Pre GE2025 Tundu Lissu awataja viongozi wa CHADEMA ambao hawajatubu kwa Mbowe na anawashughulikia ndani ya Chama

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Tundu Lissu amewataja baadhi ya viongozi na Wanachama wa CHADEMA ambao hawajatubu kwa Mwenyekiti wa Chama, Freeman Mbowe na anawashughulikia ipasavyo ndani ya Chama.

"Tukikutana hivi kwenye vikao hatupigani ngumi, hatuko kama tulivyokuwa mwanzoni. Mwenyekiti aliyekwenda gerezani, sio Mwenyekiti aliyetoka gerezani na huyo sio mimi peke yangu ninayesema hivyo, mimi sasa ni mhaini wa sasa, kulikuwa na mhaini anaitwa Peter Msigwa, kulikuwa na mhaini anaitwa John Heche, kulikuwa na mhaini anaitwa Godbless Lema, kulikuwa na mhaini anaitwa Gaston Garubindi, kulikuwa na mhaini anaitwa Ezekia Wenje kabla hajaenda kufanya Sala ya kitubio na kutubu dhambi zake kwa Baba yetu.....akisema nimekosa mimi, nimekosa sana ndio dhambi zake zikafutwa hao wengine niliowataja hawajatubu na wamekuwa wakishughulikiwa kweli kweli"
Your browser is not able to display this video.
Soma, Pia: Mbowe amvaa Dkt. Slaa kisa Tundu Lissu, adai "mpiga debe wa CCM hapaswi kutufundisha CHADEMA"
 
Mh huu mtifuano unatukumbusha ile methali
Vita vya panzi furaha kwa kunguru
Watu wa kijani naona meno yote nje kwa kicheko
 
Aliesema siasa haina rafiki wa kudumu wala adui wa kudumu alikuwa sawa kabsa.
 
Lissu hafai CDM atoke!
 
Healthy opposition.
 
mboe ni likuwadi la ccm lililoweka Hela mbele
 
Wakati wa dhoruba baharia wenu Lisu alikimbilia Kwa waliomtuma.Baada ya Mbowe kupambana na kutuliza chombo eti hafai Bali anafaa aliyekimbia Nchi πŸ˜†πŸ˜†

Upuuzi huu unaweza fanya na wajinga wa Chadema
 
Mlikosea nini huyo "baba yenu"? Kuwa muwazi au Wenje ajitokeze aseme alienda kuttubu kosa gani ? Tunataka watu making kuongoza nchi sio blah blah.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…