Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bara, Tundu Lissu, akizungumza na wanahabari siku ya Alhamisi Desemba 12, 2024, Mlimani City, Dar es Salaam, ameeleza azma yake ya kugombea uenyekiti wa CHADEMA Taifa.
"Haikuwa rahisi kwangu kufikia uamuzi wa kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa chama chetu. Tangu mwaka 2015 vishawishi vya kunitaka kugombea nafasi hiyo vilipoanza hadi miezi michache iliyopita, nimesema mara kwa mara, hadharani na faraghani, kwamba siko tayari kugombea nafasi hiyo.
Ili kuondoa mashaka yoyote juu ya msimamo wangu huo, tarehe 6 Agosti ya mwaka huu niliwasilisha rasmi kusudio langu la kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti ambayo nimeitumikia tangu Uchaguzi Mkuu wa chama uliopita wa mwaka 2019.
Kwa vyovyote vile, kubadili msimamo wangu unaojulikana wazi na kwa muda mrefu kunadai majibu ya swali la kwa nini? Swali hili ni halali na halina budi kujibiwa kwa ukweli na kwa ufasaha. Nitajaribu kufanya hivyo kwa kadri ya uwezo wangu," alisema Lissu.
Pia, Soma: Tundu Lissu: Nimewasilisha kusudio la kugombea nafasi ya Mwenyekiti CHADEMA
"Haikuwa rahisi kwangu kufikia uamuzi wa kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa chama chetu. Tangu mwaka 2015 vishawishi vya kunitaka kugombea nafasi hiyo vilipoanza hadi miezi michache iliyopita, nimesema mara kwa mara, hadharani na faraghani, kwamba siko tayari kugombea nafasi hiyo.
Ili kuondoa mashaka yoyote juu ya msimamo wangu huo, tarehe 6 Agosti ya mwaka huu niliwasilisha rasmi kusudio langu la kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti ambayo nimeitumikia tangu Uchaguzi Mkuu wa chama uliopita wa mwaka 2019.
Kwa vyovyote vile, kubadili msimamo wangu unaojulikana wazi na kwa muda mrefu kunadai majibu ya swali la kwa nini? Swali hili ni halali na halina budi kujibiwa kwa ukweli na kwa ufasaha. Nitajaribu kufanya hivyo kwa kadri ya uwezo wangu," alisema Lissu.