DOKEZO Tunaomba Serikali iingilie kati Hospitali ya Dar Group (T.O.H.S), Mmiliki hajulikani

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Watoto wamezaliwa Kwenye hii hospital hawa jamaa walikuwa vizuri Sana Kwenye huduma zao...
Serikali iingilie Kati haya malalamiko ya wafanyakazi
 
Mheshimiwa kwanza uwe na adabu unapotoa hoja zako, katika maelezo yangu sijasema kwamba STG ina matibabu yote ila ni mwongozo i.e summary inayomsaidia daktari ku assemble shule yake ya miaka mitano na mwaka mmoja wa utayari.

Kitu nilichoelezea ni mashinikizo ya kutubu nje ya muongozo na nje ya miiko ya kidaktari...kujaza vipimo vingi amabavyo haviko relevant na presenting condition ya mgonjwa au ku-exacerbate symptoms ili vipimo viandikwe vingi na dawa ziandikwe nyingi.

Kama ni daktari au mtaalamu wa afya utakuwa umenielewa.
 
Hii hospitali ina miaka zaidi ya 40 lakini inazidiwa na hospitali za juzi kama Rabininsia na bochi....!! Ni bora iwe chini ya uangalizi maalumu ili iendelezwe kuliko kuwa kisima cha wachache.

Shughuli za kitabibu hazisimamiwi kama unavyosimamia shamba lako au mtumishi wako wa ndani...kuna namna ya ku deal na haya mambo huku uki maintain privacy ya mteja. assume ww uko na daktari halafu mlango unafunguliwa ghafla na mtu aliyeshika nyundo mkononi.....huo ni ubakaji wa taalauma.
 
Broo kuna mdada ni mjamzito... mkataba wake nadhani umeisha na kanyimwa mkataba mpya japo ni mjamzito... mtu aliye nje hawezi jua kero zilizopo katika ile hospitali na hakuna mfanyakazi mwenye ujasiri wa kureport sehemu yoyote.
 
Kama kuna Hospitali ambayo Serikali ilitakiwa iimarishe zaidi ni hii, lakini nasitika imekuwa ni kama Mtoto Yatima huku pia ikidharaulika na Watu.
 
Hapa naona kama majungu kazini,Mimi na familia yangu ni Mdau mkubwa sana kwenye hiyo Hospital huduma zake ni nzuri sana na hospital inafanywa maboresho kuanzia majengo hadi huduma.
Unahudumiwa vizuri sababu madaktari na wahudumu wanajua nini wajibu wao... ila moyoni wana uchungu mwingi... usitete jambo usilolijua. Fanya uchunguzi, kwanini majungu yaanze leo yasianze zamani. Unajua kwamba hata benki ya CRDB ambayo ndio mishahara ya wafanyakazi wa pale inapitia hapo haiwakopeshi kwa sasa sababu ajira zao hazina uhakika. Ndugu usihukumu au kutoa hitimisho... usiwakaange wenzako sababu wewe upo kivulini.
 
Kama kuna Hospitali ambayo Serikali ilitakiwa iimarishe zaidi ni hii, lakini nasitika imekuwa ni kama Mtoto Yatima huku pia ikidharaulika na Watu.
hakika ndugu...hii hospitali ipo strategic area....highway inapita pale. iltakiwa iwe hospitali kubwa huenda kuliko hspital za rufaa na za kanda tunazozifahamu. wanachi wengi wanahangaika kwenda mbali lakini wangeweza pata huduma zote pale.
 
Watoto wamezaliwa Kwenye hii hospital hawa jamaa walikuwa vizuri Sana Kwenye huduma zao...
serikali iingilie Kati haya malalamiko ya wafanyakazi
Hospitali ya Dar group imejaaliwa wahudumu wa faya wenye weledi wa hali ya juu, wapo kwenye mazingira magumu lakini wanafanya kazi as if " ni salama na shwari" ila kwa sasa naona maji yanazidi unga... naona uvumilivu unawashinda. Ila ni the best doctors, ukiachana na wahudumu wa afya hata watumishi wa kada zingine wapo vizuri sana.
 
Hiyo kwenda tofauti na Mwongoz wa matibabu wa Serikali kwa ajili ya kujiongezea mapato ni uhujumu uchumi
Exactly...na hiyo ni dilema kubwa...kazi unaitaka na miiko ya kazi unataka kuifata. Nacho wapongeza madaktari ni kujitahidi kukaa kwenye miiko yao na kufanya walichofundishwa darasani japo mazingira si rafiki.
 
Kuna mambo huwa ni rahisi sana kuyatatua wala hayahitaji serikali, hapo ni kuhamasisha wananchi wasiende kupata huduma kwenye hiyo hospitali, baada ya hapo itakufa natural death, full stop.
 
Labda tabia zenu nyinyi madaktari wa hapo ndio imewafikisha hapo, yaani hamuaminiki. Mna side deals nyingi sana, yaani mwizi kapewa kazi ya kuchunga wezi wenzie
 
Labda tabia zenu nyinyi madaktari wa hapo ndio imewafikisha hapo ,yaani hamuaminiki .mna side deals nyingi sana.yaani muizi kapewa kazi ya kuchunga wezi wenzie
Sio lazima uchangie ndugu... hata kama umepewa maelekezo basi shirikisha na fahamu zako kidogo. Be humble sio kila kitu utakuwa na majibu yake... ukikaa kimya utakuwa mwenye hekima zaidi.
 
Ukiona mfanyakazi mswahili anasifia management ujue manager hasimamii vizuri...

Huu uzi unaashiria mkurugenzi hataki ujinga..
 
 
Ukiona mfanyakazi mswahili anasifia management ujue manager hasimamii vizuri...

Huu uzi unaashiria mkurugenzi hataki ujinga..
Kwahiyo kila mtawala anayelalamikiwa na walio chini yake ni sababu hapendi ujinga?? Kama watu wangekuwa wanapambanua mambo kwa staili hii basi kusingekuwa na vyombo vya kusikiliza watu au platform kama hizi..!! Kama jambo hulijui pata muda ulifatilie kwa kina. halafu punguza fikra za kigeni..." kuwa mswahili " sio fedheha....jivunie vya kwako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…