Detective J
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 24,058
- 41,518
Hawataki kusema ebola wanataka kusema Marburg Ili atakaye hoji waseme google. Eti kwamba hilo ni jina jingine wakiita "kisawe."
Cc: Ruble
Nimechelewa kuuona huu uzi.
Ila nilipofungua kabla sijasoma nikakuta mwandishi Ni brazaj nikatabasamu Kisha nikaanza kusoma na kupitia maoni ya watu.
Mkuu,
Hawa ndiyo watu wanaokimbilia ajali na kuwahi kureport kwenye social media "watu 20 wamekufa papo hapo kwenye ajali ya basi"
Siku serikali ikitangaza kwenye ile ajali walikufa watu 7 na majeruhi 25 utamsikia Tena anakuja na nyuzi kila platform na vichwa vya habari "serikali inapata faida gani kuficha vifo vya waliokufa kwenye ajali ya basi?" .Unaishia kumsamehe mtu Kama huyu kwani tatizo lake Ni moja tu; amekosa exposure ya mambo ya afya. Hakujua kuwa Kuna ambao walizimia wakazinduka baadae na Kuna ambao walifanyiwa cardio pulmonary resuscitation (CPR) na huduma zingine za 1st aid na kimatibabu kisha wakaamka nankuendela na maisha.Ila Hawa watu wakiona damu na mtu yupo kimya anahesabiwa Kama amekufa na kufunikwa khanga hadi kichwani.
Kwa matukio Kama haya Unaishia kujiuliza Sasa serikali inapata faida gani ikificha vifo vya ajali?
Serikali inapata faida gani ikificha ugonjwa eti wananchi wasijue huu ugonjwa ni Ebola?
Je, Serikali ikisema ukweli kuwa huu ugonjwa ni Ebola si ndiyo wananchi watachukua taadhari kwa umakini zaidi?
Mara ya mwisho nakumbuka ilikuwa mwezi February nilipoona video kwenye hospital ya serikali inayosisitiza tahadhari na njia za kujikinga dhidi ya Ebola na Nini Cha kufanya endapo utahisi kuna mgonjwa wa Ebola kwenye familia yako. Hii ilikuwa ni tangu ulipoibuka huu ugonjwa wa ebola kule Congo. Sasa kwa nini leo ionekane serikali inaficha wananchi wasijue ni Ebola. Kwa taaruki ipi? Kwa kuogopa nini?
Nimeshawahi kuingia kwenye majibizano na mleta mada juu ya mambo ya afya hasa suala la Corona na chanjo na Hakuna hoja ya maana aliyoongea zaidi ya siasa. brazaj ,mimi nadhani endelea kujikita na maswala ya siasa,huku kwenye afya upo shallow,achana na contents na links za kuokoteza Kisha unashusha threads. Yes utapa likes na replies nyingi za kukusuport lakini wewe ni mweupe hujui chochote kuhusu afya. Huku omba msada na siyo vinginevyo.
Kaka una uhakika ni ebola? i mean ww ni mtaalam wa afya ambae uko eneo husika na una uzoefu wa magonjwa ya mlipuko?
Nitapingana na ww, dunia imebadilika sana na info za magonjwa mengi ziko online.
accessible na watu wote duniani. Difference is experience ya ku deal na jambo lenyewe
Kwaio mungu ndio kisababishi ? Kwaio kwa uwezo wa binadamu haiwezekani sio ?Kwa uwezo wa Mungu siyo?
Ni changamoto kidogo kujadiliana naye,maana anakuja na wazo lake ambalo si sahihi,afu analazimisha wote mkubaliane naye,akikosolewa na kujiona amekosea anapindisha hoja ionekane kwamba yeye yupo sahihi hata kwa kukataa hoja zake mwenyewe alizoandika awali.Ni mbishi kwa lengo la kushinda sio kueleweshana.
Hivi nchi iitangaze Marburg kuificha Ebola kwa faida gani, si yote ni magonjwa mabaya yanayoambukizwa kwa namna sawa na hayana dawa? Unakuwa unaepusha nini ukiyataja maambukizi ya Ebola kama Marburg? Huoni umekuwa mjuaji katika hili? Na after all ukisha declare uwepo wa magonjwa ya namna hii si issue inakuwa handled kwa kushirikiana na WHO! Kwahiyo kwa mawazo yako WHO nao hawajagundua kwamba kilochopo Bukoba ni Ebola sio Marburg?Unayasomaga wapi hayo ndugu? Mbona wengine hatuyaonagi?
