Tunda la mzeituni

Tunda la mzeituni

Mwanzoni Mungu aliruhusu watu waoe dada zao, hivyo Kaini alioa dada yake. Ili kuendeleza uzao, ilibidi Lot azae na watoto wake, na wakati huo haikuwa big deal, Mungu aliruhusu.

Sasa jiulize: Kaini alipooa alikuwa na umri gani?

Kumbuka kwamba Biblia huwa haiongelei watoto wa kike, unaweza kuona ni ubaguzi lakini it is what it is. Hivyo Biblia haiongelei watoto wa kike ambao Adam na Eva walizaa, ambao ni wazi walitawanyika kwenda sehemu nyingine, pamoja na huko nchi ya Nod. Na huenda walishatawanyika miaka mingi labda hata 100, wakati Kaini alipowafuata dada zake huko waliko ili aoe mmoja wao. Hivyo si ajabu Adamu alioa akiwa na zaidi ya miaka 100, wakati labda ana dada zaidi ya 50 waliotawanyika sehemu mbalimbali

Kama unaamini kwamba Mungu aliumba mtu kwa mara ya kwanza aliposema na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa nini huamini mtu huyo alikuwa Adam kama Biblia inavyosema? Na kama Mungu alikuwa ameshaumba watu, kwa nini aseme na tufanye mtu kwa mfano wetu kama vile ndio anafanya kwa mara ya kwanza, na hata kuona ni mpweke kwa kutokuwa na mwenzi, na kumuumba Eva, ikiwa tayari kulikuwa na watu wengine sehemu fulani?

Yaani angalia isivyo na lojiki; Mungu aumbe watu zaidi ya Adam, halafu baada ya hapo aseme na tufanye mtu kwa mfano wetu, na kuumba mtu na kumuweka mbali na wengine aliokwisha waumba, kisha aone huyo mtu mwingine aliyemuumba mbali na wengine, Adam, ni mpweke, badala ya kumpeleka kule waliko watu wengine aliowaumba anaamua kuumba tena, Eva. I say, Biblia sio kitabu kigumu kiasi hicho, ni uwezo wa kutafakari mambo tu.
Nimekuelewaaaaa yaaani barikiwa
 
Voda wakikuambia ili ujiunge na kifurushi basi bonyeza *. ...# usipofanya hivyo basi airtime itatumika kwa gharama kubwa zaidi lakini bado kuna watu wanalalamika wameonewa. Tunda lilisimama badala ya choice kwamba ukichagua hii basi kitakachofuata ni hivi . Kutii ni kuheshimu unachoambiwa.
Asante
 
Hadithi yako imejaa maneno haya ya kufikirika; labda, huenda, pengine, nk.

Katika habari ukishaingiza dhana basi hadithi nzima inabeba dhana ya kufikirika.

Unaposema kaini huenda alioa dada yake, nikuulize kwanini leo mtu kuoa dada yake imekatazwa???
Hizi mila za kutokuoa ndugu yako zimejengwa na wanadamu tu ni sawa na sheria za nnchi .
 
Hizi mila za kutokuoa ndugu yako zimejengwa na wanadamu tu ni sawa na sheria za nnchi .


Kama hujui uliza au kafanye tafiti kwanini mtu kuoa dada yake imekatazwa, ukipata jibu ndipo utaona kwamba isingewezekana kwa Kaini kuoa dada yake.
 
Ndio mkuu.Zaituni tulizonazo ni zile za matunda na sio zile zinazotumika kutengenezea mafuta.
zitastawi vizur sana maana Israel zastaw na wanasema mikoa ya singda na dom gografic yake ni sawa sawa na jerusalem.
 
Hadithi yako imejaa maneno haya ya kufikirika; labda, huenda, pengine, nk.

Katika habari ukishaingiza dhana basi hadithi nzima inabeba dhana ya kufikirika.

