Tunaposikia ya Makamba na Zitto kutaka kubinafsisha TANESCO, tukumbuke yaliyofanyika TTCL

Tunaposikia ya Makamba na Zitto kutaka kubinafsisha TANESCO, tukumbuke yaliyofanyika TTCL

kmbwembwe

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2012
Posts
10,892
Reaction score
7,780
Kuna mashirika ya Serikali kutokana na wajibu wake ni kama idara za Serikali. Yanatakiwa yagharamikiwe na hazina kuu. Yanafanywa mashirika ili kuweza kudhibiti matumizi na kwamba iwepo tija.

Ukitaka kugeuza TANESCO liwe la kibiashara moja kwa moja kwanza utapata muwekezaji gani? Lazima awe wa nje na atakua na nguvu gani ya kisiasa nchini? Yeye atataka faida tu na umeme ndio roho ya uchumi wa nchi.

Sisi tunamlenga nani kuhusu maendeleo? Raia wa kawaida au wawekezaji kutoka nje? Lazima umeme utakua bei mbaya kwa raia wapiga kura na ndio mfarakano utaanzia hapo.

Hii mambo ya kubinafsisha sijui asili mia 20 TANESCO ni ile ile habari ya kubinafsisha TTCL. Wajanja wakawagawia wahindi hisa za TTCL kwa bei ya bure wakati serikali ishawekeza mabilioni. Kisha wajanja kushirikiana na wahindi wakakwapua celltel kampuni ya TTCL ya simu za mikononi.

Ikawa wahindi wameshika jikoni TTCL wakikamua hela za umma kwa ruzuku za serikali eti ni wabia wa TTCL. Magufuli akaja kuwafukuza wahindi na kuirejesha kampuni yake ya mkononi kwa kuhakikisha serikali inapewa hisa stahiki.

Sio kila anayejidai ana uthubutu ana uwezo au nia nzuri. Mashirika kama TANESCO au TTCL sio ya kuwekwa sokoni kama njuku.

Wanaoweza kuyaendesha kwa kufikia malengo yake kwa nchi kama Tanzania hakuna. Ni watanzania gani utawashawishi kuwekeza tanesco?

Hivi unaweza mshawishi mtu awekeze kwa gereza. Gereza linaweza kua mradi wa kibiashara? ..sina hakika wala sijaona. Lakini si lazima magereza yawepo? Kuna mambo lazima yawe jukumu la serikali. Ndio maana kuna kodi.

Tukikubaliana na uhuni huu wa january na zitto akijidai mpendekezaji wa hoja tunaona yale ya TTCL, TRC, na ule mradi wa umeme wa makaa kule Songwe mbeya uhuni ule wa simon group kuhusu uda na kwingine.

La kufanyika ni uongozi imara wa kisiasa usiyokua na mchezo kudhibiti mashirika makubwa ya umma kuhakikisha hakuna ubadhirifu na inakwepo tija.
 
Zito ni starter kwenye gari hivyo ujue katumwa kuwasha gari engine ikopokea yeye hana kazi tena fikiria ikipelekwa mswada bungeni wa kuuza his za tannesco utafanyaje kwenye bunge hili ndiyo maana tunataka katiba mpya,wananch tukichagua viongozi wapewe uongozi wasifanyiwe fitina naserikali kuwaapisha waliopendwa na rais.
 
Hivi kwanini tusiruhusu mashirika huru ya umeme kuanzishwa ili kuondokana na tatizo la umeme nchini?
maana kiukweli TANESCO ni wamezidiwa ile mbaya.

Yako yanazalisha umeme na kuiuzia Tanesco. Wakina Ruge na pitieli yao. Labda useme yaruhusiwe na kuweka nguzo zao kusambasa umeme kumfikishia mlaji wa mwishoi.

Nyuki wameshaingia kwenye mzinga wa babu uitwao nishati wajukuu wanafanya maandalizi ya kuanza kurina asali wagawane wale. Ninachojua asali ukivaimia kwa pupa na kuanza kuifakamia mwisho wa siku lazima uitapike tu au utapishwe. Watapishaji ni akina mamaD.
 
Chochote kilichobinafsishwa Kwa ufasaha kinafanya vizuri sana!!!...NBC,NMB,CRDB unajua kwanini umeme unaleta shida kila siku?.. Shirika hili la Tanesco halina mshindani ndio maana hata ufanisi ni sifuri!!!..Unajiuliza kwanini Taasisi kama hii ambayo ina vyuo vyake inashindwa kuwa na weledi kwenye kuhudumia wananchi?!!.. Tanesco lazima wabinafsishe tukitaka twende mbele lakini kama tutaendeleza huu utumbo hakika siku nchi itakua kiza yote na hakuna wakusema!!
 
