Mzee ES,
Kyoma,
Kwa maoni yangu Mwalimu alisuasua mno katika majadiliano yake na IMF na WB. Wakati akisuasua uchumi uliendelea kuharibika, na kufikia mahali nchi zote wafadhili zikatususa. Naamini tungekubali ushauri wa kurekebisha uchumi mapema yasingetufika haya yanayoendelea leo hii Tanzania.
Mzee JokaKuu, sijuhi hii ulonipiga ni chenga ya mwili, tobo, kanzu, au vyote kwa pamoja. Niko tayari kupata somo kutoka kwako Mzee, kuhusu hawa Majangiri wa IMF na WB. Yaani unasema Mwalimu angewasikiliza hawa Magaidi tusingekuwa hapa tulipo kiuchumi? Binafsi, nadhani tupo hapa tulipo kwasababu tulitelekeza sera za Mwalimu na Sokoine, alafu tukakumbatia za haya Majangiri , ndio maana tupo hapa tulipo. Kabla sijaenda mbali, mosi, binafsi, napendekeza haya mashirika mawili ya IMF na WB yasifanyiwe ukarabati kama wengine wanavyofikiri bali yavunjwe na kufutwa kabisa. Mbili, nadhani tulifanya makosa kama watanzania kutokufanya matembezi kama yale ya Azimio la Arusha, kuunga mkono juhudi za Nyerere na Sokoine za kupinga Masharti ya haya mashirika ya kijambazi duniani. Nitatoa mawzo yangu machache, yale ya ukeleketwa, nitayaweka kiporo, alafu naomba nikimaliza, na wewe utoe yako kuhusu hawa waheshimiwa ili niweze kupata mwanga wa kile nisichokiona.
Katika biashara ya mitaji, kama ilivyo ya mabenki yote, ukijumlisha na magaidi wa Benki ya dunia, utajiri wao mkubwa unatokana na fedha iliyo katika mzunguko, kwa maana ya kukopeshana. Tatizo sio letu, bali ni lao kwa sababu wanafedha kama mitaji. Hawawezi kutengeneza faida mpaka hizo fedha ziende kwenye mzunguko, yaani wawakopeshe watu ambao watalipa hizo fedha walizokopa, fees, na riba. Vilevile, lazima wahakikishe kuwa kuna watu wa kukopa hizo fedha kwa muda wote ili wanedelee kutengeneza faidaama sivyo biashara yao inadoda na kufa kifo cha kawaida. Ndio maana wanakuja na Cocaine, kwa maana ya masharti yatakayowadumaza na kuendelea kuwafanya mafukara wa mawazo, au tegemezi wa fedha, ili muendelee kukopa, na kuamini kuwa bila Ganja, yaani fedha za mikopo, hamuwezi kutatua matatizo mliokuwa nayo.
Ni Wizara chache ndani ya nchi zilizoendelea, amabazo zinaingiza fedha nyingi, tena kwa mkupuo, kama fedha ziingizwazo kutokana na vitengo au Wizara zianzoshughulikia masuala ya nchi zijulikanazo kama masikini duniani. Angalia idadi ya nchi zinazojiita masikini duniani, alafu jumlisha matirioni ya madola ambayo nchi hizo zinadaiwa, ongeza mlundikano wa fees na riba katika miongo kadhaa, alafu gawanya kwa idadi ya nchi tajiri. Ukifanya hesabu vizuri, utaona kwamba, kutokana na fees pamoja riba amabzo nchi zinazoitwa masikini zinalipa nchi tajiri, hawa jamaa, wamevihakikishia vitukuu vyao mlo wa neema usio na jasho kwa karne nyingi zijazo. Mitambo au Mirija inayofanikisha hili zoezi, ni mashirika ya IMF na WB. Eti sisi tunasema kuwa hawa jamaa wanatupenda sana mpaka wanatuwekea wizara au vitengo vinavyoshughulikia masuala ya Afrika. Asthakafululahkii! You are not even a Nigger!
