Tundu Lissu asusia mkutano Dar

Tundu Lissu asusia mkutano Dar

nngu007

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2010
Posts
15,860
Reaction score
5,801
Saturday, 09 April 2011

MJUMBE wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, Tundu Lisu, jana alitoka ndani ya ukumbi wa mkutano kuhusu mjadala wa maoni wa muswada wa sheria ya mapitio ya katiba, kwa madai kuwa kulikuwa na kundi la watu waliokodiwa kuvuruga mchakato huo.

Lisu alitoa kauli hiyo muda mfupi baada ya kutoka nje ya kumbi wa mikutano wa Karimjee, kufuatia kuwapo kwa kundi la watu waliokuwa wakuzomea wachangiaji wa mjadala.

Akiwa nje ya ukumbi huo, aliwaambia waandishi wa habari kuwa, kundi hilo lilikodiwa na CCM kwa lengo la kuvuruga mchakato huo, ili usifanikiwe.


Tundi pia aliwatupia lawama polisi katika Kanda Maalamu ya Dar es Salaam, kuwa wamekuwa katika katika eneo hilo, kwa lengo la kulinda kikundi hicho kilichokuwa kinafanya kazi ya kuzomea wachangiaji, waliokuwa wakikosoa muswada.

"Jana (juzi)tulikubaliana kwenye kikao cha kamati kuwa ulinzi katika mkutano wa leo (jana) ungeimarishwa na mtu yeyote atakayebainika kuwa anazomea au kuzuia maoni ya watu wengine kutolewa, polisi wangemtoa nje ya ukumbi, lakini kinchofanyika leo ni tofauti kwa sababu polisi wanawalinda wanaofanya vurugu," alisema.

Lisu pia alipinga muswada huo kwa maelezo kuwa una mapungufu mengi na kwamba hakuna

sababu ya kuupeleka bungeni kujadiliwa, kwa utumia hati ya dhararu.

Kwa mujibu wa Lisu, muswada huo ulipaswa kufuata njia ya kawaida ya kutunga sheria na si kwa hati ya dharura.


Alisema haiwezekani kwa muswada ambao ni mali ya wananchi na roho ya taifa, kujadiliwa ndani ya siku tatu na kupitishwa.

Alisema sababu nyingine ya kupinga muswada huo, ni vipengele vilivyopo ndani yake ambavyo alisema kwa maoni yake, vinakandamamiza uhuru wa watu kushiriki katika kutunga katiba.

Alisema kwa hali ilivyo, mjadala huo ulioandaliwa kwa siku chache hautakuwa na manufaa kwa wananchi na kwamba badala yake, utatengeneza manung'uniko kwa wananchi.


Alipoulizwa kuhusu hatua ya Lisu kutoka nje ya ukumbi, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Pindi Chana, alisema hawezi kulizungumzia hadi kwanza apate sababu zilizomfanya kufikia uamuzi huo.

"Mimi muda huu siwezi kuzungumza chochote mpaka niwe na ushahidi wa kile kilichomfanya atoke ndani ya ukumbi wa mikutano,"alisema Chana.


Katika mjadala huo wadau mbalimbali waliochangia walipinga baadhi ya vipengele vya muswada kwa maelezo kuwa vinavunja katiba ya sasa ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Kazi ipo na makamba anajidanganya kwamba anaweza kupambana na chadema kamuagiza mwenyekiti wa uvccm kuandaa mpango wa kupambana na chadema kila kona na eti wameomba usalama wa taifa kuhakikisha wanawajulisha mbinu zote za chadema kabla hazijatekelezwa. Jamani tuwe tayari kwa mapambano wabunge wetu tuko tayari tunawasubiri.
 
Mbona wa CCM na UDP walizomewa Chuo Kikuu, hakuna aliyesusa? Hawa Chadema wamezowewa kidogo tu wanajidai kususa. Wazomee wao tu, wakizomewa wanasusa. wakishindwa kura wanasusa, wakoje hawa?
 
Mbona wa CCM na UDP walizomewa Chuo Kikuu, hakuna aliyesusa? Hawa Chadema wamezowewa kidogo tu wanajidai kususa. Wazomee wao tu, wakizomewa wanasusa. wakishindwa kura wanasusa, wakoje hawa?

1.jpg


Hao watoto walibana nafasi watu wenye mawazo pevu wasiingie kujadili katiba.
 
huu utani sasa, kuweka watoto karimjee, kwa nini wasingewafuata huko mashuleni, Mi nadhani tungepunguza utani kwenye mambo ya msingi kama hili la Katiba.
 