Unaposema kaini huenda alioa dada yake, nikuulize kwanini leo mtu kuoa dada yake imekatazwa???
Kwa hiyo dhana kwamba Adamu alipoumbwa kulikuwa na watu wengine unaona ni rahisi kuamini kuliko niliyosema? Kama ni hivyo wewe mtu wa kuhurumiwa sana. Kizazi cha wasioamini, wana wa uharibifu.

Swali lako kwa nini baadae Mungu alikataza mtu kuoa dada yake ilikuwa ni sababu ya kisayansi. Mwanzoni Adamu aliumbwa na genes ziko perfect, hazina tatizo kabisa. Watoto wa Adamu na Eva walikuwa pia near perfect. Adamu aliishi miaka 930. Sasa wakati huo kwa kuwa genes za binadamu zilikuwa perfect haikuwa tatizo mtu kuzaa na dada yake, au mwanaume kuzaa na watoto zake kama Lot aliyeokolewa Sodoma na Gomora. Pia kuwa na genes near perfect ilifanya wawe na afya na kuishi miaka mingi. Mke wa Abrahamu alimzaa Isaka akiwa na miaka zaidi ya 90.

Kadiri miaka ilivyopita mwanadamu alizidi kupata genes zisizo perfect. Na hili mara nyingi linatokea ndani ya family kunakuwa na genes fulani dhaifu au zenye kuleta tatizo fulani. Kwa mfano rahisi, sema ndani ya familia yenu mnazaliwa na genes zenye kuleta kansa. Sasa wewe na dada yako mnaoana, mnaweza kuzaa mkazi-amplify genes zenye tatizo la kansa, mkajikuta mnazaa watoto wanapata kansa kabla hata ya miaka kumi. Lakini ukioa mtu mwenye genes tofauti na zenu, basi mkizaa inaua makali ya genes za kansa ambazo ukoo wenu unazo, au magonjwa mengine. Kama ukoo wenu una katatizo kadogo ka ukichaa kamejificha hakaonekani sana, na ukazaa na dada yako, mnaweza kuzaa mtoto kichaa wa kutupwa!

Ndio maana Mungu baadae, wanadamu walivyodhoofika na kuishi miaka chini ya 200, aliwakataza kuzaa na dada zao au ndugu zao wa karibu, japo hakuwafafanulia kwa nini.
 
Adam sio mtu wa kwanza kuumbwa bali yeye alikuwa mtu wa kwanza kuongea na Mungu au alikuwa mtu wa kwanza kupokea ufunuo wa miongozo kutoka kwa Mungu.

Katika Dini ya Uisilamu Adam anacho cheo cha unabii na utume, mtu hawi mtume hadi kuwepo na watu ambamo kwao huyo mtume ametumwa kamwe mtume hawezi tumwa bila ya kuwepo kwanza kuwepo watu, sasa inaposemwa Adam ni mtu wa kwanza maana yake ndiyo hiyo kwamba ni mtu wa kwanza kupokea ufunuo, kuongea na Mungu na kuwa civilized na akawa wa kwanza kuwafundisha watu wake mafundisho ya Mungu.

Kuja kuijaza dunia hiyo ni kanuni ya maumbile ya wanadamu na wanyama pia, wanyama pia nao huijaza dunia katika njia ileile ambayo binadamu huijaza dunia sasa wao wameambiwa wapi waje kuijaza dunia???, kwa maana hiyo maneno "kuijaza dunia" ni maneno yenye maana fulani ya kiroho.