Kabla siajenda mbali, labda tukumbushane chimbuko la hawa Majangiri. Tuwajue ni akina nani, wanatufanyia nini ambacho sisi wenyewe hatuwezi kufanya, alafu baada ya hapo tuone kama Mwalimu na Sokoine wangewasikiliza toka zamani, tungekuwa mbali. Si vibaya pia tukatafuta mifano, ambayo nadhani mzee JokaKuu utakuwanayo tele, ya nchi zilizowasikiliza hawa majangiri mapema kabla yetu, alafu zikafanikiwa, au ziko wapi sasa.
Benki ya Dunia WB na Shirika la Fedha Duniani (IMF), ambao viongozi wetu wa kisasa wanayataja haya mashirika kuwa ni miongoni mwa wahisani wetu, vilianzishwa mwaka 1944 mjini Bretton Woods, New Hampshire, wakati vita kuu ya pili ya dunia inakaribia kuisha. Mataifa wanzilishi, walihepuka mabolongo yaliyowapata baada ya vita kuu ya kwanza ya dunia. Hivyo, walitaka iwepo Benki ambayo wangeweza kupata mikopo ya muda mfupi ya kuwawezesha kuyajenga upya mataifa ya Ulaya baada ya kushinda vita. Kumbuka, wakati huo haikuwepo dunia ya tatu, bali zilikuwepo dola kubwa ambazo zilikuwa zinatawala maeneo makubwa duniani. Haya mashirika mawili hayakuundwa na jumuia ya Kimataifa, hivyo, yaliundwa kwa maslahi ya wale walioyaanzisha.
Mpaka sasa hivi, muundo wa Shirika la Fedha duniani (IMF), bado unayapa nguvu mataifa makubwa yenye nguvu za kiuchumi. Kura ya kila taifa inategemea na ukubwa wa uchumi wake. Marekani inaongoza kwa kuwa na zaidi ya asilimia 17 ya kura zote, ikifuatiwa na nchi kama Japan na Ujerumani. Kuathiri maamuzi ya IMF, unahitaji asilimia 80 ya kura zote. Hata hivyo, Marekani na nchi za Ulaya peke yake wana zaidi ya asilimia 80 ya kura zote. Kwa maana hiyo, mataifa mengine hayawezi kubadilisha kitu chochote mpaka wapate ruhusa yao.
Mikopo misaada inayotolewa na haya mashirika imekuwa na masharti magumu na yanayofanana kwa nchi zote duniani ambazo hazina nguvu za kiuchumi. Mifano ya mojawapo ya hayo masharti ni kuweka viwango vya ubadirishaji wa fedha za kigeni, matumizi katika bajeti ya nchi, Mzunguko wa fedha katika benki za ndani ya nchi, pamoja na ubinafsishaji wa mashirika ya Umma. Mathalani, tulipewa mkopo na Benki ya Dunia kwa masharti ya kubinafsisha sekta ya maji, na sisi tukajaribu kufanya hivyo, lakini tukapigwa kanyabwoya. Hata hivyo, zile fedha lazima tuzilipe na riba juu yake, hata kama hatukufanikiwa katika hilo. Kwa kifupi, IMF na WB, hawakulazimishi kupunguza mipango katika sekta, kwa mfano Afya na Elimu, bali wanakuwekea makadirio ya kiwango cha fedha unachoweza kutumia katika hizo sekta, hivyo, unaishia kupunguza baadhi ya mipango katika hizo sekta, kama tulivyofanywa katika michezo, masomo ya ufundi, n.k
Masharti mengine ni kwamba, nchi ikitaka kuongeza kiwango cha bidhaa zinazouzwa nje (export), na kupunguza kiwango cha bidhaa inazonunua kutoka nje (import), inabidi fedha ya nje iwe na thamani kuzidi ya ndani ya nchi husika ili kukatisha tamaa manunuzi ya bidhaa kutoka nje. Hivyo, unatakiwa kushusha thamani ya fedha ya nchi husika, mfano kama tulivyofanya kushusha shilingi ya Tanzania, na thamani ya dola inapanda. Hata hivyo, kwasababu tunakwenda kichwakichwa, hatukukumbuka kuwa viwango vya uzalishaji katika jamii zetu ni vya chini sana. Tunategemea malighafi kutoka nje ili tuweze kuzalisha. Mfano wa bidhaa za lazima zitokazo nje ni Mafuta, Vitabu, Madawa, na Mbolea. Bidhaa zote hizi zinanunuliwa kwa fedha za kigeni. Thamani ya fedha ya nchi inaposhuka na fedha za kigeni kupanda, gharama za uzalishaji zinakuwa juu na kusababisha mfumuko wa bei kwa bidhaa zinazozalishwa ndani ya nchi. (hupo hapo Mzee JokaKuu?). Hizi zi Sera, ni Masharti.