1.jpg



Hao watoto walibana nafasi watu wenye mawazo pevu wasiingie kujadili katiba.​

Jana Mboe Mwnyekiti wake kasema kama kushangilia sio kosa iweje kuzomea iwe kosa? au Tindu hajamsikia Bosi wake? ishu ya watoto haipo as wote inaonekana ni above 18 years, mbona kwenye maandamano wanakusanywa? kama issue ni kulala wameiga viongozi wao pale bungeni kila siku wanauchapa, hata Ngeleja keshauchapa mkutanoni mbele ya JK kule paris.
 
mbona wa ccm na udp walizomewa chuo kikuu, hakuna aliyesusa? Hawa chadema wamezowewa kidogo tu wanajidai kususa. Wazomee wao tu, wakizomewa wanasusa. Wakishindwa kura wanasusa, wakoje hawa?
napenda zomea zomea iendelee kwa wote maana inaonesha ni namna gani watanzania tunaweza kujadili!!! Inaonesha namna gani tunaweza na kumudu majadiliano!!! Inaonesha ni upeo kiasi gani tulio nao, hakuna haja ya kukemea zomeazomea!! Nadhani ni aina ya watanzania kujadili mambo!!! Zomeazomea ni burudani tosha na ni funzo pia kwa wanaopenda zomeazomea!!

Zomeaneni siku zipite tupate katiba mpya itakayokuwa 'nzuri' kwa sababu zomeazomea itakuwemo!

Wanasiasa wa nchi hii si makini, na ndilo linapelekea na wananchi kuwa kama wao. Hapo usisahau na serikali yenyewe!!!
Woote ni kama pipa na mfuniko wake!!
 
Jana Mboe Mwnyekiti wake kasema kama kushangilia sio kosa iweje kuzomea iwe kosa? au Tindu hajamsikia Bosi wake? ishu ya watoto haipo as wote inaonekana ni above 18 years, mbona kwenye maandamano wanakusanywa? kama issue ni kulala wameiga viongozi wao pale bungeni kila siku wanauchapa, hata Ngeleja keshauchapa mkutanoni mbele ya JK kule paris.

Haa haaaaa! Uliwauliza juu ya umri wao ndugu? Ukitaka kujua kama Serikali iko serious na utoaji maoni ulio huru katika Muswada huu soma kifungu cha 28 (2) na (3) cha Muswada: "28 (2) For the purposes of subsection (c) paragraph (1) the referendum campaign shall be conducted by the Commission and no political party or affiliate organization to a political party shall participate in a referendum campaign.
(3) A person who contravenes the provisions of subsection (2) commits an offence and on conviction be liable to imprisonment, without fine, to a term not exceeding two years."


Kifungu hiki kina jambo la ajabu sana: Kwamba eti Tume iliyokusanya maoni ndio ifanye Kampeni yenyewe, sasa hapo unategemea nini? Si watafanya kampeni kuvutia kile wanachoamini? Na endapo mtu mwingine anafanya kampeni eti linakuwa kosa la jinai! Sasa hapa ukiambiwa kuwa CCM/Serikali imepeleka watoto ili kukaba nafasi za watu wenye uchungu na uelewa wa mambo ya nchi yao utashangaa?
 
1.jpg

Hao watoto walibana nafasi watu wenye mawazo pevu wasiingie kujadili katiba.
Hii katiba inawahusu zaidi hao watoto, na ni uongo waliosema wamekodishwa hao walipelekwa masomo kwa vitendo, ni kawaida kabisa, hata bungeni huwa tunaona wakipelekwa! Msitafute sababu zisizo na maana.

Jee, mnataka kusema kuwa watoto hawana haki nchi hii?
 
Hii katiba inawahusu zaidi hao watoto, na ni uongo waliosema wamekodishwa hao walipelekwa masomo kwa vitendo, ni kawaida kabisa, hata bungeni huwa tunaona wakipelekwa! Msitafute sababu zisizo na maana.

Jee, mnataka kusema kuwa watoto hawana haki nchi hii?

Hawa watoto waliokodishwa kwenda kula usingizi kwenye ukumbi wa Karimjee au unazungumzia watoto wepi ndugu?
 
Majimshindo wewe ni mpumbavu wa mwisho hivi unaweza kutetea upuuzi huu,hawa wahuni(watoto) unaweza kweli kusema kwamba ni wanafunzi ambao wapo kwenye masomo ya vitendo? Wachafu,wamevaa shabeshabe halafu unataka kusema nini?!!
Jaribuni(CCM) kutumumia ubongo kufikiri badala ya unyayo
 
Hawa watoto waliokodishwa kwenda kula usingizi kwenye ukumbi wa Karimjee au unazungumzia watoto wepi ndugu?