Sasa kwa lengo la mjadala tufanye Adam ndiye mtu wa kwanza kuumbwa na baadaye Hawa akatokea "ubavuni" kwa Adamu na kisha wakazaa watoto wawili Kaini na Habili, hadi hapo walikuwepo Watu 4 (wanne) yaani; Adam, Hawa, Kaini na Habili. Kama utakumbuka imeandikwa ndani ya Biblia kwamba Kaini alimuua Habili kisha akatorokea nchi ya NOD na alipofika huko AKAOA, swali linakuja alioa kitu gani wakati alipomuua nduguye walikuwa wamebaki watu 3 watatu tu??!!, Maana yake ni hii Huko NCHI YA NOD walikuwepo watu wengine wakiishi na ndiyo maana ikaitwa "nchi" ya Nod, sote tunajua eneo likiitwa nchi maana yake watu wanaishi hapo. Huo ni ushahidi kutoka ndani ya Biblia kwamba Adam hakuwa mtu wa kwanza kuumbwa bali walikuwepo watu kabla yake naye Adamu alizaliwa kama watu wengine.

Ukisoma History ni kwamba Adam aliishi maeneo ya Babylon katika makutano ya mito miwili ya Tigris na Yufrata (Tigris and Euphrates) katika Iraq ya leo, aliishi yeye na watu wake "qawm" takriban miaka 6,000 (elfu 6) iliyopita hadi leo, bado historia inasema fuvu la mtu wa kale lilifukuliwa huko Oldivai Gorge lenye umri unaokadiriwa miaka 1000,000 isitoshe bado mafuvu na masalia ya watu wa kale yaliyokuwepo kwa maelgu ya miaka yanazidi kufukuliwa katika sehemu mbalimbali duniani, kulingana na historia kamwe huwezi kusema Adam alikuwa ni mtu wa kwanza kuumbwa bali yeye alikuwa ni mtu wa kwanza kupokea ufunuo, kuongea na Mungu, kuwa civilized au kwa neno zima yeye alikuwa mtu wa kwanza "kuumbwa kiroho"( kuumbwa kiroho maana yake alikuwa mtu wa kwanza kuwa karibu sana na Mungu).

Basi swali linaibuka je Mtu wa kwanza kuumbwa ni nani ??!!--- hilo swali ni gumu kweli kwani utakapolijibu hapohapo yataibuka maswali mengine; Kuku wa kwanza kuumbwa ni yupi?? Mbuzi wa kwanza, Bata wa kwanza, mchungwa wa kwanza, Sisimizi, Fisi, Simba, Ng' ombe nk, wa kwanza kuumbwa ni wepi?!!😒.

Lakini ni lazima kulikuwepo na watu, wanyama, mimea na hata wadudu nk, vya kwanza kuumbwa.

Dunia hii ilivyokuwa leo sio sawa na jinsi ilivyokuwepo billions ya miaka iliyopita, muundo (feature) wa dunia katika miaka hiyo kabla ya UHAI (the origion of life/ genesis) dunia yote ilifunikwa na maji ya uhai (Biotic soup) na nuru ya jua ilikuwa ikishuka mojakwamoja katika uso wa dunia, Biotic soup n8 supu iliyokuwa na mchanganyiko wa elements zilizoweza kuzalisha viumbe hai pale ambapo nuru ya jua iliposhuka moja kwa moja kama "Catalyst" kwenye hiyo supu kuchochea reaction ya kikemikali, kumbuka hiyo nuru ya jua (ultra violet rays) hivi sasa imepunguzwa nguvu yake na "ozone layer" ambapo hapo zama za "biotic soup" hakukuwa na hiyo layer na nuru ilikuja moja kwa moja katika uso wa dunia---- jinsi ambavyo viumbe wametoke duniani ni "Complex mechanism" kifupi ni kwamba hiyo ndiyo njia ya awali ya kisayansi jinsi viumbe hai walivyotokea, kwanza walianza kuumbwa Viumbe wa Baharini katika Biotic soup iliyofunika uso wa dunia, hiyo supu ilipojitenga kufanya Bahari na nchi kavu ndipo viumbe wengine wa nchi kavu wakatokea kama vile mimea na Donasours nk, baadaye sana ndipo Mtu naye akatokea hapo hali ya uso wa dunia tayari ilikuwa imebadilika vya kutosha kuweza kukidhi uhai wa mtu (Watu wa kale kina Zinjanthropus boisei), hapo tayari Ozone layer ilikuwa imeshajitokeza nk, baada ya viumbe kuwepo katika uso wa dunia viumbe hao wakaendelea kuijaza dunia kwa njia ya kujamiiana na watu wa zama hizo walikuwa "primitive sana" hawakumjua Mungu kabisa na miaka ikaenda watu wakiwepo taratibu wakipata ustaarabu hadi zama za Adam ndipo Mungu akaona inafaa kumpa ufunuo huyo Adamu ili awape watu wake ujumbe kutoka kwake Mungu ndipo Adamu akawa mtu wa kwanza kupewa ujumbe kutoka kwa Mungu.