Benki ya dunia na Shirika la fedha duniani wakisha tukopesha fedha kwa makubaliano ya hayo masharti, na madhara yakishaanza kuinyemelea nchi husika, mataifa yenye nguvu za uchumi yanaanzia yalipoishia hayo mashirika. Wanaitaka nchi ifungue milango ya biashara bila masharti yoyote, ikiwa ni pamoja na kuondoa vizingiti kwa bidhaa kutoka kutoka nje za nchi. Kuvunja vunja mashirika yetu makubwa ili mashirika ya nje yaweze kushindana vizuri, kama tulivyofanya kwa benki yetu ya NBC.
(unakumbuka Mwalimu alivyolalamika pale Kilimanjaro Hotel 1995, kuwa hawa jamaa wanawaambia viongozi wetu kuwa eti NBC ni kubwa, hivyo ivunjwe katika vibaba ili benki zao ziweze kushindana. Mwalimu aliuliza, can NBC open branch in New York? Aliuliza kuwa NBC ni benki kubwa kuzidi benki gani?), Lakini viongozi wetu walitii amri. Wanasema ni soko huria, utandawazi, ujasirimali, na ujinga mwingine unaofanana na huo. Wanasema biashara inaendeshwa na nguvu ya soko, lakini wanatuwekea masharti kuwa lazima tuwawekee mazingira bora wawekezaji kwa kutokuwatoza kodi kwa muda kadhaa. Tufungue ardhi yetu bila masharti kuruhusu makampuni makubwa kuchimba madini bila masharti.
Masharti mengine ni kwamba, fedha wanazotukopesha, kamwe, haziwezi kutumika kutumika kuwasaidia wakulima au wafugaji wetu ili kupunguza makali ya uzalishaji (subsidize). Hata hivyo, serikali zao, zinawasaidia wakulima wao ili kupunguza makali ya uzalishaji. Wanataka tufungue milango kwa maana kuwa bidhaa za wakulima wao ambazo ziko subsidized, zishindane na bidhaa za wakulima wetu ambazo haziko subsidized katika mfumo wa kitu kinachoitwa soko huria. (Ndio maana Mwalimu aliuliza palepale Kirimanjaro 1995, kuwa bingwa wa ngumi wa uzito wa juu hawezi kuingizwa ulingo mmoja na yule wa uzito wa kati. Alisema Bukina Faso and German haziwezi kuwekwa kwenye ulingo mmoja). Viongozi wetu walisalimu amri katika hayo masharti.
Matokeo ya hizi ghiliba za IMF na WB, bidhaa zinazoingia nchini kwetu kutoka nje zinauzwa kwa bei ndogo kwa sababu mbili, mosi, njia za uzalishaji katika nchi zenye nguvu za kiuchumi ni za kisasa, kwa maana ya kutumia mashine, wakati sisi tunatumia majembe ya mpini. Pili, Uzalishaji wa bidhaa zao unapatamsaada wa fedha kutoka katika serikali zao kwa lengo la kupunguza makali ya uzalishaji, kitu wanachotukataza sisi tusifanye kwa wakulima na wazalishaji wetu.
