Tunataka kuishitaki wizara ya afya, nisaidieni kujua kampuni nzuri ya mawakili

Mkipata wakili mzuri hoi kesi mnatoboa
 
Hii sio lazima iwe kampuni, kama itawapendeza nitawapa mtu ambae anaweza akaisimamia kesi yenu kwa makubaliano yenu (maalum) kwenye % and trust me mtachana nyavu

Watachana nyavu? Haya ndo majibu mepesi ya proffesionals wa Tanzania, ujapafa hata fact moja ya kesi, ushaahidi uahindi?
 
Poleni Sana Sana 😥😴😥
 
On a top of that ,Tuna vielelezo 16 na Mashahidi 4 ,wawili wanatoka nje ya nchi (Professors )kutoka vyuo tulivyosomea
 
Wanasheria saidieni vijana hawa !Naomba mguswe katika hili Jitoleeni kuwasaidia
 
On a top of that ,Tuna vielelezo 16 na Mashahidi 4 ,wawili wanatoka nje ya nchi (Professors )kutoka vyuo tulivyosomea
Itakua india? Ikishindikana sana angalieni namna nyingine tena naona mmepozeza muda mwingi sana kupelekeshana na hawa wabongo wakati mgeshatoboa nchi nyingine na kupiga kazi. Sio lazima ufanye kazi tz botswana na namibia wana uhitaji mkubwa wa MDs na mishahara ni mara kumi ya Tz.
 
Soma vizuri chief ,tumesoma vyuo vikuu tofauti tofauti ,nchi tofauti tofauti na kwa miaka tofauti tofauti
Kila nchi inataratibu zake so usilazimishe maana hata hiyo milion 4 utaipoteza bure, kiukweli ni ngumu kupewa leseni sio tz tu unless hukohuko mlikosomea au nchi zenye uhitaji wa madaktari maana kama US MD anasoma mpaka miaka 7 kabla ya 2 years of internship , cuba 6years ya darasani tu na practical 2 years internship , russia 7 ya darasani tu, South Afrika 6 years ya darasani excluding internship, Canada wanasoma mpaka miaka 10plus internship, sasa wewe mwenye degree ya miaka 4 nani atakuamini?
Hata ukienda hizo nchi nilizokutajia hawakupi leseni itabidi urudi shule tu. Sister wangu yuko SA ni doctor ila ilimbidi akaongeze ujuzi kwanza hawakuiamini degree yake ya miaka mitano ya muhimbili maana wao ni miaka sita. So ushauri wa bure timkieni nchi zenye uhitaji kama namibia na botswana ila kama mnafungua kesi fungueni ila ukweli mchungu ni kwamba hamtapewa hizo leseni hiyo idara ya afya ni sensitive sana so kabla ya kwenda kusoma nje lazima ufanye research vizuri sana. Sio nyie tu wapo wengi wamesoma china na malaysia wamerudi hawatambuliki ni noma yani.
 
Uko sawa ndiyo msingi wa kesi yetu ni watuambie wapi kuna madhaifu,ndiyo maana hata wewe umekiri kuwa dada yako ni daktari USA (HONGERA SANA INAONEKANA UNATOKA FAMILIA BORA) ,lakini alilazimika kusoma tena ili kukubalika katika nchi husika na dhani alirudia miaka michache . Nasisis ndicho tulicho kiomba tukanyimwa ,tuliomba ikiwa kuna madhaifu ingawa sisi hatu yaoni,watusaidie kuongeza ujuzi kuliko kutunyanyasa
 
Hapana sio USA ni SA south africa, hapana sitoki wealthy family ni struggle zake mwenyewe. Kila lakheri mkuu. Ila vikishindikana pita njia nyingine nyie ni watu muhimu sana na kama sio hapa tz bdo ni muhimu kwingine .
 