Watoto wanahaki sawa kama babu, kwanza wanasoma civics kwa vitendo kama ni swala la kukodisha ccm walimkodi Tambwe , chadema nao walikodi Slaa kuwakilisha mawazo ya chama.

Tatizo linakuwa palepale, wenye makosa ni wale walioanzisha kuzomea wenzao, binadamu inabidi kuheshimu mawazo ya mwezako hata kama wewe unayona ni ya kipuuzi. Na unapoona hivyo na mwezako pia anayoana mawazo yako ni ya kipuuzi. kwa hiyo mkubaliane kuzomeana. Haiwezekani wewe uzomee tuuuu harafu kinyume chake kisiwe sahihi.

Mimi nawashangaa hawa viongozi, wanashindwa kuelewa tu ya kwamba mnapotofautiana kimawazo kila upande kwa mawazo yao huona wako sahihi kwa asilimia 100% na kila upande huona upande mwingine ni wenye mawazo ya kipuuzi. Hivyo basi, muungwana hunyamaza na kuondoka, lakini uki opt kuzomea eti kwa sababu mawazo yake umeyaona ni ya kipuuzi ndivyo hivyo naye atazomea maana atakua anaamini kabisa nawe ni u mpuuzi.
 
why masomo kwa vitendo, then wanakaba nafasi za sensitive contributors? Kama ndivyo, si wangepewa viti vyao tofauti na hivyo ili wakae kama listeners wakiwa pembeni?
 
Mbona wa CCM na UDP walizomewa Chuo Kikuu, hakuna aliyesusa? Hawa Chadema wamezowewa kidogo tu wanajidai kususa. Wazomee wao tu, wakizomewa wanasusa. wakishindwa kura wanasusa, wakoje hawa?

chadema ni chama makini. Mtu yeyote ambae hafikiri kwa maslahi binafsi atakubaliana na mimi. Chadema hakiwezi kuzomea kwenye mikutano it is way above that
 
Kilichofanyika jana ni upumbavu na aibu kubwa kwa taifa, ni ujinga tu.
 
chadema ni chama makini. Mtu yeyote ambae hafikiri kwa maslahi binafsi atakubaliana na mimi. Chadema hakiwezi kuzomea kwenye mikutano it is way above that

Mbona Lissu hakutoka nje wakati Tabwe anazomewa mpaka wakahairisha mkutano, tuwe wauungwana kwa kuheshimiana kwanza.
 
Hii katiba inawahusu zaidi hao watoto, na ni uongo waliosema wamekodishwa hao walipelekwa masomo kwa vitendo, ni kawaida kabisa, hata bungeni huwa tunaona wakipelekwa! Msitafute sababu zisizo na maana.

Jee, mnataka kusema kuwa watoto hawana haki nchi hii?

CCM mnapesa za kuchezea mngewekeza kwenye elimu, afya, michezo tungekuwa mbali sana.

Ukiwauliza hao watoto mjadala ulikuwaje nn kilizungumzwa hawatakuambia kitu maana wamepiga mbonji wengi wanadai waliamshwa saa 11 usiku kuwahi kubana nafasi ukumbini.
 
Hata kama watoto wana haki sawa lakini kuna maamuzi mengine lazima yafanywe na watu wazima au wazazi wao kwa manufaa yao. Lissu was right to walk out huwezi kujadili mambo ya msingi na watoto tena waliolala kwa kisingizio cha haki sawa.

Hizi mbinu wanazofanya CCM zilifanywa na nchi mbalimbali lakini hazikufanikiwa matokeo yake waliokuwa wanazuia waliishia jela(Kenya).

1.jpg
 
Jana Mboe Mwnyekiti wake kasema kama kushangilia sio kosa iweje kuzomea iwe kosa? au Tindu hajamsikia Bosi wake? ishu ya watoto haipo as wote inaonekana ni above 18 years, mbona kwenye maandamano wanakusanywa? kama issue ni kulala wameiga viongozi wao pale bungeni kila siku wanauchapa, hata Ngeleja keshauchapa mkutanoni mbele ya JK kule paris.

wewe ni mtu wa ajabu sana...kukaa kimya pia ni hekima............jana palikuwa na watot wa kuanzia miaka 11 hadi 17........kama huna uwezo wa kuweka hoja zenye mashiko au unachangia kwa ushabiki basi wewe hufai na hujui nini unakizungumza
 
Back
Top Bottom