Uchaguzi 2020 Tundu Lissu amepewa uhuru uliopitiliza

Halafu Utasikia Wanasena Hakuna Haki ya Kuongea au kujilekeza Wakati wamekuwa huru mpka wanataka kumshika Simba Sharubu UNAFKI UNATAWALA SANA KWA HIKI CHAMA CHA MBOWE
 
Humu naona kuna baadhi ya watu wanachukia kwa sababu wako huru! Ukiona hivyo ujue tu hujiwezi unataka kuendeshwa
 
Anapowatukana marais kuwa ni wezi asidhani watu wataendelea kumuangalia tu
Mtu akikuambia wewe ni mwizi amekutukana? Bila shaka utadai athibitishe labda ikiwemo mahakamani.

Tunachojua marais wanakingwa wasishtakiwe, Je wanakingwa hata kutuhumiwa?
 
Kumbe serikali inakaa mahali hivi inaanza kugawa uhuru kwa kila raia kama token?

Wewe dada nimekuja kukuona una matatizo ya thinking....

Uhuru ni commodity ambayo serikali inagawa kwa tokenization process kwa jinsi mtu serikalini anavyojisikia?

Sio sheria na katiba yetu ndio ina garantii uhuru wa wananchi wake kama grupu na mmoja mmoja?

Ulisoma Civics chooni?
 
Nilitegemea ungeandika hayo matusi matokeo yake umeleta simulizi tu hapa

Lissu sasa hivi yupo above "snake line"ukisoma ambacho tai huwa anawafanya nyoka ndio utaelewa.

Yaani ukimfikisha adui yako level ambapo hana tena mbinu ya kukushambulia kinachofuata hapo ni Kifo chake tu.

Ndicho Lissu alichawafanya CCM.
 
Pole sana ndg yangu, ukandamizaji wa waTZ unaouringia na kuung'ang'ania ndio umeondoka.
Siku utakapo kuja tambua kuwa ulikuwa umeathirika kwa kushangilia, badala ya kuukemea uminywaji wa uhuru na haki za wananchi utakuja kumshukuru sio shujaa Lissu tu bali na hata waliokuwa wamesimama nae katika kipindi cha GIZA.
Tunakuombea kwa Mungu ili upate nguvu za kumkataa shetani aliekufikisha huko na kutubu kwa kweli, ili uweze kusamehewa na kuwa mtu mpya anaethamini utu, uhuru, haki na maendeleo ya kweli kwa watu. AMEN.
 
Uhuru ni haki ya kila mtanzania. Hakuna baya ambalo Lisu kafanya. Mbona nyie mnamuita katumwa na Mabeberu kuja kuuza nchi. Tulieni mvua za mawe zije kwenu
 
Sipati picha hali ingekuaje kama nchi hii wagombea wange pitia mdahalo kabla ya uchaguzi.

Wakati wa kampeni wagombea hawaulizwi maswali. Ndio maana kuna wanao dai wenzao hawana sera nzuri.

Hebu tuendane na nyakati
Hizi si nyakati za vifichovificho.
 
Weka tusi alilotukana lissu
 



Naomba utoorozeshee hayo matusi anayotukana Tundu Lissu. Husipofanya hivyo tutajua tu kwamba mmezidiwa hoja hivyo mnatafuta huruma kutoka vyombo vya ulinzi na usalama,NEC na Msajili.
 

Ametoa tusi gani kwa Rais kwa mfano.?
 
Ameshawahi kukanusha kwamba yeye siyo kibaraka wa mabeberu? Aende mahakamani kama anasingiziwa.
Basi na huyo unaesema katukanwa nendeni mahakamani acheni kuwa na mawazo ya 60s huku. Magufuli mnamuona kama mungu kila siku kujipendekeza kwake. Sasa kiboko yake kapatikana na kamwe endapo atashinda hatoweza kuwaburuza tena watanzania.
 
kwani ana madhara gani hata akiendelea kubwabwaja?...
unajichosha na taarabu za kwenye vigodoro?
 
Nani asiyejua huyo mgombea wenu alivyo na mdomo mchafu?

Taja hayo matusi ili tujiridhishe ni kweli au ni hoja zake mnazoshindwa kuzijibu kwa mnataka vyombo vya ulinzi na usalama,NEC na Msajili wawasaidie.

Kikwete aliwaambie msitegemee hivyo vitu mtakuja anguka. Lissu sasa hivi anawaambie polisi hamjaongezewa mshahara miaka mitano, kuna kikokotoo kipya kipo pending kupisha uchaguzi,kinarudi 2021. Wakiwaamrisha mtupige mabomu msikubali maana mtamsaidie mtu ambae hajali maslahi yenu wala ya ndugu zenu. Ujumbe huo huo ameeafikishia watumishi wengine wa umma. Au haya ndiyo unayoyaita matusi?

Magufuli alikuwa anatuswaga kama hakutokuwa na uchaguzi,sasa hivi anajifanya kukenua meno na kurukaruka mziki wa akina Zuchu,hatudanganyiki tunajua jiwe hawezi kubadilika na tutamkataa ili aibe kura aongoze kwa mabavu bila ridhaa yetu wananchi.

Yaani kila sehemu unayogusa moto wa maisha magumu umewaka kuanzia utumishi wa umma mpaka sekta binafsi,tena husijaribu kujiajiri utakoma,kwenye kilimo moto mazoao ya biashara yote yameporoka bei,kuanzia korosho,ufuta,mbaazi,pamba,tumbaku,katani mpaka kahawa.
 
Lissu hapo alipo ukimgusa anamwekua MWEKUA..........

Mguseni msikie paah.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…