Tunaposema Sera za CCM zimeshindwa hatutanii, mfano hai huu..

Tunaposema Sera za CCM zimeshindwa hatutanii, mfano hai huu..

301102_518863438129478_1120496333_n.jpg
Wapo baadhi yetu ambao wanaamini kuwa "sera za CCM ni nzuri ila zimekosa watekelezaji tu". Wapo wanaoamini kuwa sera hizi ni nzuri sana vitabuni ila hazijapata watu wazuri kuweza kuzifanyia kazi. Wengine wamefikia kuamini kuwa uzuri wa sera hizi unasababisha hata nchi jirani kuzi"copy" na kuzi"paste" kwenye mipango yao. Wale wenye kuamini hivi hatimaye huamini kuwa siku moja CCM itaweza kupata watu wazuri wa kuzitekeleza sera zake - hadi hivi sasa inaonekana watu hao hawapo. Miaka hamsini ya kutawala ati hawajapatikana watu wakuzitekeleza sera hizi vizuri.

Sisi wengine tunasema siyo tu wamekosa watu wa kuzitekeleza bali hata wakipata watu wazuri kiasi gani sera hizo hazitekelezeki. Hazitekelezeki kwa sababu ni sera mbovu zilizoandikwa kwa maneno mazuri. Kwa watu wanaopenda maneno matamu ni rahisi sana kuhadaika na sera hizo.

Mfano mzuri ni hili la Kenya kutuwekea ngumu mabasi yetu ya kubeba watalii (tour buses) kutumia viwanja vyao kwa ajili ya watu wetu kubeba watalii na kuja nao Bongo. Ukiangalia kwa haraka haraka utaona kuwa ni matokeo ya kushindwa kwa sera mbalimbali; kuanzia ya usafiri, uchukuzi, uchumi n.k Sasa watu wengine wanapolalamikia Kenya na kuona kama Wakenya hawaoneshi kujali udugu na ujirani mwema wanasahau kuwa ukipanda mbigili usitegemee kuvuna mpunga! Tunavuna tulichopanda.

Inawezekana vipi katika mipango yetu yote na matumizi yote ya hela kwa miaka hamsini na ushee bado tunategemea huruma na hisani ya majirani zetu kufanikisha mojawapo ya kinachoitwa ni sekta muhimu sana? Hivi kwa muda wote huo watawala wetu walioshindwa wamekuwa wakinufaika kwa sababu ya huruma ya Kenya? Hivi wamesahau kabisa historia? Cha jirani siyo chako; hata kama kakuazima.


Kwamba kisa ni masuala ya sheria ya miaka 30 iliyopita ambayo inaonekana kushindwa kwenda na wakati au mahitaji nalo linathibitisha tu kushindwa kwa viongozi wetu. Hivi hatuwezi kufikiri mbali hadi itokee migogoro? Inawezekana kweli watawala wetu wanaendeshwa na matukio na siyo maono yenye kueleweka? Wengine wanasema na sisi tulipize kisasi; sawa lakini mwisho wake ni nini? Inaonekana kwenye utalii sisi ndio tuko kwenye huruma ya Wakenya.

Angalia kwenye sekta nyingine vile vile utaona tatizo hili la kushindwa kwa sera zao liko wazi japo hatujapata watu wenye kulionesha hili bayana. Miye nimedokeza kitu ambacho kiko dhahiri. Cha kushangaza na kusikitisha kuwa wapo baadhi yetu bado wanafikiria kuwapa tena watu wale wale miaka mingine mitano ya kujaribu sera zile zile ambazo zimethibitika kushindwa huko nyuma ati kwa vile watakuwa na sura tofauti. Kwani tatizo letu sisi sura? Ni sera.

Kama kuna mtu anasema wana sera nzuri; naombeni hata mfano mmoja wa maana wa uzuri wa sera zao.

mwanakijiji sema neno lolote kwenye mada hii ukizingatia kipindi hiki cha uchaguzi.
 