Wakati Magufuli anaonyesha kiburi cha madaraka kwa kuhujumu upinzani mlikuwa mnachekelea kuwa ccm imeimarika.

Leo wamebaki CCM wenyewe na hawataki kukosolewa, matokeo yake chain ya wapigaji inaanza kurudi ndio mnalialia.

Acha hao wahuni warudi kwenye ulaji, na wauze kila kitu kwa bei ya kutupa ili siku nyingine mjue balance of power maana yake ni nini.

Akina Januari na wahuni wenzenu uzeni hiyo TANESCO bei ya kutupwa ili mliokuwa mnafurahia siasa na chaguzi za kishenzi mjifunze.
 
Huo upuuzi wa kubinafsisha TANESCO pelekeni huko na Zitto wenu. Nendeni tu hapo Kenya kwa mabepari muone Kama wamebinafsisha KENGEN au KPLC. Shenzi kabisa vibaraka nyie
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Kuna mashirika ya serikali kutokana na wajibu wake ni kama idara za serikali. Yanatakiwa yagharamikiwe na hazina kuu. Yanafanywa mashirika ili kuweza kudhibiti matumizi na kwamba iwepo tija.
Ukitaka kugeuza tanesco liwe la kibiashara moja kwa moja kwanza utapata muwekezaji gani? Lazima awe wa nje na atakua na nguvu gani ya kisiasa nchini? Yeye atataka faida tu na umeme ndio roho ya uchumi wa nchi. Sisi tunamlenga nani kuhusu maendeleo? Raia wa kawaida au wawekezaji kutoka nje? Lazima umeme utakua bei mbaya kwa raia wapiga kura na ndio mfarakano utaanzia hapo.
Hii mambo ya kubinafsisha sijui asili mia 20 tanesco ni ile ile habari ya kubinafsisha ttcl. Wajanja wakawagawia wahindi hisa za ttcl kwa bei ya bure wakati serikali ishawekeza mabilioni. Kisha wajanja kushirikiana na wahindi wakakwapua celltel kampuni ya ttcl ya simu za mikononi. Ikawa wahindi wameshika jikoni ttcl wakikamua hela za umma kwa ruzuku za serikali eti ni wabia wa ttcl. Magufuli akaja kuwafukuza wahindi na kuirejesha kampuni yake ya mkononi kwa kuhakikisha serikali inapewa hisa stahiki.
Sio kila anayejidai ana uthubutu ana uwezo au nia nzuri. Mashirika kama tanesco au ttcl sio ya kuwekwa sokoni kama njuku. Wanaoweza kuyaendesha kwa kufikia malengo yake kwa nchi kama tanzania hakuna. Ni watanzania gani utawashawishi kuwekeza tanesco? Hivi unaweza mshawishi mtu awekeze kwa gereza. Gereza linaweza kua mradi wa kibiashara? ..sina hakika wala sijaona. Lakini si lazima magereza yawepo? Kuna mambo lazima yawe jukumu la serikali. Ndio maana kuna kodi.
Tukikubaliana na uhuni huu wa january na zitto akijidai mpendekezaji wa hoja tunaona yale ya ttcl na ule mradi wa umeme wa makaa kule songwe mbeya uhuni ule wa simon group kuhusu uda na kwingine.
La kufanyika ni uongozi imara wa kisiasa usiyokua na mchezo kudhibiti mashirika makubwa ya umma kuhakikisha hakuna ubadhirifu na inakwepo tija.
Du kazi kweli kweli, haya mawazo ya kijamaa ndio yanayoturudisha nyuma. Mashirika mengi ya umma yalikufa haya kama TANESCO yameendelea kuwepo kwasababu tu yanapatiwa ruzuku serikalini ambayo ni kodi za wananchi tunalipia uzembe wote na wizi wote katika shirika hili. Dawa ya haya yote ni kilivunja shirika hili kuwa katika sehemu 3 au mbili generation and trasmission na distribution and collection of revenue. Yabinafsishwe kwa uwazi na kuzingatia sheria yunaweza kutafuta uzoefu kwenye mataifa mengine. Na kuweka vigezo vitakavyolinda maslahi ya Taifa kwa uwazi na kwa faida ya walaji. Generation ndio vital watupe ememe usio na kutetereka na penalt incase of default. mfano gas/ nuclear could be the cheapest source of power, sisi tumekimbilia water generation. Kurudi kwenye mashirika ya umma ni ngumu kumeza.
 
