanyiwa kumbukumbu ya heshima ya aliyekuwa waziri wao mkuu, waziri msafi, aliyechukia ufisadi, kuliko kufanyiwa kumbukumbu ya mtu msafi na mafisadi.
 
presdaa anataka kujifanya baba wa taifa kila anaetofautiana nae anajidai kumfungia mwaka huu inakula kwake ngoja uchaguzi ufike utjua alikuwa kimya au alikuwa kazini, na babu seya lazima atoke korokoroni.
 
Duh! kwa hakika umenikumbusha hii figure, sijui iko wapi! Jamaa kaamua kuwa kimya kwelikweli!
 
ni moja ya wanaCCM wanaofahamu vema siasa za nchi..ndio maana hawezi kuongea kwa sasa..
 
mwacheni, JK na Makamba wanajifanya majinias sana.
 
''mimi mangula,nipo lupembe hapa BARAZANI!nasimamia mashamba yangu ya chai...''
karibuni lupembe vijana
 
Mangula kashindwa siasa za fitna na rushwa za CCM kaamua kulima.

Kama kumbukumbu zangu ni nzuri Mangula aligombea uenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa akashindwa,bila shaka mtandao ulihakikisha hapenyi.

Lakini nakumbuka baada ya kushindwa alilalamika uchaguzi kugubikwa na rushwa kitu ambacho yeye alidai hawezi kukifanya. Alisema siku hizi wapiga kura hawataki vipeperushi, wanataka vipeperushwa.
 
Inasemekana Mangula katka uchaguzi wa 2005, alikuwa kambi ya Sumaye, hakuwa ana mfagilia Kikwete aingie madarakani. hivyo kikwete alivyo win akaamua kumpoteza kisiasa.
 
Nimejifunza mambo mengi juu mzee jumbe ningependa kujua tena kuhusu sokoine.mara uliuliwa lakin inasemekana ni mwanamapinduzi wa ukweli kwa nin aliuliwa? Alikuwa anapinga ufisadi wa enzi hizo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…