Mungu anazo njia 3 za uumbaji, Uumbaji wa kwanza ni kuumba kutoka katika utupu (creation of something from nothing), uumbaji kutoka katika sehemu ya kitu, na uumbaji wa kuzaliana. Njia ya Uumbaji wa viumbehai wa Mwanzo niliyoieleza ni hiyo njia ya pili.

Njia hiyo ya pili leo bado inatokea duniani; kuna baadhi ya watu wakifungwa POP (hogo) kwa muda fulani litakapoenda kuondolewa utashangaa kukuta ndani kuna chawa wengi, swali hao chawa wametoka wapi???---- ni muunganiko wa chemikali kutoka kwenye POP, ngozi ya mhusika iliyokufa, jasho linalotoka katika mahali ilipofungwa POP, joto la mwilini, hewa ya carbon kutoka katika mwili sehemu ilipofungwa hiyo POP, kutaja kwa uchache tu hizo ni kama "Biotic soup" inaweza kuzalisha chawa ndani ya POP.

Juu ya yote Adam hakuwa mtu wa kwanza KUUMBWA.
unapotosha...
 
Kwa hiyo dhana kwamba Adamu alipoumbwa kulikuwa na watu wengine unaona ni rahisi kuamini kuliko niliyosema? Kama ni hivyo wewe mtu wa kuhurumiwa sana. Kizazi cha wasioamini, wana wa uharibifu.

Swali lako kwa nini baadae Mungu alikataza mtu kuoa dada yake ilikuwa ni sababu ya kisayansi. Mwanzoni Adamu aliumbwa na genes ziko perfect, hazina tatizo kabisa. Watoto wa Adamu na Eva walikuwa pia near perfect. Adamu aliishi miaka 930. Sasa wakati huo kwa kuwa genes za binadamu zilikuwa perfect haikuwa tatizo mtu kuzaa na dada yake, au mwanaume kuzaa na watoto zake kama Lot aliyeokolewa Sodoma na Gomora. Pia kuwa na genes near perfect ilifanya wawe na afya na kuishi miaka mingi. Mke wa Abrahamu alimzaa Isaka akiwa na miaka zaidi ya 90.

Kadiri miaka ilivyopita mwanadamu alizidi kupata genes zisizo perfect. Na hili mara nyingi linatokea ndani ya family kunakuwa na genes fulani dhaifu au zenye kuleta tatizo fulani. Kwa mfano rahisi, sema ndani ya familia yenu mnazaliwa na genes zenye kuleta kansa. Sasa wewe na dada yako mnaoana, mnaweza kuzaa mkazi-amplify genes zenye tatizo la kansa, mkajikuta mnazaa watoto wanapata kansa kabla hata ya miaka kumi. Lakini ukioa mtu mwenye genes tofauti na zenu, basi mkizaa inaua makali ya genes za kansa ambazo ukoo wenu unazo, au magonjwa mengine. Kama ukoo wenu una katatizo kadogo ka ukichaa kamejificha hakaonekani sana, na ukazaa na dada yako, mnaweza kuzaa mtoto kichaa wa kutupwa!