Mkuu niliandika uzi juzi Kuhusu hii ishu
Barua ya wazi kwa Dkt. David Mnzava the Medical council of Tanganyika "Secretary and registrar"(The MCT registrar and secretary of the board)

watu wakaniona Mi natetea ujinga Na wengine Wakadhihaki but meeen This issue is serious sana watu hawajui watu wanapitia nini
Nilitamani kuongea vitu kuhusu baraza letu lakini sheria haziniruhusu kuwa lower "esteem" baraza letu tukufu lakini kuna mahali naona hakuo sawa Sasa sijui ni baraza au ni Wizra ya afya ,Just imagine Course inafnana kwa kila kitu ila wanazuia just because hukusoma Tanzania Meehn hatuwez wote kusoma Tanzania,Kila mtu ana machaguo yake...
Hauko peke yako mkuu kuna jopo kubwa la watu wanaoumia na kulia sema sheria na Kanuni za baraza zinawabana hawawez kuongea machungu yao ila trust me this is serias issue but...again trust me This issue mtatuzi wake sio TCU,Wala mahakama hii issue ili iishe Try kucommunicate na CHAMA CHA SHIRIKISHO LA MADAKTARI AU Chama cha shirikisho la vyama vya madaktari MAT i think wanaweza kukaa chini na MCT baada ya kuexamine vithibitisho vyote na kwakuwa baadhi ya member wa shirikisho ni Membee pia wa MCT you can win this but no Mahakama inaweza kuamua kesi ya kiproffessional kama hiyo ambayo Registrar kapewa mamlaka makubwa ya kuamua kusajili au kutokusajili kulingana na kanuni alizopewa.
 
mnaweza kuishtaki nakuomba mahaka iiamuru kufanya au kubadili msimamo wao
Me nachomshauri asishtaki kwanza arudi mezani tena wakae wote na ikibidi aite pia viongozi wa shirikisho (MAT) na Viongozi wa wizara ikiwemo daktari mkuu wa serikali CMO (Chief medical officer),Katibu mkuu wa wizara (au mwakilishi) na mwakilishi kutoka Kutoka TCU sana sana awe ni Wa abroad study quality asessment, na Wote wakae meza moja na Naamin watafikia Muafaka kwa pamoja wakiwa mbalimbali wote watarupiana mpira na muafaka haufopatikana.

My take:
kesi hii kuipeleka mahakamani trust me itakushinda na utajikuta umepoteza Kesi na sio tu kesi hata usajili wako utakuwa nullfied according to Medical, dental and allied health acts no 11 ya mwaka 2017 ibara ya 7 power of the council na pia kama utapata kijinafasi kapitie hiyo sheria mkuu ndo utanielewa nachosema zaidi ukisoma ibara ya 17 ya sheria hiyo inasema wanasema
............"Bila ya kujali masharti ya sheria nyingine yoyote iliyoandikwa, hakuna hatua au shauri lolote litakalowekwa au kufunguliwa dhidi ya mjumbe yeyote wa Baraza au kamati zake, au baraza kwa ujumla au afisa au mfanyakazi yeyote wa Baraza kwa au kuhusiana na kitendo au jambo lolote lililofanywa au kuachwa. ifanywe kwa nia njema katika utekelezaji wa madaraka yaliyotolewa na Sheria hii.".......
Mkuu usiwaone hawajui wanachofanya they know how to play with cards
Sasa jitahidi kwanza ukae nao ukiona napo haujaridhika unakata rufaa kwenye juu zaidi kama mahakama na vinginevyo
 
Mkuu kuna mtu kasoma Msc Cardiology na mwingine kapiga Msc ya urology na kuna mwingine wamepiga Msc in neurology ambazo hzo kwa nchi za wenzetu hutolewa kwa Wale walio na bachelor degree walipokuja Tz wakaambiwa hawana sifa za kusoma kwa sabbu mtaala wa Tz unaruhusu kusma kozi hizo baada ya MMED (master ya medicine) kwahyo wakanyimwa Licence fo perfom as a specialist na wakaambiwa wataendelea kutambulika kama MD just a plain Medical practitioner as A General P.
kwahyo mkuu naelewa maumivu yako naelewa unavyooitia ila ipeleke hii ishu polepole usije ukapoteza haki yako
Ya kwangu ni hayo tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…