Last edited by a moderator:

Wapo baadhi yetu ambao wanaamini kuwa "sera za CCM ni nzuri ila zimekosa watekelezaji tu". Wapo wanaoamini kuwa sera hizi ni nzuri sana vitabuni ila hazijapata watu wazuri kuweza kuzifanyia kazi. Wengine wamefikia kuamini kuwa uzuri wa sera hizi unasababisha hata nchi jirani kuzi"copy" na kuzi"paste" kwenye mipango yao. Wale wenye kuamini hivi hatimaye huamini kuwa siku moja CCM itaweza kupata watu wazuri wa kuzitekeleza sera zake - hadi hivi sasa inaonekana watu hao hawapo. Miaka hamsini ya kutawala ati hawajapatikana watu wakuzitekeleza sera hizi vizuri.

Sisi wengine tunasema siyo tu wamekosa watu wa kuzitekeleza bali hata wakipata watu wazuri kiasi gani sera hizo hazitekelezeki.

tehteh........
cc: Pasco,TeamLowassa,[URL="https://www.jamiiforums.com/member.php?u=60503"]VUTA-NKUVUTE,[/URL]Ocampo four,[URL="https://www.jamiiforums.com/member.php?u=138049"]Lizaboni, [/URL]Kibo10,
 
Mhhhh!
HAKUNA ANAYEFANIKIWA KWA KUMSHUSHA ALIYE JUU! Huu mchezo wa kudhani ushindi unakuja kwa kunyooshea chama tawala vidole, hata sijui umetoka wapi na ni nani amedanganya kwamba hiyo ndio siri!
Wanaoendekeza siasa hizi wamesahau kabisa; la muhimu kwa wananchi ni SERA; sio bahati nasibu; na sio ujuzi wa kunyosheena vidole.
*Thread hii inazungumzia "Sera" mbovu za CCM! ...
Kweli? Zipo wapi sera "mbadala"?
Huwa ninasikiliza sana zile hotuba za "mawaziri vivulil"... Tafadhali nisaidie... ni lini umesikia waziri kivuli akitangaza sera "mbadala"? NI rahisi sana kupiga mawe kilichopo mezani! LAkini ukweli ni kwamba; hadi hapo wapinzani watakapoweka sera zao mezani? Maneno haya yote ni bure tu!
Dawa kamili ya "sera mbovu" ni kutoa sera "mbadala"; na kuhakikisha "sera hizo mbadala" zinafanyiwa kazi... kuanzia kwenye
halmashauri ambazo "wapinzani ndio watawala".
WEKENI SERA MBADALA, sera zinazoeleweka kirahisi, na tuonyesheni mfano wa mafanikio!
Leo ni February; IWAPO kwa miezi hii michache iliyobaki watu mtaendelea na siasa za kunyooshea "vidole"; na hakuna mawazo/sera mbadala... nadhani ni haki tu niseme "mjiandae kisaikolojia".
Peace!
umewahi kujiuliza ni kwanini wabunge wa upinzani wanatimuliwa bungeni na kubaki chama tawala kikipitisha hoja???
 
Cha kushangaza na kusikitisha kuwa wapo baadhi yetu bado wanafikiria kuwapa tena watu wale wale miaka mingine mitano ya kujaribu sera zile zile ambazo zimethibitika kushindwa huko nyuma ati kwa vile watakuwa na sura tofauti. Kswani tatizo letu sisi sura? Ni sera.
Hapa ndipo ninaposimamia, Cha kushangaza na kusikitisha!, washindani wakubwa ni wawili tuu!, Edward Lowassa na JPM, ukishauri watu wasimchague Lowassa, hata bila kusema wamchague nani, unamanisha wamchague JPM, hivyo sasa ni heri uchague wale wale kuliko kubadilika?!.