Ndio maana Mungu baadae, wanadamu walivyodhoofika na kuishi miaka chini ya 200, aliwakataza kuzaa na dada zao au ndugu zao wa karibu, japo hakuwafafanulia kwa nini.
Usisumbuke muulize Iceberg9 mtaelewana vizuri huyu jamaa ye habari za kuwa Adam haikuwa wa kwanza ila alikuwa kiroho kuongea na Mungu ni nahis ananichanganyia ugali na zege.
 
Tunda hili navyosikia ndio tunda walilokula Adam na Hawa na ndio hilihili Mungu aliwakataza wasile.

Kama ni Kweli hilo ndio tunda lenyewe naomba nielezee kidogo na kama sitakuwa sahihi mnisahihishe.

Kwanijuavyo ni kuwa maana ya lile tunda walilokatazwa ni kutokufanyana, kwa bahati mbaya wakafanyana na Mungu akawaambia mtazaa kwa uchungu nawe mwanaume mtakula kwa jasho ndio ukawa mwanzo wa kuzaliana mpaka leo kisa tunda (utamu)

Sasa hili tunda la mzeituni ambalo watu ndio wanasema walikatazwa Adam na Hawa wasile na ndio linauzwa dar kwa sh4000/= , hili ni la wapi? Je, ukila hautodhurika? Hamna tafsiri au maana ya ukila hilo tunda la mzeituni?. Mnaojua mtupe matumizi ya hilo tunda na ni kwa nini linauzwa bei kubwa hivyo kuzidi tufaa?

Kama tunda alilowakataza Adam na Hawa linaitwa mzeituni kwanini walipewa adhabu ile? Kwa nini waliambiwa wakaijaze dunia? Kwa nini maandiko mengi ya Biblia inakataza usizini? Je, hamuoni hiyo ndio ilikuwa dhambi ya asili (kuzini) na wala sio kula lile tunda la mzeituni linalouzwa Dar 4000/=?

Kama ni tunda hilo (mzeituni) ndio walikatazwa na sisi tumelijua kwanini bado tunakula?.

Nakaribisha muongozo.
Komamanga 1=10'000/- TZS.
Hoja zako dhaifu unasimamia andiko gani?
Je tunda la mti wa uzima Ni lipi?
 
Kama hujui uliza au kafanye tafiti kwanini mtu kuoa dada yake imekatazwa, ukipata jibu ndipo utaona kwamba isingewezekana kwa Kaini kuoa dada yake.
Lakini mkuu kwanini mgumu km nyundo?

Hakuna pahala pameandikwa marufuku kuoa Dada yako vinginevyo hatua Kali itachukuliwa.

Hivo swala la kutokuzalishana ndugu kwa ndugu ni ukuaji wa elimu ya Dini,, na mpaka sasa kuna makabila wanazaana yaani mjomba atamzalisha mtoto wa dada yake na wala hamna sheria inayomfunga.



Sema tu lile tunda alilokula Adam na hawa limefanyakazi vema mpaka sasa, kwani mwanzo waliona aibu wako uchi siku zilivokwenda binadam akaona aibu kuzaa na ndugu yake vile vile hata kuvaa kyupi ya mdogo wako huwezi hii ni moja ya faida ya ulaji wa lile tunda kiasi kwamba tunajitambua sana hadi HAYA tunaona tufanyapo jingajinga.
 
Komamanga 1=10'000/- TZS.
Hoja zako dhaifu unasimamia andiko gani?
Je tunda la mti wa uzima Ni lipi?
Nilipotaja tunda sikumaanisha lazima liwe hilo na ndio maana nikasema mwongozo tafadhari!

Na unaposema tunda la mti wa uzima yote hayo ni juu yako kunieleza ni tunda linaitwaje na je ni la kuliwa kupitia mdomoni km matunda mengine?


Ukumbuke Maelezo yangu sijaleta km najua kila kitu vizuri,, nimeishia na kuomba mwongozo.
 
