Uchaguzi 2020 Tundu Lissu abadili upepo, aanza kumsifu Rais Magufuli

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu abadili upepo, aanza kumsifu Rais Magufuli

eddy

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2007
Posts
16,054
Reaction score
11,568
Lisu katika harakati za kusaka wadhamini akiwa mjini Tanga na Muheza amesifia kazi za awamu ya tano kuwa wanajenga reli mpya bwawa kubwa la umeme na miradi mingi mikubwa. Kafananisha kazi hizo na zile zilizofanywa na watawala wa kizungu na mwalimu nyerere, akasema wajerumani walijenga reli ya Tanga arusha na Dar Kigoma, huku waingereza wakiunganisha Tanga Dar na Tabora Mwanza.

Kasema amekaa ulaya miaka mitatu nao wana miundo mbinu kama ya kwetu na bado wanajenga mingine, hili ni jambo jema sana. Ila nimkumbushe wazungu walitawala miaka 75 na nyerere miaka 25 jumla yao ni miaka 100, JPM atafanya hayo ndani ya miaka kumi tu hongera JPM.

Kasema wajerumani walijenga shule moja tu ya Tanga school, yaani kwa miaka 35 waliyokaa hii nchi walijenga shule moja tu, leo hii tuna shule zaidi ya elfu 20 nchi nzima tena zenye walimu madawati na vitabu watoto hawabebi makwanja wala kuchangishwa fedha ya lebo na madawati.

Kasema nayeye akichaguliwa ataendeleza pale JPM atakuwa kafikia basi kama ni kweli ni jambo jema kabisa, ila basi atuonyeshe angalau ajenge ofisi ya makamu mwenyekiti CHADMA pale Dodoma tuamini hayo anayotuambia, alivyokuwa arusha kakuta ofisi ya chama imechomwa moto achilia kutohamasisha ukarabati wa ofisi hata kutoa mia ya pole hamna, hajazungumzia chochote afya ya mlinzi wala hajaenda kumpa pole. Nasikia ile nyumba niyakupanga sasa chama kitaikarabati au mwenye nyumba shauri yake?
 
Nini kinaendelea hapa?
tenor.gif
 
Ila nimkumbushe wazungu walitawala miaka 75 na nyerere miaka 25 jumla yao ni miaka 100, JPM atafanya hayo ndani ya miaka kumi tu hongera JPM.
Mkuu mimi ninamkubali na kumtetea Magufuli like no other, lakini inapofikia ukweli lazima usemwe.
Magufuli hajafikia hata nusu ya mambo aliyofanya Nyerere, tuache ushabiki wa ajabu ajabu.

Nyerere alijenga vyuo mbali mbali, shule nyingi, barabara kiasi chake, alijenga viwanda vingi sana vilivyo kuwa vinamilikiwa na serikali, alinunua ndege, aliwekeza kwenye mambo mengine mengi.

Magufuli ni kiongozi ninaye mkubali sana lakini bado hajafikia viwango vya Nyerere kila nyanja iwe kiuchumi au kijamii.
 
Mkuu mimi ninamkubali na kumtetea Magufuli like not other, lakini inapofikia ukweli lazima usemwe.
Magufuli hajafikia hata nusu ya mambo aliyofanya Nyerere, tuache ushabiki wa ajabu ajabu.

Nyerere alijenga vyuo mbali mbali, shule nyingi, barabara kiasi chake, alijenga viwanda vingi sana vilivyokuwa vinamilikiwa na serikali, alinunua ndege, aliwekeza kwenye ambo mengine mengi.

Magufuli ni kiongozi ninaye mkubali sna lakini bado hajafikia viwango vya Nyerere kila nyanja iwe kiuchumi au kijamii.

Mie nimeongelea sehemu moja ambayo Lissu kaizungumzia ya ujenzi wa Reli na shule, jpm kakarabati reli yote Dar Tanga Arusha, Dar Tbr kigoma na anajenga nyingine mpya, kwahayo Magufuli ni vyema tumtendee haki tumpe heshima yake, mie sijamfananisha na nyerere la hasha, Ni Lissu kasema anafanya kazi kama Nyerere.
 
You are misguiding us. He said that as a mockery. "Hata wakoloni walijenga reli na barabara". It is a mockery and not a praise. Hotuba yake yote tunayo You-tube. Unapotosha makusudi au hujaielewa. Pole sana.
Mkuu mimi nakubaliana kabisa kuwa maendeleo ni "Multiplier effect" yaani hayana mwisho japan wanaendelea marekani wanaendelea na sisi tunaendelea, tofauti iliyopo kwa JPM ni "speed and efficiency" yake.
 
Kama kweli leo kaongea hivyo basi hayo ni mabadiliko makubwa na ni kiashiria cha kampeni nzuri kwake na kwa mstsksbsli wa amani ya nchi kwa ujumla.
 
Mie nimeongelea sehemu moja ambayo Lissu kaizungumzia ya ujenzi wa Reli na shule, jpm kakarabati reli yote Dar Tanga Arusha, Dar Tbr kigoma na anajenga nyingine mpya, kwahayo Magufuli ni vyema tumtendee haki tumpe heshima yake, mie sijamfananisha na nyerere la hasha, Ni Lissu kasema anafanya kazi kama Nyerere.
Hapo sawa.
Nilitaka kukushangaa sana, Nyerere ni habari nyingine.
Hii elimu bure hadi kidato cha nne kwa Nyerere ilikuwa kuanzia darasa la awali, shule ya msingi, sekondari hadi chuo kikuu.
Tena yeye alienda mbali sana kwa kutoa huduma ya chakula bure cha mchana na kifungua kinywa(uji saa nne asubuhi) shule za msingi, sekondari huko usiseme, vyuo vikuu kulikuwa na mabomba ya maziwa, mikate, matunda, vyakula vya kutosha na likizo watu walilipiwa nauli hadi za ndege na serikali.

Yule mzee hakuwa mtu wa kawaida kama waliomfuatia.
Hii inayo itwa mikopo ya elimu ya juu ilikuwa bure kabisa tena 100%.
Kitu cha kushangaza watu waliofaidika kupitia huduma hii ndiyo walikuja kupiga kura bungeni kupitisha sheria ya bodi ya mikopo na wengine kuandaa kanuni wizarani watu walipe hii fedha kama mikopo.
Wakapanga walipe waliofaidika kuanzia miaka ya 1990 na kitu wakajitoa wao wa miaka ya 80's kurudi nyuma wasilipe huduma hizo walizopewa bure na Nyerere.
Hapo kati nchi ilioza sana kwa ubinafsi na ufujaji mali ya umma, hao wazee kama haitoshi wakabadili muda wa kustaafu wakajiongezea muda ili waendelee kula wao na kuajiri ndugu zao.
Wenzetu wanashusha umri wa kustaafu ili kutoa fursa kwa vijana nao waajiriwe wapate mitaji sisi tunafanya kinyume chake!!!
 
Back
Top Bottom