Mfano halisi katika nchi yetu, tuna idadi ya kutosha ya wananchi wetu ambao ni wafugaji. Hata hivyo, ilitupate mkopo kutoka Benki ya dunia, hata kama ni wa kununua Ndege ya Raisi, na hauna mahusiano yoyote na wafugaji, basi, WB itakwambia kuwa umekuja kwetu kukopa fedha kwasababu huna mipango mizuri ya kuingiza fedha. Hatuingilii Uhuru wako, lakini fedha zetu zina masharti yatakayo kusaidia kurekebisha matumizi yako ya fedha ili uwe na fedha na usije kukopa tena. Masharti yenyewe ni kuwa uondoe vikwazo ili makampuni ya nje yaingize nchini kwako maziwa ya Unga. Of course, maziwa ya Unga yanauzwa kwa bei rahisi ukilinganisha na maziwa ya Ngombe. Hii ina maana, wafugaji wetu wanapigwa kaputi kwa sababu maziwa yao yanashindana soko ma maziwa ya Unga. Pia, watu wetu hawapati lishe bora kwasababu maziwa ya Ng'ombe ni bora kuliko ya Unga.
Mfano mwingine ni ule wa Serikali yetu kuwekewa masharti isiwape fedha (subsidize) wakulima wa Pamba, lakini nchi ya Marekani inawasaidia fedha (subsidize) kwa kiasi kikubwa wakulima wake wa Pamba. Wakulima wetu wanatumia majembe ya mkono na wale wa Kimarekani wanatumia Mashine za kisasa. Hata hivyo, Pamba inayotoka Marekani na ile ya Tanzania inauzwa kwa mashindano katika soko la pamoja bila kuangalia upendeleo katika njia za uzalishaji. Haya ndio masharti ya IMF na WB, yaliyojumlishwa katika mfumo wa uchumi wa Soko huria au utandawazi, ambapo njia zote zinazoweza kuinua viwango vya maisha ya wakulima na wazalishaji wa watu wa nchi yetu zinapigwa mweleka na haya majinamizi.
Ndio maana baada ya kifo cha Sokoine na Nyerere, uchumi wa nchi yetu unaendeshwa na mataifa ya nje kwa kutumia mitambo ya ukopeshaji inayoendeshwa na mashirika ya fedha ya kimataifa IMF na WB, hivyo kuondoa dhana nzima ya matumaini na ndoto za kujitegemea. Viongozi wetu wanasema huu ndio uhisani. Binafsi, naamini kuwa Mhisani anapashwa kuwa mtu wema, anayependa kuwasaidia wenzake bila hila, ulaghai, au utapeli (kamusi ya kiswahili sanifu 1981). IMF na WB sio wahisani bali ni Majangiri. Nyerere na Sokoine walikuwa na haki ya kukataa masharti yao.
Azimio Rome Februari 2003, na lile la Paris Machi 2005, yaliyohudhuliwa na wabia pamoja na mataifa yanayojiita masikini duniani, ambapo Tanzania ilitia saihi maazimio yote mawili, yalikuwa na lengo la kupunguza ukali wa masharti ya mikopo na kuziachia nchi masikini uwanja wa kufurukuta na kupanga mipango ya maendeleo. Hata hivyo, waliweka vipengele katika hayo makubaliano kuwa lazima kuwepo na uangalizi wa wabia katika baadhi ya nyanja. Mathalani, Mgogoro uliojitokeza kati ya Denmark na Serikali ya Tanzania, ni matokeo ya mwendelezo wa maazimio ya Paris na Rome. Mswada wa marekebisho ya sheria ya rushwa unaojadiliwa na Jambo Forums sasa hivi, umetokana na msukumo kutoka nje ya nchi na si msukumo wa wananchi wa Tanzania. Tumefikia mahala mabapo sheria za kuendesha nchi yetu, zinatungiwa Paris na Rome, wala sio Kiwaga, Arusha, iringa, au Musoma kama tulivyokuwa tumezoea enzi za Sokoine na Nyerere. Of course, wabunge muda wote wamekuwa ni vikaragosi wa Serikali.