Kwa hiyo dhana kwamba Adamu alipoumbwa kulikuwa na watu wengine unaona ni rahisi kuamini kuliko niliyosema? Kama ni hivyo wewe mtu wa kuhurumiwa sana. Kizazi cha wasioamini, wana wa uharibifu.

Swali lako kwa nini baadae Mungu alikataza mtu kuoa dada yake ilikuwa ni sababu ya kisayansi. Mwanzoni Adamu aliumbwa na genes ziko perfect, hazina tatizo kabisa. Watoto wa Adamu na Eva walikuwa pia near perfect. Adamu aliishi miaka 930. Sasa wakati huo kwa kuwa genes za binadamu zilikuwa perfect haikuwa tatizo mtu kuzaa na dada yake, au mwanaume kuzaa na watoto zake kama Lot aliyeokolewa Sodoma na Gomora. Pia kuwa na genes near perfect ilifanya wawe na afya na kuishi miaka mingi. Mke wa Abrahamu alimzaa Isaka akiwa na miaka zaidi ya 90.

Kadiri miaka ilivyopita mwanadamu alizidi kupata genes zisizo perfect. Na hili mara nyingi linatokea ndani ya family kunakuwa na genes fulani dhaifu au zenye kuleta tatizo fulani. Kwa mfano rahisi, sema ndani ya familia yenu mnazaliwa na genes zenye kuleta kansa. Sasa wewe na dada yako mnaoana, mnaweza kuzaa mkazi-amplify genes zenye tatizo la kansa, mkajikuta mnazaa watoto wanapata kansa kabla hata ya miaka kumi. Lakini ukioa mtu mwenye genes tofauti na zenu, basi mkizaa inaua makali ya genes za kansa ambazo ukoo wenu unazo, au magonjwa mengine. Kama ukoo wenu una katatizo kadogo ka ukichaa kamejificha hakaonekani sana, na ukazaa na dada yako, mnaweza kuzaa mtoto kichaa wa kutupwa!

Ndio maana Mungu baadae, wanadamu walivyodhoofika na kuishi miaka chini ya 200, aliwakataza kuzaa na dada zao au ndugu zao wa karibu, japo hakuwafafanulia kwa nini.


Mwandishi wa Kitabu cha mwanzo ni Nabii Musa (Mosses), huyo alikuwa ni mtu wa Mungu kwa maana hiyo lazima utazame maandiko yake kwa mtazamo wa kiroho zaidi.

Dhana yako kwamba Adam alikuwa mtu wa kwanza kuumbwa inazo kasoro kubwa na wala haiingii akilini kwa mtu anayefikiri, shida iliyopo kwenu mnasoma maandiko ya kiroho yaliyokuwa mafumbo (metaphoricals) na kuyafanya dhahiri (literals).

Inaposemwa Eva alitokea ubavuni mwa Adam--- hiyo ni metaphor, na maana yake ni kwamba Eva aliendana na Adam kitabia kiasi kwamba wangeishi vyema kama mume na mke, inaposemwa Adam ni mtu wa kwanza maana yake ni yeye alikuwa ni mtu wa kwanza kuongea na Mungu.

Inaaminiwa kimakosa kwamba Adam na Eva ndiyo waliotuzaa wanadamu watu wote duniani hivyo watu wote wazazi wetu ni Adam na Hawa, sasa iweje kuna wazungu, Waafrika, native Americas, Aborigines nk, wote hao wakiwa na Genetic make up tofauti??, wazungu au Waafrica au Aborigines Genes (DNA) ni tofauti kati yao, hii maana yake ni kwamba kila race inacho chanzo na ndiyo maana kuna huo utofauti wa DNA.

Unaposema kwamba Genes za Akina Adam zilikuwa perfect inabidi ulete uthibitisho tujue ni mtaalamu gani alipima hiyo perfection.

