Getrude Mollel
JF-Expert Member
- Apr 26, 2022
- 270
- 362
Sidhani kama kuna mtu atabisha kwamba, kwenye nchi hii hakuna wakati sekta ya kilimo imepata mazingatio makubwa sana kuliko wakati wowote ule kwenye historia ya nchi yetu.
Ushahidi wa kwanza wa hoja yangu ni Rais Samia Suluhu kuongeza bajeti ya kilimo kwa zaidi ya asilimia 200, kutoka TZS Bilioni 294 2021/22 hadi TZS Trilioni 1.3 2024/25. Kiwango cha ongezeko hili, hakijapata kutokea kwenye ardhi ya Taifa lote chini ya kiongozi yeyote.
Lengo na mapinduzi haya ni nini? Kwanza, ni kufanya sekta hii ichangia 10% kwenye Pato la Taifa ifikapo 2030, kuongeza ajira kwa kuzalisha ajira mpya zaidi ya milioni 3 kwa vijana ifikapo 2025 (BBT), kuifanya Tanzania kama muuzaji mkubwa wa chakula barani Afrika na duniani na pia, kutengeneza mazingira ya kuwa na chakula cha kutosha nchini.
Kutoka na uwekezaji huu, muda huu Tanzania ina uteshelevu wa chakula wa zaidi ya asilimia 124, kiwango kikuwa zaidi kuwahi kutokea nchini. Hii imetokana na Rais Samia Suluhu kusimamia ujenzi wa vihenge na maghala mapya ya kuhifadhia chakula katika Kanda nane nchini zenye hifadhi ya chakula ambazo ziko chiini ya NFRA.
Ili ujue kwamba Rais Samia yuko serious kwenye kilimo, bajeti ya utafiti na uzalishaji wa mbegu imeongezwa kwa asilimia 250, huku bajeti ya kuhudumia ma afisa ugani vijijni ikipata kutoka TZS 600 milioni hadi TZS Bilioni 17.7, hakika haya ni mapinduzi makubwa sana na hayapaswi kupuuzwa hata kidogo.
Baada ya miaka kadhaa mbele, naona kabisa ndogo ya kuifanya Tanzania kuwa the 'Africa Food Basket' inakwenda kutimia, tumeongeza eneo la umwagiliaji na hadi kufikia 2025 eneo litakuwa limefikia hekta zaidi ya 1,000,000, kuna skimu mpya za umwagiliaji zaidi ya 20 zinajengwa muda huu na serikali inazidi kuimarisha vyama vya ushirika nchini na hivi majuzi kwenye maandimisho ya siku ya Nane Nane, Mama amekabidhi matrekta mapya 500 na Powertillers 800 kwa wakulima, lengo ikiwa ni matrekta 10000 na powertiller idadi hiyohiyo, zisambazwe kwa wakulima nchi nzima kabla ya kufika 2030.
Ushahidi wa kwanza wa hoja yangu ni Rais Samia Suluhu kuongeza bajeti ya kilimo kwa zaidi ya asilimia 200, kutoka TZS Bilioni 294 2021/22 hadi TZS Trilioni 1.3 2024/25. Kiwango cha ongezeko hili, hakijapata kutokea kwenye ardhi ya Taifa lote chini ya kiongozi yeyote.
Lengo na mapinduzi haya ni nini? Kwanza, ni kufanya sekta hii ichangia 10% kwenye Pato la Taifa ifikapo 2030, kuongeza ajira kwa kuzalisha ajira mpya zaidi ya milioni 3 kwa vijana ifikapo 2025 (BBT), kuifanya Tanzania kama muuzaji mkubwa wa chakula barani Afrika na duniani na pia, kutengeneza mazingira ya kuwa na chakula cha kutosha nchini.
Kutoka na uwekezaji huu, muda huu Tanzania ina uteshelevu wa chakula wa zaidi ya asilimia 124, kiwango kikuwa zaidi kuwahi kutokea nchini. Hii imetokana na Rais Samia Suluhu kusimamia ujenzi wa vihenge na maghala mapya ya kuhifadhia chakula katika Kanda nane nchini zenye hifadhi ya chakula ambazo ziko chiini ya NFRA.
Ili ujue kwamba Rais Samia yuko serious kwenye kilimo, bajeti ya utafiti na uzalishaji wa mbegu imeongezwa kwa asilimia 250, huku bajeti ya kuhudumia ma afisa ugani vijijni ikipata kutoka TZS 600 milioni hadi TZS Bilioni 17.7, hakika haya ni mapinduzi makubwa sana na hayapaswi kupuuzwa hata kidogo.
Baada ya miaka kadhaa mbele, naona kabisa ndogo ya kuifanya Tanzania kuwa the 'Africa Food Basket' inakwenda kutimia, tumeongeza eneo la umwagiliaji na hadi kufikia 2025 eneo litakuwa limefikia hekta zaidi ya 1,000,000, kuna skimu mpya za umwagiliaji zaidi ya 20 zinajengwa muda huu na serikali inazidi kuimarisha vyama vya ushirika nchini na hivi majuzi kwenye maandimisho ya siku ya Nane Nane, Mama amekabidhi matrekta mapya 500 na Powertillers 800 kwa wakulima, lengo ikiwa ni matrekta 10000 na powertiller idadi hiyohiyo, zisambazwe kwa wakulima nchi nzima kabla ya kufika 2030.