Mkutano wa mataifa yaliyo na maendeleo ya viwanda duniani G8, uliofanyika mjini Gleneagles, Scotland Julai 2005, Ulifuta madeni ya nchi 19 zilizokuwa zimebeba msalaba mkubwa wa madeni ikiwemo Tanzania, kwa masharti kadhaa yaliyowekwa na hizo nchi. Kitu cha maana kilichoongelewa Gleneagles ambacho kinawanufaisha Wakulima na Wazalishaji wengine wa nchi masikini duniani kuliko mikopo na madeni yaliyoishia kwenye mikono ya wajanja wachache, ni mfumo wa biashara ya haki duniani. Kuweka mazingira na kuondoa masharti yanayowakwaza wakulima wa nchi masikini na yanawaneemesha wakulima wa nchi tajiri. Waliliweka hilo jukumu katika mkutano wa Mawaziri wa Jumuia ya Biashara Duniani (WTO) uliofanyika Hong Kong, China Disemba 2005. Hata hivyo, hakuna maamuzi yoyote yaliyofikiwa juu ya suala hilo katika huo mkutano. Hata mkutano wa G8 uliofuatia huko St. Petersburg, Russia, haukuwa na agenda ya kuleta mfumo wa biashara ulio na haki duniani.
Binafsi, sikubaliani na nia ya mataifa yenye nguvu za kiuchumi duniani, ingawa kwa nje wanaonekana kuazima sera za utu za kutufutia madeni. Haya mataifa hayawezi kumpinga shetani upande mmoja kwa kutufutia madeni, alafu wakahalalisha shetani upande wa mwingine kwa kukataa kuondoa mifumo ya uchumi duniani isiyo ya haki. Tumefutiwa madeni, lakini mifumo iliyo ndani na nje ya nchi yetu iliyotuingiza kwenye madeni, bado iko palepale. Tunachokifanya ni kuzunguka duara, na mwishowe tunarudi palepale.
Binafsi, sipingi nchi kukopa, ila napendela zaidi mifumo ya uchumi ambayo inatoa haki sawa kwa wote. Ikibidi kukopa, basi tuhakikishe tunahitaji (needs) hizo fedha, na sio tunazitaka (wants) fedha. Ili niweze kueleweka vizuri, nitatoa mifano ya baadhi ya fedha tulizokopa kutoka Benki ya Dunia na jinsi ambavyo tungehepuka hiyo mikopo. Benki ya dunia ni wasiri sana, hivyo, si rahisi kujua masharti yanayoambatanishwa na hii mikopo ninayoielezea chini. Lakini mikopo yote hii ina masharti magumu ya kutushikisha adabu. Leo nitaanza michache, na mingine naiweka kiporo.
Disemba 16, 2003, Serikali ya Tanzania ilipata mkopo wa dola za kimarekani milioni 40 kutoka katika Benki ya Dunia kwa ajili ya kuboresha Sekta ya Afya (Health Sector Development Project). Lakini kabla ya kukopa hizo fedha, kulikuwa na udhaifu katika Idara ya Afya ambao tungeuondoa kwanza ili fedha ziweze kuwafikia walengwa. Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha wa 2002/2003, Wizara ya Afya ilitumia shilingi 85, 300, 510 katika manunuzi hewa ya vifaa na madawa. Pia, Wizara hiyo, ilionyesha kuwa imeilipa Bohari Kuu ya Madawa kiasi cha shilingi 651, 235, 602 kwa ajili ya usambazaji wa madawa na vifaa mbalimbali, kumbe kiasi cha fedha kilichotumika kufanya kazi hiyo ni sh 44,625,191.
Mei 9, 2006 Washington , habari namba 2006/400/AFR, Serikali ya Tanzania ilipata mkopo wa dola za kimarekani milioni 40 kutoka katika Benki ya Dunia kwa ajili ya Uwajibikaji, Uwazi, na Uadilifu (Accountability, Transparency and integrity program). Lakini kabla Serikali haijakopa hizo fedha, Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha wa 2004/2005 inaonyesha kuwa Serikali ilipata hasara ya shilingi bilioni 140 kwa sababu ya kukosa nidhamu katika matumizi ya fedha. Yaani, tunakosa nidhamu ya matumizi ya fedha, hivyo, tunakwenda kukopa fedha ili tupate nidhamu ya matumizi.
