Uchaguzi 2020 Tundu Lissu aache kuzungumzia masuala ya kupigwa risasi kila Mkutano

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu aache kuzungumzia masuala ya kupigwa risasi kila Mkutano

Chidu Mangalili

Senior Member
Joined
Mar 24, 2017
Posts
144
Reaction score
96
Mgombea uraisi kwa tiketi ya Chadem ndg.Tundu A.Lisu anahitaji kuiachilia nafsi yake kwa kusamehe mabaya yaliyomkuta miaka mitatu iliyopita.Kuyaongelea kila mahali ampatapo wa kumsimulia,hasa majukwaa ya kisiasa,kutazidishia machungu kwake na wale wote wanaomhusu.

Niliwahi kumsikia mwenyekiti wake,Mh.Freeman Mbowe, akiongelea kutaka maridhiano ya kisiasa kati ya upande wa upinzani na chama tawala.

Huenda aliona umuhimu wa kuachilia au kutokuendelea kunyoosheana vidole kwa hisia zitokanazo na tofauti za kiitikadi.

Labda Mh.Tundu angepata wasaa wa kumuuliza mwenyekiti wake mantiki ya mrengo huo.

Inawapunguzia pia vyombo vya uchunguzi wa tukio la kushambuliwa kwake uzito wa kuwiwa kijamii na kiuwajibikaji umuhimu wa kulifanyia uchunguzi wa aliyehusika.Kwani litabeba taswira ya "ushabiki au kupuuzia kuwa ni wanasiasa ktk hoja zao za kutafuta kura".

Aliachilie kwa ajili ya nafsi yake na itamuongezea umaarufu zaidi wa kisiasa kwani binadamu wengi hasa wastaarabu wanapenda kusikia neno msamaha kuliko kulipiza au kuendelea kulaani na kushutumu.Ipo mifano mingi,tena ya matukio ya mtendwa na mtendewa kujulikana wazi na jamii.

Pia kuendelea kumhisi mtu kuwa ndie mtekelezaji wa shambulio sio vyema.
Inaleta mpasuku zaidi kiasi kuwa hata kuachia na kusamehe inakuwa ngumu baadae kwani nae yule unampiga risasi za nafsi,huku ukiwa hauna uhakika wa yeye kuhusika atakuwa na majeraha ya nafsi ambayo huwa ni magumu kuachilia bila rehema ya Mungu nae kumwingia.

Hata kama ni mbinu za kutafuta kura basi isiwe kibinafsi kiasi hicho.
Iko siku mtakutana mtataniana kuwa mlichuana bali walio mashabiki wenu mnakuwa mmekwisha watenganisha kwa kujijengea uadui wa nafsi kwa jinsi ya upande waliopo.

Tunajijua Watanzania ni watu wa kukanyagwa bila hata kuuliza kwanini umenikanyaga na kuanzisha vita huwa tunamwambia aliyekukanyaga " samahani",kama umemjua,nae atakuomba samahani pia hata kama alifanya makusudi.
Mungu aliyekuponya ni Mungu wa msamaha,ni Mungu asiyependa kisasi wala kinyongo.

Kuachilia ni ushujaa kwani kunaiweka nafsi huru.Huenda ni mpango wa Mungu hata juu ya sintofahamu ya kipi kinaendelea kiuchunguzi ili kutoa mwanya wa kuyasamehe na maisha yaendelee kwani yeye ameshakuponya dhidi ya adui,tena usiemfahamu bado,naomba kusisitiza kuwa haumfahamu bado.

Usijikite kwenye kumnyooshea kidole mwingine kwani mara zote kiubinadamu huwa tunapenda kumlaumu kwa kila jambo baya litufikalo yule tunaevutana nae juu ya maslahi au Imani zetu.

Una wito wa kufanya siasa,umerudi ulingoni kaza daluga fanikisha uliyoyakusudia.

UTAKUWA UMEPONA MWILI NA NAFSI.
 
Jiweke kwenye nafasi yake uone kama ni rahisi hivyo...kuongea ni tiba bora ya afya ya akili..kuongea huleta nafuu ya fukuto la maumivu makali
Na kwa kufanya hivyo kila mara anapeleka ujumbe muhimu na wa kutisha kwa watesi wake kuwa yuko imara kuliko hata kabla ya shambulio na HAJASAHAU....hajafanya nini!? HAJASAHAU.....!!!!
 
