Tunaosubiri namba E tukutane hapa

Kuna namba D ukiiangalia mara 1 tu hutamani hata kuiangalia tena.

Na kuna namba B au C ukiiona utageuza shingo.
 
Kuangalia usajili wa plate namba za gari kisha kukadiria bei(thamani) ya gari sio sahihi na nikukosa uweledi wa kujua thamani halisi ya chombo. Sababu kuna watu wana gari zilizosajiliwa kwa B... zpo vizuri zaidi kuliko DVW.

Kipimo sahihi kujua thamani ya gari husika kwa ajili ya resale. Inatakiwa iwe;

1. Uchakavu wa gari husika (body, engine na interior)

2. Mwaka wa uzalishaji gari

3. Kama imeshawahi pata ajali (kama imepata ajili bei lazima iwe chini)

4. Umbali uliotembea (hapa unakuta crown imetembea 150,000KM na bado watu wanauziwa kwa bei sawa na iliyotembe umbali wa 50,000KM)[emoji31]

5. Record za service

UKIJUA THAMANI YA HELA YAKO HUTAKUBALI KUUZIWA GARI JUST BASED ON REGISTRATION PLATES.
 
Hio ni kweli. Ila nikisema nikuuzie gari namba C iliokaza against number D ya gari hio hio hata kama sio nzuri utanunua ya C kweli?
 
Mnaosubiri namba E ina maana hamna uhakika wa kununua gari ingine baadae?!! E ipo miaka mingine 5-8 sasa kimuhemuhe cha nini? Nimetulia zangu na D mbili na C moja wala sina pressure. Katika series hizi mpya ni B tu ilinipita bila kununua gari nilikomaa na A mpaka C katikati.
 
Kuna hamaa yangu gari ipo bond toka mwezi wa tano anasubiri E
 
Siyo tu kuwastukia , inaeza leta kizaa zaa pia ,
Sidhani kama kuna control nzuri ya hizi random plate numbers , wahalifu wanaweza kuchora namba zao na kufanya tukio huku raia tukidhani kuwa ni usalama .
Sasa hivi watu wanajiwekea namba tu hovyo hovyo hamna control yoyote. Mtu anaweka herufi mbili za chassis number na vinamba vitatu tayari anapuyanga nalo mtaani! Hakuna control kabisa. Kama msimamia sheria anavuruga utaratibu unafikri watu wengine mtaani watafanyaje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…