Lusungo
JF-Expert Member
- Jan 4, 2014
- 28,259
- 41,416
Nimeshangazwa na namna Tundu Lisu anavyopewa umaarufu wa bure bila sababu za msingi. Wakati Lisu akitumia vyombo vikubwa vya habari duniani kuinanga serikali na bunge lake, bunge linatumia TBC kumjibu, tena wala hawatumii extenal service kama ipo.
Najiuliza tu kama msemaji wa bunge au serikali hawawezi kumpinga na kumshushua Tundu Lisu kwa kutumia media za kimataifa.
Ingependeza hata kumuona msemaji wa CCM ndugu Polepole kwenda pale BBC au CNN kuweka mambo sawa dunia ijue ukweli.
Lakini yupo mwanaccm nguli ambaye ana uzoefu kidogo na hizo International media ndugu yetu Pascal Mayalla, katika hili nadhani angeweza kusaidia.
Cha msingi Tundu Lisu ni lazima ajibiwe kwa njia ile ile anayoipitia kushambulia na siyo hadi tumsubiri Salary slip atuletee mashambulizi hayo kwa tafsir ya kiswahilii ndio tukurupuke kumjibu.........Ndio sababu tunanukuliwa vibaya.
Niwatakie Ijumaa njema
Maendeleo hayana vyama!
Mna kichwa gani huko CCM cha kuweza jibu au shiriki vipindi kama hard talk? Nyote ni makasuku mnaoropoka vya kumezeshwa!! Kama mkuu wenu wa Jela anatamka intapretenyuaa atweza lingua ya huko Mbele? No wonder ni mtupu sana kichwani kiasi cha kujiita kichaa
Sent using Jamii Forums mobile app