Ama kweli JF raha sana 🤣🤣
Mkuu umetoa taadhari nzuri... Ila jaribu kujielimisha zaidi juu ya magonjwa mbali mbali, watu waliosomea afya wanakushangaa, unapotaka kuaminisha Ebola ni Marburg... kisa msamiati Marburg kwenye kiswahili haupo,.... Sasa Kama ugonjwa wenyewe haujawahi tokea kabla uswahilini watu wangejuaje huo msamiati....... Kiufupi Mimi Neno Marburg nimekutana nalo 2007 wakati nasomea afya, magonjwa mengine yanayofanana na Marburg ni Ebola, chikungunya na dengue yote haya yaitwa hemorrhagic disease , hivyo neno Marburg sio jipya ....
Hii comment inatosha kuonyesha ni mtu wa aina gani tunajadiriana naye hapa.Wapi nimesema ni ebola ndugu?
Watu wa siasa Hawa,wasikusumbue kichwa mkuu.
Hawa ndiyo wakishika madaraka wanawalazimisha wataalamu waseme wanavyofeel wao na siyo Hali halisi ilivyo. Na Mara nyingi hawapendi kushindwa au kuonekana hawaju
Hawa wakiwahi kwenye tukio la ajali ndiyo umfunika khanga Hadi kichwani kila mtu ambae amelala kimya na kuandika mtandaoni RIP. Serikali ikija kutangaza idadi ya vifo Ni watu watatu wanaibuka Tena kwa nguvu mishipa ya shingo umesimama " serikali iache kudanganya,nimeshuhudia kwa macho yangu wamekufa watu 13 tena Mimi nilikuwa nimeshiriki kuwasitiri" Kumbe Kuna mambo ya kitaalamu yalifanyika Kama CPR na Kuna ambao walizimia tu wakaamka baadae.
Hawa watu hawapendi kuwasikiliza wataalamu wanasema nini. Wao wanashikilia misimamo isiyo na mantiki na kucreate attention mitandaoni.
"serikali ijitokeze kusemaa ukweli kwamba huu ugonjwa ni Ebola na si kufichaficha,mbona nchi fulani jirani wamenyooka na kutoa tahadhari kwa raia wao"
"serikali iache kulishughulikia hili Jambo Kama enzi ya Corona. Jiwe hayupo,Sasa kwa Nini inaendesha mambo ya hovyo Kama enzi zile za Corona?"
Hii comment inatosha kuonyesha ni mtu wa aina gani tunajadiriana naye hapa.
Rejea title ya maada yako... Na comments zako za mwanzo mwanzo wa thread..Ukiulizwa wapi, ustaarabu ni kuonyesha "pale" kwa kuleta kuleta ushahidi.
Rejea title ya maada yako... Na comments zako za mwanzo mwanzo wa thread..
Mwenyewe unajiona umeandiiika hadi bhaas. Yaani Serikali ifiche ugonjwa kwa maslahi ya nani!? Hivi Ebola unaijua unaisikia, tema mate chini usiombe hilo gonjwa likaitokea katika jamii yetu.Tumekumbwa gonjwa hatari lenye kuuwa hadi 90% ya wahanga.
Sisi kwa tunachoita kuondoa taharuki tumependelea kuliita Marburg badala ya jina lake linalofahamika uswahilini, yaani Ebola.
View attachment 2562190
"Kwamba tumependa kutoliita koleo kwa jina lake."
Maajabu ya Mussa.
Tangu lini uswahilini neno Marburg likafahamika? Kwani gonjwa hili lilipokuwa Congo, Uganda, Guinea, Gabon, Sierra Leone au Liberia tuliwahi liita Marburg?
Katika kinachoitwa kuepuka taharuki gonjwa halipewi umuhimu wala coverage yoyote ya maana kwenye media zetu. Kwetu Simba au Yanga kwenda robo fainali ni habari kubwa, Lakini si gonjwa hili.
Maisha yanaendelea kama vile kila kitu ni sawa.
Ya nini kutoambiana ukweli wote tukajipanga kukabiliana nalo ana kwa ana kama nchi?
Kwenye tahadhali zilizotolewa na wizara katika namna za kujikinga, kutogusana nayo imo. Inawezekana namna gani kwenye maisha yetu ya kawaida watu kutokugusana masokoni, magulioni, mashuleni, makanisani, misikitini, kwenye mabasi au kwenye madala dala?
Ebola si ya maji tiririka, barakoa, michaichai, matango pori wala upigaji nyungu.
Walioyasikia ya kwetu wameshtuka kuliko sisi wakati sisi tukichukulia poa. Dhidi ya gonjwa hili dunia tayari inatunyanyapaa.