Juni 15, 2006 Washington, habari namba 2006/472/AFR, Serikali ya Tanzania ilipata mkopo wa dola za kimarakani milioni 12 kwa ajili ya kufanya mfumo wa utozaji kodi uwe wa kisasa (Tax Modernization Project), kwa kuzifanya huduma ziwe bora kwa wateja, haki pamoja na uadilifu. Binafsi, nafikiri tungekuwa tunakusanya kodi kwa haki na uadilifu tusingehitaji kukopa hizi fedha. Februari 2006, Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mheshimiwa Lawrence Masha, aliliambia Bunge kwamba Serikali imekusanya jumla ya dola za kimarekani 54, 765, 462 kama (royalty) kutoka katika makampuni ya kuchimba madini yaliyopo nchini kwetu, toka mwaka 2000 mpaka 2004. Pia alilieleza hilo Bunge kuwa mwaka 2003 Serikali ya Tanzania ilitia saihi mkataba na kampuni ya Kimarekani Alex Stewart (Assayers), kuyafanyia uchunguzi makampuni ya madini yaliyoko nchini mwetu ili kujua ni kiasi gani wanapashwa kulipa kama (royalty fees). Mpaka Februari 2006, Serikali yetu ilikwisha ilipa Alex Stewart dola za kimarekani 30, 915, 642 na senti 80.
Kwa tafsiri yangu, katika kipengele cha (royalty) peke yake, wastani wa mapato ya Serikali kwa mwezi toka 200 mpaka 2004 na wastani wa mwezi wa gharama tunazoilipa Alext Stewart, Serikali inabakia na dola za kimarekani 282,180 na senti 27. Lakini Jarida linalotolewa na (Tanzania Chamber of Minerals and energy 2006), linasema kwamba madini yenye thamani ya dola za kimarekani milioni 693 yalisafirishwa nje ya nchi kwa mwaka mmoja peke yake wa 2004. Lakini toka mwaka 1997 mpaka 2005, Serikali ilikusanya mapato ya dola za kimarekani 255.5 kutokana na kodi za aina zote katika madini. IMF na WB ndio walituwekea masharti ya kusamehe kodi za makampuni yanayopora madini yetu. Wakati huohuo, wanatukopesha fedha ili tuwe na mifumo ya kisasa ya utozaji kodi. Sasa tukiwa na hiyo mifumo ya kisasa, tutamtoza nani hiyo kodi? Kinachotakiwa sio kwenda kukopa fedha ili kuleta haki na uadilifu katika mfumo wa utozaji kodi, bali ni kuipitia hii mikataba na kukusanya kodi.
June 8, 2004 Serikali ya Tanzania ilipata mkopo wa dola za kimarekani milioni 43.8 kutoka katika Benki ya Dunia kwa sababu ya mpango wa dharura wa kupunguza makali ya mgao wa umeme uliokuwa ukilikabili taifa letu. Hata hivyo, kadili ya Ripoti iliyotolewa na (Transparency International), Serikali ya awamu ya tatu iliridhia na kukubali Tanesco isaini mkataba wa kuilipa IPTL dola za kimarekani 2.5 kila mwezi kwa muda wa miaka 20, hata kama Tanesco hainunui umeme au inanunua. Kambarage na Sokoine si wanaruka kichura chura huko waliko. Mzee JokaKuu, Kambarage na Sokoine, hawakuwa na makosa ya kukataa masharti ya IMF na WB. Tumefika hapa tulipo sio kwa sababu ya matendo yao ya kukataa masharti, bali ni kwasababu ya umasikini wetu wa mawazo. Ebu fanya mahesabu hapo juu kati ya mkopo tunaowatwisha wananchi wetu, na fedha tunayowalipa IPTL kila mwezi.
Kila mkopo hapo juu unajitegemea. Kadiri ya Benki ya dunia, makubaliano ya kila mkopo niliyoiongelea hapo juu ni pamoja na ada ya uazimaji (commitment fee) asilimia 0.35, gharama ya kuhudumia mkopo (service charge) asilimia 0.75 kwa kipindi chote cha miaka 40 ya ukomavu (maturity) na kipindi cha madahiro (grace period) cha miaka 10. Hivi ni viwango vya Jumuia ya Maendeleo ya Kimataifa (IDA). Baada ya miaka 40, hakuna kiongozi yeyeto wa sasa atakayekuwa hai. Ndio maana wanafanya huu ushetani kwa kushirikiana na Majangiri wa IMF na WB.