Uchaguzi 2020 Tundu Lissu, ilani yako na CHADEMA itahitaji msaada zaidi ya asilimia 90, tutarudi utumwani

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu, ilani yako na CHADEMA itahitaji msaada zaidi ya asilimia 90, tutarudi utumwani

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2016
Posts
17,506
Reaction score
16,003
Ndugu zangu,

Nimepata fursa ya kumsikiliza Tundu Lissu akitangaza ilani ya Chadema nikiri kwa kusema kuwa ili kutekeleza "wish list" yake inahitaji kufadhiliwa na fedha za nje kwa asilimia zaidi ya 90 na uenda akashindwa kulipa hata mishahara ya watumishi wa umma.

Tundu Lissu anasema ataondoa kodi na nyingine atazipunguza ili kuchochea biashara na uwekezaji. Ukitaka kujua kuna utapeli hasemi ataondoa kodi zipi?na atapumguza zipi na kwa asilimia ngapi?

Tundu Lissu ameendelea kuhadaa umma kuwa atalipa fidia watu waliobomolewa kupisha ujenzi.Hapa atatumia sheria ipi kulipa fidia mtu zaidi ya mmoja zaidi ya mara moja kwa eneo lile lile?Je atakuwa tayari kufanya double standard hiyo nchi nzima?ukiacha waliobomolewa kupisha barabara,kuna waliobomolewa kwa kujenga eneo la reli,eneo la miundombinu ya maji na kadhalika atakuwa tayari kufanya hivi nchi nzima?Watu waliolipwa fidia miaka ya 70 na 80 kupisha ujenzi wa miondo mbinu wakawauzia wengine je hapo serikali italipa fidia kwa sheria ipi?Huu ni utapeli.

Mfuko wa bodi ya mikopo ya elimu ya juu (HELSB) kama tujuavyo hii ni "relvolving fund" ili wengine wanufaike lazima walionufaika kabla walipe la sivyo mfuko utakufa.Tundu Lissu anaongopea watu kuwa inawezekana watu kulipa kiduchu kiduchu,hii haiwezekani,bodi itashindwa kujiendesha na matokeo yake sababu ya makudanyo hafifu ya marejesho wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu watakuwa wachache.Hili halikubaliki.

Kwa kifupi,ilani hii ya Chadema na Tundu haina uhalisia labda kama nchi itageuzwa "NGO" ya akina Robert Amsterdam"

Nimalize kwa kusema hakuna nchi inayoweza kuwa huru kama serikali yake haikusanyi kodi na wananchi wasipowajibika.

Tujadili kwa makini
 
Hizi ilani ni nyimbo tu kila msikilizaji akipenda kuisikia atakua anarudiarudia huo mziki bila kujali nyimbo zingine huleta kelele kwa walio karibu.. na wengine huenda hiyo nyimbo waisiiepende, na wakapenda ya kusikiliza nyimbo mwimbaji flani na kusahau kuwa ni kelele kwa wengine, kifupi kila mwenye kuipenda nyimbo aichague mwenywe.
 
Anasema atapunguza kodi ili iwe rahisi kwa watu wengi zaidi kuanzisha biashara na miradi ya ujasiriamali.

Mfumo wa sasa hivi umejikita ktk kukamua wafanyabiashara na wawekezaji kwa kodi kubwa, na hauchochei wananchi wengi zaidi kuanzisha biashara na kuwekeza.

Kwa msingi huo basi, kupunguza idadi ya kodi anakokuzungumzia kutaongeza idadi ya wawekezaji,wafanyabiashara, ajira, walipakodi, na hivyo kuongeza mapato / makusanyo ya serikali.

Kila aliyebomolewa makazi yake kupisha mradi wa miundombinu anapaswa kulipwa fidia stahiki. suala hili halipaswi kuwa na mjadala hata kidogo.

Tuna tatizo la "revolving fund" ya mikopo ya elimu ya juu ni kukosekana kwa uwezo wa kurudisha fedha za mikopo kwa wale wanaokopeshwa.

Vijana wetu wengi wanazagaa mitaani bila ajira baada ya kuhitimu masomo huku wakiwa na mzigo wa madeni. Hili ni jambo baya sana, tunajenga tabaka la watu wenye MADENI kabla hata hawajaingia ktk ajira ktk nchi yetu.

..Tunapaswa kutatua tatizo la UKOSEFU WA AJIRA kwa vijana wanaohitimu elimu ya juu, na kuwawezesha kuwa na vipato vya kulipa mikopo yao ili mfuko wa mikopo ya elimu ya juu uendelee kuwa salama.
 
Tuambie kwanza deni la taifa mpaka sasa figure imeshuka au imepanda zaidi, kama kwa miaka hii mitano limekua jiulize mara mbili na nadhani utaupata ukweli.