Pasco
 
Tuseme huyu mzee wetu kuja na sera ya elimu kwanza inaweza kuwa na msaada mkubwa sana au mnaonaje kwa hili?
 
hapa ndipo ninapokubaliana na mfanyabiashara Mengi kuwa 'tuwe na akiba ya maneno' unaweza kuumbuka siku moja
 
mwisho chechemea ni 25/10/2015 magufuli arudi chato kupalilia karanga na maharage yake, ni upumbavu mkubwa sanavkuendelea kuipigia kura ya ndiyo ccm. swali langu: Kahama, Geita, na hadi Buzwagi hivi sasa zinaelea juu kutokana na kazi kubwa mno inayoendelea chini ya uchimbaji wa dhahabu katika eneo hilo: Je hivi watanzania wenzagu tutalifukia na nini hilo shimo kubwa kama jehanamu? je unaweza kutuambia ni faida gani Tanzania yetu imepata kutokana na dhahabu inayochimbwa eneo hilo? je ulishamsikia magufuli analiongelea swala hilo ndani ya bunge ukizingatia dhahabu inachimbwa karibu kabisa na nyumba kwao?

je hivi wewe unakubali kabisa eti Mkapa pamoja na usomi wake huo alisain serikali ipate Tsh 3 katika 100? je bado unadanganywa kuwa ccm inahuruma na watanzania waliopo sasa na wale watakao ishi miaka 100 ijayo; na je umewahi kujiuliza ni kwanini Mkapa alisaini mpaka miaka 100 ijayo? je unafikiri dhahabu ya Geita na Kahama itakuwa bado ipo mpaka mda huo ukizingatia wazungu wameteremsha mashine mpya na zenye nguvu na zina fanyakazi 24hrs? je umewahi kujiuliza ni kwa nini Rais wetu Kikwete amesaini haraka sana mikataba ya gase?

Sisi tunaoshuhudia haya tunabaki tunalia usiku na mchana tukijililia sisi wenyewe na watanzania watakao ishi miaka 80 ijayo; je ni kwanini serikali inalipa deni la dowans huku ikijipiga kifua kuwa kamwe haimjui mmiliki wake? zinduka!! ihurumie nchi yako inayobakwa na watawala wetu tokea enzi ya uhuru: jitokeze kupiga kura ya ndiyo kwa Ukwa ili angalau tuondoe kabisa mfumo wa kifisadi uliojengwa na watawala wetu; tunahitaji kuondoa ile nadharia ya uchama tawala maana kupitia huo Watanzania tunaibiwa hasa ukizingatia wengi wetu hatuna uwezo wa kuujua utajiri wa Taifa letu hii ni kutokana na ukweli kwamba wengi wetu hatukuenda shule; maana ni shule pekee ndiyo itampa mtu kujua geografia ya nchi yake: Sema ndiyo kwa LOWASSA kwa ajili ya mabadiliko na utaiokoa nchi yako.
 
301102_518863438129478_1120496333_n.jpg

Wapo baadhi yetu ambao wanaamini kuwa "sera za CCM ni nzuri ila zimekosa watekelezaji tu". Wapo wanaoamini kuwa sera hizi ni nzuri sana vitabuni ila hazijapata watu wazuri kuweza kuzifanyia kazi. Wengine wamefikia kuamini kuwa uzuri wa sera hizi unasababisha hata nchi jirani kuzi"copy" na kuzi"paste" kwenye mipango yao. Wale wenye kuamini hivi hatimaye huamini kuwa siku moja CCM itaweza kupata watu wazuri wa kuzitekeleza sera zake - hadi hivi sasa inaonekana watu hao hawapo. Miaka hamsini ya kutawala ati hawajapatikana watu wakuzitekeleza sera hizi vizuri.

Sisi wengine tunasema siyo tu wamekosa watu wa kuzitekeleza bali hata wakipata watu wazuri kiasi gani sera hizo hazitekelezeki. Hazitekelezeki kwa sababu ni sera mbovu zilizoandikwa kwa maneno mazuri. Kwa watu wanaopenda maneno matamu ni rahisi sana kuhadaika na sera hizo.

Mfano mzuri ni hili la Kenya kutuwekea ngumu mabasi yetu ya kubeba watalii (tour buses) kutumia viwanja vyao kwa ajili ya watu wetu kubeba watalii na kuja nao Bongo. Ukiangalia kwa haraka haraka utaona kuwa ni matokeo ya kushindwa kwa sera mbalimbali; kuanzia ya usafiri, uchukuzi, uchumi n.k Sasa watu wengine wanapolalamikia Kenya na kuona kama Wakenya hawaoneshi kujali udugu na ujirani mwema wanasahau kuwa ukipanda mbigili usitegemee kuvuna mpunga! Tunavuna tulichopanda.

