Hoja yako umeielezea upande mmoja tu wa Chama.
Chama kila kipindi cha usajili huwa anakuja na drama zake.
Nitajie mwaka gani ambao msimu wa usajili umefika hujasikia longolongo za Chama
Akifakisha achukuliwe hatua na hiyo ndio inapaswa kuwa nidhamu endelevu, wachezaji wajue kuheshimu mamlaka.
Sisi mashabiki na sisi tutambue kuwa wachezaji wetu tunaowapenda tuna fursa ya muda mdogo sana ya kumuona mchezaji.
Katika huo muda ni awapo kiwanjani tu, na akiwa hapo hutamuona akiongea.
Maana yake kuna mengi yanayofanyika akiwa eneo ambalo sisi mashabiki hatupo.
Eneo hilo ndio sehemu anayopata fursa ya kuongea na kufanya mambo mengi ambayo mengine pengine hata sisi mashabiki tungepata fursa ya kuyaona kama si kupunguza mahaba yetu basi tungeweza kumchukia mazima.
Sasa kama huko ndio anafanya mambo yanayokiuka sheria, sisi mashabiki hatuwezi kuwa na guts za kuwalaumu viongozi kwa adhabu watayotoa kisa tu ni mchezaji kipenzi.