Shida kubwa ni kwenye kubinafsisha huku na negotiations za watu wetu unaweza kuliangamiza Taifa. Ubinafsi na uchu wa kijitajirisha ndio tatizo kubwa kwa nchini nyingi za Kiafrica. Mikataba sio ya wazi na hata mingine hazipelekwi Bungeni. Au zinapelekwa je Wabunge wapo keen enough? Shida sio ubinasfishaji ni jinsi ya kuingia mikataba yenye manufaa kwa WaTZ.
 
Makamba na Zitto msijaribu hata kidogo kubinafsisha tanesco
Kuna mashirika ya serikali kutokana na wajibu wake ni kama idara za serikali. Yanatakiwa yagharamikiwe na hazina kuu. Yanafanywa mashirika ili kuweza kudhibiti matumizi na kwamba iwepo tija.
Ukitaka kugeuza tanesco liwe la kibiashara moja kwa moja kwanza utapata muwekezaji gani? Lazima awe wa nje na atakua na nguvu gani ya kisiasa nchini? Yeye atataka faida tu na umeme ndio roho ya uchumi wa nchi. Sisi tunamlenga nani kuhusu maendeleo? Raia wa kawaida au wawekezaji kutoka nje? Lazima umeme utakua bei mbaya kwa raia wapiga kura na ndio mfarakano utaanzia hapo.
Hii mambo ya kubinafsisha sijui asili mia 20 tanesco ni ile ile habari ya kubinafsisha ttcl. Wajanja wakawagawia wahindi hisa za ttcl kwa bei ya bure wakati serikali ishawekeza mabilioni. Kisha wajanja kushirikiana na wahindi wakakwapua celltel kampuni ya ttcl ya simu za mikononi. Ikawa wahindi wameshika jikoni ttcl wakikamua hela za umma kwa ruzuku za serikali eti ni wabia wa ttcl. Magufuli akaja kuwafukuza wahindi na kuirejesha kampuni yake ya mkononi kwa kuhakikisha serikali inapewa hisa stahiki.
Sio kila anayejidai ana uthubutu ana uwezo au nia nzuri. Mashirika kama tanesco au ttcl sio ya kuwekwa sokoni kama njuku. Wanaoweza kuyaendesha kwa kufikia malengo yake kwa nchi kama tanzania hakuna. Ni watanzania gani utawashawishi kuwekeza tanesco? Hivi unaweza mshawishi mtu awekeze kwa gereza. Gereza linaweza kua mradi wa kibiashara? ..sina hakika wala sijaona. Lakini si lazima magereza yawepo? Kuna mambo lazima yawe jukumu la serikali. Ndio maana kuna kodi.
Tukikubaliana na uhuni huu wa january na zitto akijidai mpendekezaji wa hoja tunaona yale ya ttcl na ule mradi wa umeme wa makaa kule songwe mbeya uhuni ule wa simon group kuhusu uda na kwingine.
La kufanyika ni uongozi imara wa kisiasa usiyokua na mchezo kudhibiti mashirika makubwa ya umma kuhakikisha hakuna ubadhirifu na inakwepo tija.
na
 
Rais Magufuli alipoliunda upya shirika la ndege na kufanya ndege kuwa za serikali na Air Tanzania kukodi ndege hizi ili wazifanyie biashara was very fine. Je shirika hili linaloiingizia Taifa hasara linawajibishwaje? Mimi nilifikiri approach could be any bidder could bid kuendesha Air Tanzania kibiashara kwa kutumia ndege za Serikali na kuilipa serikali kodi ya kukodi ndege and kulipa kodi ya biashara wanayoifanya kwenye faida zao.
 
Wakati Magufuli anaonyesha kiburi cha madaraka kwa kuhujumu upinzani mlikuwa mnachekelea kuwa ccm imeimarika. Leo wamebaki ccm wenyewe na hawataki kukosolewa, matokeo yake chain ya wapigaji inaanza kurudi ndio mnalialia. Acha hao wahuni warudi kwenye ulaji, na wauze kila kitu kwa bei ya kutupa ili siku nyingine mjue balance of power maana yake ni nini. Akina Januari na wahuni wenzenu uzeni hiyo TANESCO bei ya kutupwa ili mliokuwa mnafurahia siasa na chaguzi za kishenzi mjifunze.
CCM hakuna wanachoshindwa, watatumia hadi jeshi kupitisha wanachotaka
Unakumbuka wakati wa JK, pamoja na akina Lissu na lema kupinga sana mikataba ya gesi bado CCM waliipitisha usikuusiku kwa hati ya dharura.
 
Back
Top Bottom