Tundu Lissu anastahili kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA lakini siyo Rais wa Tanzania

Unahangaika Sana Jo..sometimes sio lazima uandike unajidhalilisha
 


Sijajua kwanini mods waliufungia huu uzi. Asante kwa wazo lako
 
Lissu sio mbaya lakini kwa urais bado na hatapata. Mimi nashauri ateuliwe ubalozi hapo Rwanda au Burundi. Sio mbaya pia Kama atatuwakilisha hapo Congo DR au Sudani kusini ikishindikana Uganda hapo.

H.E Tundu Antipas Lissu
 

Umesema vyema saana,Ila hata kua mwenyekiti wa CDM naona bado anachangamoto ya kua na Skills za ku manage hasira na namna ya kujiexpress bila jazba kama kiongozi Mkuu wa chama.
Naona anafaa zaidi ile nafasi ya Tanzania Law Society(TLS) ana skills za sheria na kujenga Hoja ila kwenye Maswala ya siasa simuoni akifanya vizuri kwani Majukwaa yanawatu wake wenye Public speaking skils,Hana maneno ya kuomba kura kwa watanzania cha zaidi naona kageuka kua Mlalamikaji na sio Mgombea wa kunadi sera za Chama chake.
Nashauri ajikite kwenye profession yake ya Sheria.
 
Kwa nini urais hatoshi?
Rais anatakiwa awe na sifa zipi?
 
Na hii nayo unaiita thread? Halafu Moderator huwa anakupendelea sana! Mauchafua yako mengi huwa wanayaacha! Sijui ili wasionekane wanapendelea upinzani? Mmezoea kubebwa hamna hoja stupid.
 

Hao waliotosha wametuletea nini kwa miaka zaidi ya 50! uchumi mdogo kuliko hata Kenya. Tanzania inahitaji fikra tofauti
 
Lissu sio mbaya lakini kwa urais bado na hatapata. Mimi nashauri ateuliwe ubalozi hapo Rwanda au Burundi. Sio mbaya pia Kama atatuwakilisha hapo Congo DR au Sudani kusini ikishindikana Uganda hapo.

H.E Tundu Antipas Lissu
Endelea kuigeuza siasa kuwa ya kisayansi muda muafaka tutaelewana.
 
Nashindwa kukuelewa ndugu yangu.
Kwa kuwa umeshindwa kueleza kilichopungua kwa mgombea wa Chadema katika nafasi yake ya kusaka urais, hivyo ukaona anafaa kuwa mwenyekiti wakati zote ni taasisi zinazoongozwa na katiba, sheria na taratibu zingine, kama unaona anafaa kuwa mwenyekiti basi na kuwa rais pia anafaa.
Njoo na hoja itakayo mshawishi mtu kwanini asimpe mtu asimpigie mgombea fulani na achague mgombea wa chama fulani.
KUMBUKA; Wagombea wote waliopitishwa na tume wananafasi sawa za kuwa rais iwapo tu watawashashiwi watanzania kuwapigia kura na wakafanya hivyo.
 
Sasa kama mlichagua Mbuzi kutoka Burundi awe Rais na akawa sembuse msomi Mahiri Tundu Lissu?
 
Bwashee naamin kama bwana yule ameweza hata mie naweza kwa Lissu mbali sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…