Unadai Luti alizaa na wanawe (Mungu apishe mbali), lakini hukusema ni katika mazingira gani huyo Luti alifanyishwa uchafu huo, hujui kwamba alileweshwa kwanza??!!--- kwani mtu mwenye akili timamu hawezi kufanya uchafu huo mbaya zaidi na bintiye!!! ndiyo maana wakamlewesha ili akili imtoke.

Bado nasisitiza kamwe haiwezekani huyo Adam awe ni mtu wa kwanza kuumbwa na awe ndiye aliyezaa watu wote duniani, never ever.

Huyo Adam aliyeishi takriban miaka 6,000 iliyopita awe ndiye aliyemzaa Zinanthropus Boisei aliyeishi katika Bonde la Oldivai takriban miaka 1000,000 iliyopita???!!🤣🤣 hata akili ya kichaa haitakubali kwamba Adam ni wa kwanza kuumbwa.

Kumbuka Nabii Nuhu ni kitukuu wa Adamu huyo mnayemsema ni mtu wa kwanza kuumbwa.
 
Lakini mkuu kwanini mgumu km nyundo?

Hakuna pahala pameandikwa marufuku kuoa Dada yako vinginevyo hatua Kali itachukuliwa.

Hivo swala la kutokuzalishana ndugu kwa ndugu ni ukuaji wa elimu ya Dini,, na mpaka sasa kuna makabila wanazaana yaani mjomba atamzalisha mtoto wa dada yake na wala hamna sheria inayomfunga.



Sema tu lile tunda alilokula Adam na hawa limefanyakazi vema mpaka sasa, kwani mwanzo waliona aibu wako uchi siku zilivokwenda binadam akaona aibu kuzaa na ndugu yake vile vile hata kuvaa kyupi ya mdogo wako huwezi hii ni moja ya faida ya ulaji wa lile tunda kiasi kwamba tunajitambua sana hadi HAYA tunaona tufanyapo jingajinga.


Wewe ni mgumu kama Almas.

Kama kuoa dada yako ni sawa, wewe unaona aibu ya nini??? Aibu yako juu kuoa dada yako inatoka wapi?? Au unaogopa nini???

Hata mbuzi angekula lile tunda naye angevaa nguo???.

Akili za kuambiwa changanya na-------.
 
Yaani Maelezo baadhi yapo fresh ila hili la uwepo wa watu wengi kipindi cha Adam nahisi wenge Kali ku mkichwa.
Mwanzo 1: 27 Basi Mungu akamuumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimuumba; mwanamume na mwanamke aliwaumba.

hapo inasema Mwanaume na Mwanamke na sio wanaume na wanawake
 
Sasa kama tunda ni kuto kukunjana ,sasa na ile kauli ya "Enendeni mkaijaze dunia" mbona inakuwa haina mashiko?
 
Kwa kukusaidia tu biblia bila usaidizi wa rohomtakatifu kamwe hutaelewa!. Kabla ya kuanza kuisoma omba mwongozo wa msaada wa rohomtakatifu kwanza akusaidie kuelewa ujumbe huo wa Mungu naamini utakuja kutoa ushuhuda hapa.!!
Mtu huwa akisema omba usaidizi wa roho mtakatifu huwa ndo nachanganyikiwa zaidi
 
Sasa kama tunda ni kuto kukunjana ,sasa na ile kauli ya "Enendeni mkaijaze dunia" mbona inakuwa haina mashiko?
Wengi hapo juu

Tunda wamesema ni UTII
Sasa hiyo ya enendeni mkaijaze dunia jichanganye kivyovyote maana siielewi iliingilianaje.
 
Tena alimuumba mwanaume tuuuu,, baadae akaonaanyofoe ubavu wa mwanaume huyo ili ampatie msaidizi (mwanamke) lakini jomba Mokaze kanivuruga kbsaaa.
Mwanzo 1: 27 Basi Mungu akamuumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimuumba; mwanamume na mwanamke aliwaumba.

hapo inasema Mwanaume na Mwanamke na sio wanaume na wanawake
 
Back
Top Bottom