Kupigwa risasi ni hali halisi ya nchi yetu ilipofikia. Kama wewe huoni ni muhimu usisikilize lakini Kwa Watanzania wengi wanataka aongelee ni sawa na kusema Mandela asiongelee kugugwa kila wakati. Hii inaonyesha utoto wa baadhi ya wanajamii hapa. Inawezwkana ujakuwa kiasi cha kuelewa umuhimu wake bado ipo siku utaelewa. Hii issue ni kubwa sana kwako kuielewa
 
Naona umevuviwa ndotoni ili ufikishe ujumbe, ila ninachojua Lissu ni kama Magu, hawashauriki hawa jamaa!
 
Tundu Lisu lazima aongee kuhusu kupigwa risasi kila siku na asiache. Hii inawauma sana ndiyo maana hampendi kusikiliza. Hii inafanya baadhi ya segment ya population kama vile akina mama wajue uovu wa CCM na Viongozi wao. Ukifanya unyama lazima ukubali kuambiwa ukweli. CCM ni Chama cha majambazi. Jambazi mkubwa ni yule anayeongoza, hata remorse ya kupiga risasi 38 na 17 zikampata hajawahi kutubu. Ila kazidi kumfanyia unyama Lisu:
1. Kumyima matibabu ili afe- wakashindwa
2. Wakamkatia mshahara wake Bungeni - wakashndwa
3. Wakamfukuza Bungeni - Bado wanashanagaaa yupo live.

The "Guilty Are Always Afraid"
 
Huyo jamaaaa, asipotumia hiyokiki ya alioigiza ili ije impe promo kwenye uchaguzi huuu na kuwalagai chama chake wamuhurimie agombeee yeye eti kisa anamuujiza, inje yahapo kichani kwa masuala ya kujenga hoja ya kisiasa yuko empty kichwaniii.

Sasa yeye kuchakutwa ni kutushuhudia miujiza, lakini pamoja na umahili wa sheria alionao hatujawahi onatukio lake lile analipereka mahakamani atasikumojaa.


Huu ushuhuda lazima autumie kila kona ilikuutengenezea kiki ya kuhurumiwa kupewa uraisiii.
 
Tueleze kwanza wewe unaijua amani ipi, haudhani mtu kupigwa risasi ni moja ya uvunjifu wa amani na ni kitendo kinachiwatia hofu wananchi.
 
Utakuwa yule Mzee mwenye roho mbaya wewe sio Bure
Ukisikia Lissu anaongelea jinsi Mlivyopanga hadi Mazishi yake Mwili wako unatetemeka kwa Dhambi
 
Acha kuwaza kama mbwia ugoro
Huyo jamaaaa, asipotumia hiyokiki ya alioigiza ili ije impe promo kwenye uchaguzi huuu na kuwalagai chama chake wamuhurimie agombeee yeye eti kisa anamuujiza, inje yahapo kichani kwa masuala ya kujenga hoja ya kisiasa yuko empty kichwaniii.

Sasa yeye kuchakutwa ni kutushuhudia miujiza, lakini pamoja na umahili wa sheria alionao hatujawahi onatukio lake lile analipereka mahakamani atasikumojaa.
Huu ushuhuda lazima autumie kila kona ilikuutengenezea kiki ya kuhurumiwa kupewa uraisiii.
 
Kaona matatizo yake Ndio hoja
Muache
Huyo ndio tuna aminishwa na Vibendera fuata upepo atamuondoa Magufuli
Akili zingine nitaabu tu
 
CCM wamejenga viwanda na ajira fake wanatangaza kila kona. Ungewashauri CCM kwanza waachane na habari za ajira na viwanda fake kila wanapoona mike mbele yao kabla hujamshauri Tundu Lissu kuusema uovu halisi aliofanyiwa na watu wenye mamlaka na sihaha
 
Aliyehusika na jaribio la mauaji ya Lisu anajijua na anajua la kufanya ili kupunguza ama kuondoa tatizo la kuumizwa kwa dhamiri yake.

Anapaswa kuomba msamaha,kutafuta maridhiano kama alivyoambiwawa na Mbowe,aache kushupaza shingo.

Ninyi wafuatao wake mnapaswa kumwambia mhusika aombe msamaha na amlipe Lisu haki zake zote,mambo yatakuwa shwari
 
Back
Top Bottom