Tunaomiliki salon za kiume Tukutane hapa tuambizane namna ya kuziinua zaidi

Kwa upande wangu nina miezi tisa saiz....wakati nafanya kazi mkoa fulani hivi nilikua na urafiki na jamaa mmoja na muda mwingi alikua yupo tu....

Then akaja kunieleza kua yeye masuala ya kunyoa na music anayaweza...

Then nikanunua vifaa vyote vya saluni, tukatafuta fremu na kazi ikaanza chapu...

Mi zangu ni kumwambia na wewe unatakiwa ufungue ofisi kutokana na ofisi hii hii na uwasaidie wazazi wako....mi muda wa kukufatilia sina ila kama unaipenda uliyonayo sawa....mi sina cha kupoteza....pambana kijana....mi rafiki yangu ni yule anayepambana....uamuzi ni wako kijana....umri bado mdogo na unanafasi kubwa sana ya kufanikiwa....ukifanya kwa uaminifu cha mwezako na chako utakifanya kwa uaminifu

Mpaka leo sinashida nae na akikwama sana kwenye kwa mwezi ni mshahara wa mwalimu wa shule ya msingi anatuma....tupo mikoa tofauti but he is still keeping the trust na yupo na hali

Ninachojaribu kusema ni kwamba umpate mtu mshawishi tu biashara yeyote inakuaga poa
 
Aisee,, hongera sana mkuu kwa kumpata kijana mwenye uaminifu na nidhamu ya kazi. Hakika vijana hao wapo wachache sana siku hizi.
 
Hiyo inaitwa shukrani ya punda[emoji23][emoji23]

Ulifanya biashara kwa muda gani mkuu!!
 
Ndo akili zao hao, halafu kila siku wanalalmika kazi hakuna!
 
Wadau tujuzane vitu vya muhimu katika salon ya kiume na gharama zake
 
Wadau tujuzane vifaa vya muhimu vya saloon ya kiume na bei zake,ahsante.
 

Wewe ndio umeongeaa ukweli.
Maneno yanaathari kubwa kwa mwajiriwa wako.

Matatizo baadhi ni kwa mabosi
 
Kikubwa ni kufunga CCTV camera pale ili kila kichwa kinarekodiwa na mapato mnagawana kwa asilimia kama kunyoa ni buku jero yake jero ya ofisi ni buku hapo lazima kazi ifanyike
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…