Tunda la mzeituni

Nimekuelewaaaaa yaaani barikiwa
 
Asante
 
Hizi mila za kutokuoa ndugu yako zimejengwa na wanadamu tu ni sawa na sheria za nnchi .
 
Hizi mila za kutokuoa ndugu yako zimejengwa na wanadamu tu ni sawa na sheria za nnchi .


Kama hujui uliza au kafanye tafiti kwanini mtu kuoa dada yake imekatazwa, ukipata jibu ndipo utaona kwamba isingewezekana kwa Kaini kuoa dada yake.
 
Ndio mkuu.Zaituni tulizonazo ni zile za matunda na sio zile zinazotumika kutengenezea mafuta.
zitastawi vizur sana maana Israel zastaw na wanasema mikoa ya singda na dom gografic yake ni sawa sawa na jerusalem.
 
Kwa hiyo dhana kwamba Adamu alipoumbwa kulikuwa na watu wengine unaona ni rahisi kuamini kuliko niliyosema? Kama ni hivyo wewe mtu wa kuhurumiwa sana. Kizazi cha wasioamini, wana wa uharibifu.

Swali lako kwa nini baadae Mungu alikataza mtu kuoa dada yake ilikuwa ni sababu ya kisayansi. Mwanzoni Adamu aliumbwa na genes ziko perfect, hazina tatizo kabisa. Watoto wa Adamu na Eva walikuwa pia near perfect. Adamu aliishi miaka 930. Sasa wakati huo kwa kuwa genes za binadamu zilikuwa perfect haikuwa tatizo mtu kuzaa na dada yake, au mwanaume kuzaa na watoto zake kama Lot aliyeokolewa Sodoma na Gomora. Pia kuwa na genes near perfect ilifanya wawe na afya na kuishi miaka mingi. Mke wa Abrahamu alimzaa Isaka akiwa na miaka zaidi ya 90.

Kadiri miaka ilivyopita mwanadamu alizidi kupata genes zisizo perfect. Na hili mara nyingi linatokea ndani ya family kunakuwa na genes fulani dhaifu au zenye kuleta tatizo fulani. Kwa mfano rahisi, sema ndani ya familia yenu mnazaliwa na genes zenye kuleta kansa. Sasa wewe na dada yako mnaoana, mnaweza kuzaa mkazi-amplify genes zenye tatizo la kansa, mkajikuta mnazaa watoto wanapata kansa kabla hata ya miaka kumi. Lakini ukioa mtu mwenye genes tofauti na zenu, basi mkizaa inaua makali ya genes za kansa ambazo ukoo wenu unazo, au magonjwa mengine. Kama ukoo wenu una katatizo kadogo ka ukichaa kamejificha hakaonekani sana, na ukazaa na dada yako, mnaweza kuzaa mtoto kichaa wa kutupwa!

Ndio maana Mungu baadae, wanadamu walivyodhoofika na kuishi miaka chini ya 200, aliwakataza kuzaa na dada zao au ndugu zao wa karibu, japo hakuwafafanulia kwa nini.
 
unapotosha...
 
Usisumbuke muulize Iceberg9 mtaelewana vizuri huyu jamaa ye habari za kuwa Adam haikuwa wa kwanza ila alikuwa kiroho kuongea na Mungu ni nahis ananichanganyia ugali na zege.
 
Komamanga 1=10'000/- TZS.
Hoja zako dhaifu unasimamia andiko gani?
Je tunda la mti wa uzima Ni lipi?
 
Kama hujui uliza au kafanye tafiti kwanini mtu kuoa dada yake imekatazwa, ukipata jibu ndipo utaona kwamba isingewezekana kwa Kaini kuoa dada yake.
Lakini mkuu kwanini mgumu km nyundo?

Hakuna pahala pameandikwa marufuku kuoa Dada yako vinginevyo hatua Kali itachukuliwa.

Hivo swala la kutokuzalishana ndugu kwa ndugu ni ukuaji wa elimu ya Dini,, na mpaka sasa kuna makabila wanazaana yaani mjomba atamzalisha mtoto wa dada yake na wala hamna sheria inayomfunga.



Sema tu lile tunda alilokula Adam na hawa limefanyakazi vema mpaka sasa, kwani mwanzo waliona aibu wako uchi siku zilivokwenda binadam akaona aibu kuzaa na ndugu yake vile vile hata kuvaa kyupi ya mdogo wako huwezi hii ni moja ya faida ya ulaji wa lile tunda kiasi kwamba tunajitambua sana hadi HAYA tunaona tufanyapo jingajinga.
 
Komamanga 1=10'000/- TZS.
Hoja zako dhaifu unasimamia andiko gani?
Je tunda la mti wa uzima Ni lipi?
Nilipotaja tunda sikumaanisha lazima liwe hilo na ndio maana nikasema mwongozo tafadhari!

Na unaposema tunda la mti wa uzima yote hayo ni juu yako kunieleza ni tunda linaitwaje na je ni la kuliwa kupitia mdomoni km matunda mengine?