Angalia Rwanda, The New Times - Rwanda on Marburg alert after Tanzania outbreak
Angalia mabeberu, BBC News - Ebola-like Marburg virus kills five people in Tanzania
Coverage zao ni makini na kamilifu (extensive and focussed). Kwetu wenge la awamu ile na njama za mabeberu bado lingalipo.
Kwanini watu wasiambiwe ukweli wote kukiwa kungali mapema? Ya nini kujidanganya?
Magonjwa haya si vita (vya kiuchumi). Ebola si corona ambayo kuuwa kwake kulikuwa hadi 2%. Hiyo hata ikihusianisha uzee na uwepo wa magonjwa mengine pia.
Kwa hakika kwenye ugonjwa huu tusipoamka mapema, usanii wetu uliozoeleka utatuumbua.
Hata hao Plasmodium wako tofauti. Ukishikwa na malaria iliyyosababishwa na Plasmodium malariae, vivax au falsparium unakutana na mziki tofauti kabisa. Mziki wa Ebola ni moto wa kuotea mbali, hawa Maburgs wana tabia zinazofanana kwa mbali na ebola lakini hawatishi. Japo wakikupata bila usaidizi wa kitabibu wanakutoa roho ndani ya muda mfupi.Ebola na Marburg kisayansi (yaani in scientific details) ni magonjwa mawili tofauti. Malaria na Plasmodium kisayansi ni vitu viwili tofauti. Uswahilini plasmodium haina maana yoyote ila malaria.
"Marburg and Ebola viruses are filamentous filoviruses that are distinct from each other but that cause clinically similar diseases characterized by hemorrhagic fevers and capillary leakage. Ebola virus infection is slightly more virulent than Marburg virus infection."
Ninakazia uswahilini neno Marburg halina maana yoyote ila ebola linalofahamika kuhusiana na huu ugonjwa.
Ya nini kujikinga mvua chini ya mwembe wakati nyumba za bati zipo?
Zingatia ugonjwa huu umekuwapo katika mataifa kadhaa kabla. Ni kwa mara hii tu Tanzania imeuita Marburg kwa watanzania. Kulikoni?
Mwongozo wako tafadhali.
Tatizo lako ni kwamba unadandia taaluma za watu. Ungeijua epidemiolojia ya Maburg na Ebola wala usingeendeleza hii hoja. Jambo kama hulijui usilikomalie kwa hoja za hisia, ulizia kwa wanaofahamu wakupe ufafanuzi ndg.Ugonjwa huu si wa kwanza kwetu. Umekuwapo mataifa mengine. Ni mjinga kweli kweli anayeweza kuamini kuwa hadi sasa hakuna taarifa mpya eti kwamba ni wagonjwa wale 8 na vifo vile 5 vilivyotokea na tatizo liliishia hapo.
Yaani nimejilinda na UKIMWI nije kufa kwa marburg sio uungwana kwa kweli
Mwenyewe unajiona umeandiiika hadi bhaas. Yaani Serikali ifiche ugonjwa kwa maslahi ya nani!? Hivi Ebola unaijua unaisikia, tema mate chini usiombe hilo gonjwa likaitokea katika jamii yetu.
Ugonjwa ulioripotiwa Kagera ni wa Maburg na ni wa virusi wa jamii ile ile ya Ebola lakini wa ukoo tofauti. Huu hauna ukali ule wa Ebola, tahadhari zikichukuliwa vizuri waathirika wake huweza kupona hata kwa 100% na maambukizi yake yanawweza kudhibitiwa kwa muda mfupi tofauti na wa Ebola yenyewe.
Tuwe na utamaduni wa kuheshimu maelekezo ya Serikali hasa inapotokea suala la Magonjwa. Ugonjwa ukifichwa fichwa maana yake kutakuwa na athari kubwa sana na za kijamii na kiuchumi ambapo pamoja na wananchi kuathirika, Nchi kama Nchi itaathirika pakubwa zaidi kwa kuwa itashindwa hata kupata misaada kutoka mashirika ya Kimataifa katika kuudhibiti ugonjwa. So hakuna sababu yoyote ya sreikali kuficha linapotokea janga kama hilo.
Wakati mwingine kabla hujatoka hadharani na kutupa hoja yako, jaribu kujiridhisha kwa kufanya utafiti kidogo
Tatizo lako ni kwamba unadandia taaluma za watu. Ungeijua epidemiolojia ya Maburg na Ebola wala usingeendeleza hii hoja. Jambo kama hulijui usilikomalie kwa hoja za hisia, ulizia kwa wanaofahamu wakupe ufafanuzi ndg.