Uchaguzi 2020 Tundu Lissu aliwahi kuisaidia nini Tanzania? Mwenye uelewa atuelezee

Serikali ya CCM ilivyokuwa haikioendi chadema iliwaacha na ushahidi wote huooo?? Ahahahhahah kichwa panzi wewe, kwa matukio hayo chadrma ingekwishafutwa be maana wangeitwa magaidi
 
Unazeeka vibaya nyau wewe
 
Yeye kila siku Ana hesabu kesi tulizo shtakiwa watanzania yani Tundulisu siwez kumpa kura hata ccm angekua shetani mana hata tundulisu ni shetani mwenzake
 
Uzwazwa ulionao ndio utakaokufanya utukanwe mpaka uwakumbuke wazee wako kijijini, yaani mpaka leo hujajua umuhimu wa lissu? Kwanini hujiulizi kwanini walitaka kumuua mchana kweupe!?


Ungelist tu mkuu..

Kafanya..

1.
2.
3.
...
 
Yeye kila siku Ana hesabu kesi tulizo shtakiwa watanzania yani Tundulisu siwez kumpa kura hata ccm angekua shetani mana hata tundulisu ni shetani mwenzake
Na aliyetuingiza katika kesi hizo unamuachaje kwa mfano! Be rational bro
 
Kwani huyo aliyepo madarakani ametusaidia nini. Ninachoona ni kutumia kodi zetu vibaya. Gharama za hayo Magari yanayomlinda kwa mwaka zinatosha kwa watanzania wote kusoma bure bila ya hata kununua kalamu. Na hayo unayosema anatufanyia kwa kodi zetu wenyewe. Sisi tunataka taasisi imara, ili kiongozi yoyote atakaekaa madarakari aweze kutuletea maendeleo kutokana na sheria zetu na sio Matamko ya mtu fulani
 
Jibu hoja.wanachadema shida sana.ndio mnataka kuchukua nchi ninyi.kama swali dogo kama ili unajibu kwa jazba utaweza wapi kuitetea nchi yako
Kuna watu kama wewe mpaka unashangaa ni ujinga au upumbavu ulionao. Hivi mpaka leo hujui mchango wa Lisu katika midani za siasa Tanzania. Hakika wewe ni mburula?
 
I wonder ndio maana nchi yetu ni masikini kuanzia baba wa taifa mwenyewe na wewe binafsi kua na thinking wrong kiasi hiki...

Wewe,unaweza isaidia Tanzania kitu gani meaningful maana huna madaraka,huna hela,huna lolote ni mwananchi wa kawaida?

Mtu yeyote asie na madaraka yeyote,au pesa yeyote,au any position of mass change,then unaweza isaidia hii nchi kwa hali kubwa kwa baadhi ya kufanya haya:

1.Fanya kazi kwa bidii kazini kwako au biashara yako
2.Tunza familia yako kwa bidii
3.Usimuonee au kufanya crime kwa wananchi wenzako
4.Lipa kodi yako halali
5.Shiriki kwenye process za demokrasia kama kupiga kura,kuchagua au kuchaguliwa,etc

Jingine lipi unataka?

Kuisaidia Tanzania??????Kivipi yaani?

Kupika uji na kugawa barabarani?

Usikute unachanganya vitu viwili hapa,"charity" na "kusaidia nchi" which means kama ni kusaidia kama hivyo huna jeuri ya kusaidia nchi kipesa au kimaamuzi maana hakuna mwenye madaraka to effect that change needed....

Sijui unataka nini hasa?

Maana serikali ya Tanzania ni organization yenye madaraka kwa wananchi wa Tanzania above God,wanafanya lolote watakalo,wanakusanya hela watakayo,mwananchi ni powerless tiny being compared to the government,kuisaidia labda ufanye kazi bidii na kulipa kodi zako kihalali basi....

Charity ni mambo binafsi ya mtu
 
Umeshawahi kujiuliza wakati lisu akiwa mwanaharakati pesa alikuwa anazitoa wapi.muulize zito alichofanyiwa figisu na lisu.
 
Unachanganya mambo sana ndugu. Hatuongelei kufanya kazi wala masaa ya kazi. Haki ni kitu kinachoendana na wajibu.
Haki za watu kuvunjwa na kukiukwa ndio hoja mezani.
 
Je alipowatetea wazungu kwenye makinikia ilikuwaje tena
Hakuwatetea mabeberu, alikuwa anatoa tahadhari kwa serikali, kwamba, badala ya kutumia ubabe kwenye mikataba ambayo ni HALALI, ni vema ikatumia njia ya majadiliano. Kutumia NGUVU badala ya MIJADALA ni upungufu wa busara kwa upande wa serikali. Kumbuka kwamba ni huyuhuyu mwamba tunayemsifu ndio alituingiza hasara ya kulipa meli ya samaki ambayo aliikamata kinyume na utaratibu. Ili kuyaepuka hayo ndio hapo Tundu Lissu alikuwa anatoa tahadhari. Mwisho wa siku tumeruhusu mabeberu waondoe makinikia yao na zile Noah tulizoahidiwa hatujapewa 🤣 🤣 🤣
 
Kwani Jiwe kaisaidia nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…