Ukumbuke Maelezo yangu sijaleta km najua kila kitu vizuri,, nimeishia na kuomba mwongozo.
 


Mwandishi wa Kitabu cha mwanzo ni Nabii Musa (Mosses), huyo alikuwa ni mtu wa Mungu kwa maana hiyo lazima utazame maandiko yake kwa mtazamo wa kiroho zaidi.

Dhana yako kwamba Adam alikuwa mtu wa kwanza kuumbwa inazo kasoro kubwa na wala haiingii akilini kwa mtu anayefikiri, shida iliyopo kwenu mnasoma maandiko ya kiroho yaliyokuwa mafumbo (metaphoricals) na kuyafanya dhahiri (literals).

Inaposemwa Eva alitokea ubavuni mwa Adam--- hiyo ni metaphor, na maana yake ni kwamba Eva aliendana na Adam kitabia kiasi kwamba wangeishi vyema kama mume na mke, inaposemwa Adam ni mtu wa kwanza maana yake ni yeye alikuwa ni mtu wa kwanza kuongea na Mungu.

Inaaminiwa kimakosa kwamba Adam na Eva ndiyo waliotuzaa wanadamu watu wote duniani hivyo watu wote wazazi wetu ni Adam na Hawa, sasa iweje kuna wazungu, Waafrika, native Americas, Aborigines nk, wote hao wakiwa na Genetic make up tofauti??, wazungu au Waafrica au Aborigines Genes (DNA) ni tofauti kati yao, hii maana yake ni kwamba kila race inacho chanzo na ndiyo maana kuna huo utofauti wa DNA.

Unaposema kwamba Genes za Akina Adam zilikuwa perfect inabidi ulete uthibitisho tujue ni mtaalamu gani alipima hiyo perfection.

Unadai Luti alizaa na wanawe (Mungu apishe mbali), lakini hukusema ni katika mazingira gani huyo Luti alifanyishwa uchafu huo, hujui kwamba alileweshwa kwanza??!!--- kwani mtu mwenye akili timamu hawezi kufanya uchafu huo mbaya zaidi na bintiye!!! ndiyo maana wakamlewesha ili akili imtoke.

Bado nasisitiza kamwe haiwezekani huyo Adam awe ni mtu wa kwanza kuumbwa na awe ndiye aliyezaa watu wote duniani, never ever.

Huyo Adam aliyeishi takriban miaka 6,000 iliyopita awe ndiye aliyemzaa Zinanthropus Boisei aliyeishi katika Bonde la Oldivai takriban miaka 1000,000 iliyopita???!!🤣🤣 hata akili ya kichaa haitakubali kwamba Adam ni wa kwanza kuumbwa.

Kumbuka Nabii Nuhu ni kitukuu wa Adamu huyo mnayemsema ni mtu wa kwanza kuumbwa.
 


Wewe ni mgumu kama Almas.

Kama kuoa dada yako ni sawa, wewe unaona aibu ya nini??? Aibu yako juu kuoa dada yako inatoka wapi?? Au unaogopa nini???

Hata mbuzi angekula lile tunda naye angevaa nguo???.

Akili za kuambiwa changanya na-------.
 
Yaani Maelezo baadhi yapo fresh ila hili la uwepo wa watu wengi kipindi cha Adam nahisi wenge Kali ku mkichwa.
Mwanzo 1: 27 Basi Mungu akamuumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimuumba; mwanamume na mwanamke aliwaumba.

hapo inasema Mwanaume na Mwanamke na sio wanaume na wanawake
 
Sasa kama tunda ni kuto kukunjana ,sasa na ile kauli ya "Enendeni mkaijaze dunia" mbona inakuwa haina mashiko?
 
Kwa kukusaidia tu biblia bila usaidizi wa rohomtakatifu kamwe hutaelewa!. Kabla ya kuanza kuisoma omba mwongozo wa msaada wa rohomtakatifu kwanza akusaidie kuelewa ujumbe huo wa Mungu naamini utakuja kutoa ushuhuda hapa.!!
Mtu huwa akisema omba usaidizi wa roho mtakatifu huwa ndo nachanganyikiwa zaidi
 
Sasa kama tunda ni kuto kukunjana ,sasa na ile kauli ya "Enendeni mkaijaze dunia" mbona inakuwa haina mashiko?
Wengi hapo juu

Tunda wamesema ni UTII
Sasa hiyo ya enendeni mkaijaze dunia jichanganye kivyovyote maana siielewi iliingilianaje.
 
Tena alimuumba mwanaume tuuuu,, baadae akaonaanyofoe ubavu wa mwanaume huyo ili ampatie msaidizi (mwanamke) lakini jomba Mokaze kanivuruga kbsaaa.
Mwanzo 1: 27 Basi Mungu akamuumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimuumba; mwanamume na mwanamke aliwaumba.

hapo inasema Mwanaume na Mwanamke na sio wanaume na wanawake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…