Tunaweza kuwa na kombe la muungano (April 26) kwa timu za taifa za bara (Tanganyika) na visiwani (Zanzibar) kwa wachezaji wa ligi za ndani tu?

Tunaweza kuwa na kombe la muungano (April 26) kwa timu za taifa za bara (Tanganyika) na visiwani (Zanzibar) kwa wachezaji wa ligi za ndani tu?

Infantry Soldier

JF-Expert Member
Joined
Feb 18, 2012
Posts
15,892
Reaction score
16,476
Mambo vp JamiiForums

Sasa tunalo kombe la mapinduzi kwa vilabu kutoka Tanganyika na Zanzibar, kwanini tushindwe kuwa na kombe la muungano (April 26) mechi moja tu kwa timu za taifa za bara (Tanganyika) na visiwani (Zanzibar) kwa wachezaji wa ligi za ndani tu? Lilianza mwaka 1982 na kufa mwaka 2003.

Timu ya taifa ya Zanzibar
=====
gftrfvbg.jpg

Ninasema ni kombe la muungano kwa wachwzaji wa ligi za ndani nikiwa na maana mchezaji wa Zanzibar anayecheza ligi ya Tanganyika hatoitwa katika kikosi cha timu yake ya taifa na vivyo hivyo kwa mchezaji wa Tanganyika anayecheza ligi kuu ya Zanzibar.

Tunataka kuona viwango combination ya vijana wa Malindi, Mlandege, K.M.K.M, Kipanga na Jang'ombe Boys wakiwa wanacheza kwa pamoja. Ni wachezaji wa vilabu vya ndani tu, akina Samatta hatutawaita katika muktadha huu

HISTORIA NDOGO YA KOMBE LA MUUNGANO
==========
Ligi ya Muungano ilianza rasmi mwaka 1982 lengo ni kudumisha Muungano wetu na kutoa usawa wa kiuwakilishi katika michuano ya kimataifa ya vilabu, hii ni kutokana na Tanzania bara kuwa na ligi yake na Zanzibar kuwa na ligi yake.

Upande wa pili (Zanzibar) ukiwa sio mwanachama wa shirikisho la soka barani Africa caf, hivyo kukosa sifa ya timu zake kushiriki michuano ya vilabu bingwa africa na kombe la washindi (ilijulikana hivyo miaka hiyo).

Kwa kuwepo kwa ligi ya Muungano ambayo ilikuwa inajumlisha timu 3 zilizomaliza nafasi juu kwenye ligi husika basi timu kutoka Zanzibar nazo zilipata nafasi ya kuiwakilisha Jamhuri ya Muungano kwenye michuano ya CAF.

Moja ya timu iliyofanya vizuri sana kimataifa katika uhai wa miaka 21 ya michuano hiyo kwa upande wa Zanzibar ni timu ya Malindi.

Leo hii ni miaka 18 sasa tangu michuano ya ligi ya Muungano ife, michuano ambayo ilifanyika kwa miaka 21 mfululizo. Lakini kama wasemavyo wahenga "Tumbo la shari huzaa kheri" kwa namna moja iliwafungua macho Zanzibar kuomba uanachama CAF ili vilabu vyake vishiriki michuano ya kimataifa.

Sababu michuano hii ilikuwa inafanyika December nimeona sio vibaya tukakumbushana kidogo. Pale ambako unaona rekodi hazipo sawasawa unaweza kuwasiliana nami.
==========

SWALI: Tunaweza kuwa na kombe la muungano (April 26) kwa timu za taifa za wanaume bara (Tanganyika) na visiwani (Zanzibar) kwa wachezaji wa ligi za ndani tu?

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
 
Ni gharama kwa sisi walipa kodi, maumivu plus
Gharama kwa mechi moja tu? Mapinduzi ina mfululizo wa mechi mbona hamlalamikii gharama? Umewaza kuhusiana na suala zima la kampuni za udhamini (sponsorship)?
 
Mnyika na Mbowe wanavyotawanya pesa za ruzuku kwa matumizi ya familia zao sio gharama kwa walipa kodi? Nyumbu wa ufipa mnapaswa kuwa Milembe Dodoma.
Watakuja kukurukia kama mwewe. Subiri uone. Mimi sio mwanasiasa mkuu.
 
Sababu ilizofanya hayo mashindano kuwepo miaka hiyo ya nyuma, kutoa atakae cheza champions league na winners cup, kwa sasa haipo tena, kama yakirejeshwa yatakuwa hayana mvuto kama yalivyo Mapinduzi cup kwa sasa, itakuwa ni wastage of time and resources.
 
kama yakirejeshwa yatakuwa hayana mvuto kama yalivyo Mapinduzi cup kwa sasa, itakuwa ni wastage of time and resources.
Umefanya research wapi na kujua kuwa hayana mvuto? Ni mara ngapi timu za taifa za bara za visiwani zinacheza mechi ya pamoja? Hivi unajua tanganyika hasimu wake mkubwa wa soccer ni Zanzibar kuliko Kenya?
 
Sababu ilizofanya hayo mashindano kuwepo miaka hiyo ya nyuma, kutoa atakae cheza champions league na winners cup, kwa sasa haipo tena, kama yakirejeshwa yatakuwa hayana mvuto kama yalivyo Mapinduzi cup kwa sasa, itakuwa ni wastage of time and resources.
Hii ni hoja mufilisi mdogo wangu
 
Umefanya research wapi na kujua kuwa hayana mvuto? Ni mara ngapi timu za taifa za bara za visiwani zinacheza mechi ya pamoja? Hivi unajua tanganyika hasimu wake mkubwa wa soccer ni Zanzibar kuliko Kenya?
Mfano halisi kwa sasa kuna Mapinduzi cup, yanayohusisha timu kutoka bara na visiwani, yana mvuto gani? zaidi ya timu kama Simba kupeleka kikosi B chake, au wale wachezaji ambao hawajapata nafasi kucheza VPL, na wachezaji wanaofanya trials tu.
 
Mfano halisi kwa sasa kuna Mapinduzi cup, yanayohusisha timu kutoka bara na visiwani, yana mvuto gani?
Mkuu, kama hayana mvuto kwako usisemee nafsi za watanzania wote kila mmoja ana mapenzi yake
 
Back
Top Bottom