Tunaoishi single (Ghetto Geez) Tukutane hapa

Tunaoishi single (Ghetto Geez) Tukutane hapa

Most of the time inadepend na maokoto ya siku iliyopita na iliyopo sisi wengine kipato chetu cha unga mwana leo unaweza kuotea laki afu ukakaa wiki nzima bila mchongo wowote.

Sasa hii ni budget wakati shimo limetema

Asubuhi
  • Supu na chapati mbili 3000
  • Sambusa na yai la kuchemsha 1000
  • Pepsi na Maji Lita moja 1300

Mchana
  • Zege na mishikaki miwili 4000
  • Maji Lita moja na nusu 700

Usiku
Hapa chief cooker nakuwa mwenyewe
- kinapitiwa kidali cha broiler chicken 4000 unga unakuwepo geto linatolewa dongo
-maji lita moja 500

Total 14000 Tz Shillings

Sasa kuna hii budget wakati harakati hazieleweki

Asubuhi inatoka kwenye ratiba nakuja kula mihogo miwili na soda 1100 majira ya saa sita nikitoka hapo natulia mpaka usiku napitia mayai mawili 600 na nyanya moja 200 litapikwa ugali mkubwa wakati wa kula ni kuhakikisha mayai na ugali vinaisha sambamba hapa maji ya kunywa ni ya bomba hichi ndio kipindi mikakati ya fedha kichwaani inakuwa mingi ila pesa ikipatikana nasahau shida zote

Total 1900 Tz Shillings
unaonekana jeuri sana ukiziotea 😁😁😁
 
mh! mkuu performance ya kitandani ipo vyema kweli au sio shida zako😁?
Naamini ipo mkuu japo Nina siku nyingi sana. 😂😂. Unakimbizana na maisha mjini hapa unarudi muda kama huu huyo Aisha utamuona saa ngapi? Kama imepungua basi itajirekebisha mbele ya safari huko hata sijali😂
 
Yaani kabisaa mwanaume unauwezo wa kupata ten kwa siku halafu unakaa pekee yako kama kaburini vijana wangu nyumba so kaburi tafuta mtu wa kuishi nae
😁😁😁😁... Nakuelewa mkuu ila kuishi na mtu ni zaidi ya kula, Kuna mambo mengi mtu unapoamua kuoa/kuolewa kwahiyo kwa sasa acha tuangapie gharama zetu sisi tulio single
 
Natumia wifi ya hoteli fulani hivi inapiga mtaa mzima.
Ngoja tubadirishe password mtakua mmekalia 🖕🏽🖕🏽🖕🏽 mtaa mzima na hamtaweza kuaccess mpaka u-scan QR Code tuone mnavyopigwa 🖕🏽🖕🏽🖕🏽 mtaa mzima
 
Ngoja tubadirishe password mtakua mmekalia 🖕🏽🖕🏽🖕🏽 mtaa mzima na hamtaweza kuaccess mpaka u-scan QR Code tuone mnavyopigwa 🖕🏽🖕🏽🖕🏽 mtaa mzima
Sa matusi ya nini
 
Back
Top Bottom