Inawezekana vipi katika mipango yetu yote na matumizi yote ya hela kwa miaka hamsini na ushee bado tunategemea huruma na hisani ya majirani zetu kufanikisha mojawapo ya kinachoitwa ni sekta muhimu sana? Hivi kwa muda wote huo watawala wetu walioshindwa wamekuwa wakinufaika kwa sababu ya huruma ya Kenya? Hivi wamesahau kabisa historia? Cha jirani siyo chako; hata kama kakuazima.


Kwamba kisa ni masuala ya sheria ya miaka 30 iliyopita ambayo inaonekana kushindwa kwenda na wakati au mahitaji nalo linathibitisha tu kushindwa kwa viongozi wetu. Hivi hatuwezi kufikiri mbali hadi itokee migogoro? Inawezekana kweli watawala wetu wanaendeshwa na matukio na siyo maono yenye kueleweka? Wengine wanasema na sisi tulipize kisasi; sawa lakini mwisho wake ni nini? Inaonekana kwenye utalii sisi ndio tuko kwenye huruma ya Wakenya.

Angalia kwenye sekta nyingine vile vile utaona tatizo hili la kushindwa kwa sera zao liko wazi japo hatujapata watu wenye kulionesha hili bayana. Miye nimedokeza kitu ambacho kiko dhahiri. Cha kushangaza na kusikitisha kuwa wapo baadhi yetu bado wanafikiria kuwapa tena watu wale wale miaka mingine mitano ya kujaribu sera zile zile ambazo zimethibitika kushindwa huko nyuma ati kwa vile watakuwa na sura tofauti. Kwani tatizo letu sisi sura? Ni sera.

Kama kuna mtu anasema wana sera nzuri; naombeni hata mfano mmoja wa maana wa uzuri wa sera zao.

Kama wangekuwa na sera nzuri tungeona uzuri huo unajitokeza pia kwenye kuandika katiba mpya maana idadi kubwa ya wajumbe walikuwa ni kutoka ccm na wenyeviti wa kamati pia wengi walikuwa kutoka ccm. Utaalamu huo tungeuona pia ukijitokeza bungeni wakati wa kujadili na kupitisha bajeti na sheria. Lakini badala yake kulikuwa mbwembwe na kupitisha sheria kiubabe! Kuendelea kuamini kuwa chini ya ccm nchi hii itabadilika na kuwa ya asali na maziwa ni kujidanganya kwa hali ya juu. Mfumo chakavu wa ccm unatakiwa uachwe na badala yake tuwe na mfumo mpya usiotokana na ccm. Wanaoogopa mabadiliko wafikirie pia kama waasisi wetu wangeogopa kujitawala tungekuwa bado tuko chini ya wakoloni. Kila mabadiliko yanaleta changamoto zake - inabidi tuzikabili na hatimaye tuanze kuona matunda ya mabadiliko. Kuna msemo unasema: "Cowards die many times before their real death." Hivyo, kuogopa kubadilika ni sawa na kufa kabla ya kufa kwenyewe hakujafika.
 
sera za ccm ni kuua tembo,vifaru,na kupandisha twiga kwenye ndege na kupeleka udongo ulaya ili kufanya utafiti wa madini ,tumebakiwa na mahandaki makubwa.
 
Acha ulofa wewe mtoa maada kama sio ccm ungekua hapo ulipo we we?
 
sera za ccm ni kuua tembo,vifaru,na kupandisha twiga kwenye ndege na kupeleka udongo ulaya ili kufanya utafiti wa madini ,tumebakiwa na mahandaki makubwa.

Kwa nini sasa Chadema wachukue mtu aliyetoka hukohuko na kushiliki hayo yote ndo awe mgombea? Huyo si ataibadilisha Chadema kuwa CCM nyingine?
 
jumbo+px.jpg

Hii biashara mwisho wake ni October 25.
 
MM njoo huku maana jamaa wanapekuwa makabrasha.
 
M.M.M Akiwa Katika Ubora Wake, Kabla Ya Kukutana Padri Muasi Usa. Sasa Unayameza Matapishi
 
Back
Top Bottom