Tundu Lissu hafai kuwa kiongozi kwasababu anatoa hadharani madhaifu ya Chama chake

Hiyo uliyotoa siyo hoja! Tangu lini "udhaifu" au "madhaifu" yakawa ndiyo "siri" za chama? Siri za chama ni mbinu au mikakati chama kilichonayo kwa ajili ya ushindani wa kisiasa, na ambayo inasubiri muda muafaka ndipo iwe hadharani. Sasa hii ndiyo ikianikwa kabla, kinyume na utaratibu wa chama, huko ndiko kuvunisha ziri za chama. Hakuna chama madhubuti kinachojivunia maovu au tuhuma za rushwa au ubadhilifu wa fedha kama siri zake. Hata katika familia maovu kama kuchepuka (kuvunja uaminifu wa ndoa), kumnyanyasa mke/mume/mtoto hakuwezi kuwa siri ya familia. Siri ya familia ni mipango mizuri ambayo familia inayo kwa ajili ya kujiletea maendeleo, ambayo kama itatolewa kwa watu wengine kabla ya muda wake, familia inaweza kuhujumiwa katika mipango yake. Hii ndiyo inaweza kuwa siri ya familia.
 
Kumuattack Mwenyekiti hadharani ni jambo baya sana linavipa Vyama pinzani ticketing ya kuwa hawafai na mbaya zaidi kwa kukiri hadharani
 
Kumuattack Mwenyekiti hadharani ni jambo baya sana linavipa Vyama pinzani ticketing ya kuwa hawafai na mbaya zaidi kwa kukiri hadharani
Hajamu'attack' mtu, bali ni tafsiri ya watu kwamba alikuwa akimshambulia mwenyekiti wake. Na watu leo wanasema hivi, kesho vile, na si lazima wanachosema ndio ukweli. Angemtaja kwa jina labda, au kwa namna ambayo inaonyesha wazi hivyo. Hapo ndipo ungesema, na pia ingetegemea na tuhuma zenyewe. Kama ni za kweli, si sawa na kusema, ila kama si za kweli, hapo ndipo angekuwa yuko offside. Yaani.mtu akituhumiwa jambo ambalo ni la kweli, hakuna kosa. Akituhumiwa jambo ambalo si kweli, kuna kosa.
 
Cc.Mwl Nyerere
 
Badilikeni mbona kama tunawapa faida upande wa pili watatucheka sana hawa.
Mabadiliko muhimu, Wanachama wa Chadema wameanza kupotoka badala ya kuendesha gari wameanza kugombana na dereva wao
 
UWT tulieni
 
lissu hanaga kona kona, kama ni nyeupe tu atakuambia sio kubembeleza! kumwambia mtu kama anakosea Kwa kumbembeleza huo ni uchawa πŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒ
 
Hata Nyerere aliwahi anika msdhaifu ya CCM, hivyo hivyo kwa JK n.k
Madhaifu yanayoonekana sio siri, ndio ukomavu. Tofautisha Kati ya madhaifu na mikakati.
Na angesems tu nitagombea, wenye akili wangemshsngaa.
Mtu ansyejikosoa hadharani huyo amekua.
 
Ameona kuna mapungufu, ndyo maana ameamua kugombea yeye uwenyekiti. Na mapungufu hayo ni lazima ayaseme. Ndyo njia pekee ya kupata kura. You are looking into it in a wrong direction!!
 
Ameona kuna mapungufu, ndyo maana ameamua kugombea yeye uwenyekiti. Na mapungufu hayo ni lazima ayaseme. Ndyo njia pekee ya kupata kura. You are looking into it in a wrong direction!!
Chama chako ukikisema hadharani inatengeneza mtafaruko
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…