Kusema ukweli kama vilivyosemwa jana ndo vipaumbele vya ilani ya ccm tunasafiri kwa kasi downhill. Yaani uwanja wa mpira na ununuzi wa midege ina faida gani kwa sasa? Lakini pia issue ya bodi ya mikopo ni suala linaloumiza wengi hebu fikiria kijana aliyemaliza masomo 2015 hana ajira wala hakuna mazingira wezeshi ya yeye kujiajiri, mpaka leo na alikopehwa say mil 10,000,000 kila mwaka deni linaongezeka kwa 15% maana yake mpaka sasa ananadaiwa 17,500,000 kwa nini riba iwe kubwa hivyo? Huko kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii waajiriwa wa sekta binafsi wanakumbana na adha kubwa ya kupata mafao yao. Kama upo Dar fanya survey kidogo Ofisi yeyote ya NSSF utajionea shida na dhuluma wanayofanyiwa hao watu, ni mwendo wa kukatishwa tamaa tu na mbaya zaidi unakuta mtu hana kazi muda huo.
 
Huo utumwa "tuliutokamo" lini?

Kwa miaka 5 ya jiwe utumwa umeongezeka kwa kupoteza hata kale ka uhuru tulikokunako!, awamu hii hatitizami tukaona, hatuli tukashiba, hatulali tukasinzia,..sheria kandamizi zimekuwa nyingi mno, don't,.. don't,. Zimekuwa nyingi mno!
 
Kamanda hivi ukiweka kwenye orodha ya vikwazo vya biashara kodi ni namba moja?unataka kusema leo ukifuta kodi zote viwanda vitajaa?

Hivi unajua ni viwanda vingapi vimeshindwa kujengwa sababu ya ukosefu wa umeme wa uhakika?siku zote kodi hulipwa kwenye faida mtu anayopata na kwa Tanzania kwa makampuni yaliyoorodheshwa kwenye soko la hisa la Dar ni hutozwa asilimia 25 wakati yaliyoorodheshwa hulipa asilimia 30.

Kwenye kujenga msingi wa kufuta,kupunguza au kuongeza kodi lazima Chadema watuambie wakifuta fedha ngapi zitapungua au kuongezeka na mikakati ya kuziba pengo na si maneno ya jumla jumla la sivyo nchi itakuwa ya kimafia kwa kuendeshwa na watu wachache badala ya serikali.
..anasema atapunguza kodi ili iwe rahisi kwa watu wengi zaidi kuanzisha biashara na miradi ya ujasiriamali.

..mfumo wa sasa hivi umejikita ktk kukamua watu wachache kwa kodi na hauchochei wananchi wengi zaidi kuanzisha biashara.

..kwa msingi huo basi, kupunguza idadi ya kodi anakokuzungumzia kutaongeza idadi ya walipa kodi, kutaongeza ajira, na kutaongeza mapato / makusanyo ya serikali.

..kila aliyebomolewa makazi yake kupisha mradi wa miundombinu anapaswa kulipwa fidia stahiki. suala hili halipaswi kuwa na mjadala hata kidogo.

..Tuna tatizo la "revolving fund" ya mikopo ya elimu ya juu ni kukosekana kwa uwezo wa kurudisha fedha za mikopo kwa wale wanaokopeshwa. Wanafunzi wetu wengi wanazagaa mitaani bila ajira baada ya kuhitimu masomo huku wakiwa na mzigo wa madeni. Hili ni jambo baya sana, tunajenga tabaka la watu wenye MADENI ktk nchi yetu.

..Tunapaswa kutatua tatizo la UKOSEFU WA AJIRA kwa vijana wanaohitimu elimu ya juu, na kuwawezesha kuwa na vipato vya kulipa mikopo yao ili mfuko wa mikopo ya elimu ya juu uendelee kuwa salama.
 
Kuna kitu kinaitwa Debt/GDP ratio, kwa Tanzania bado deni la Taifa ni himilivu kwani ratio ipo chini ya asilimia 50.

Elewa,acha kupotoshwa bila maendeleo ya vitu (miundombinu) hakuna maendeleo ya watu
Tuambie kwanza deni la taifa mpaka sasa figure imeshuka au imepanda zaidi, kama kwa miaka hii mitano limekua jiulize mara mbili na nadhani utaupata ukweli. Kusema ukweli kama vilivyosemwa jana ndo vipaumbele vya ilani ya ccm tunasafiri kwa kasi downhill. Yaani uwanja wa mpira na ununuzi wa midege ina faida gani kwa sasa?

Lakini pia issue ya bodi ya mikopo ni suala linaloumiza wengi hebu fikiria kijana aliyemaliza masomo 2015 hana ajira wala hakuna mazingira wezeshi ya yeye kujiajiri, mpaka leo na alikopehwa say mil 10,000,000 kila mwaka deni linaongezeka kwa 15% maana yake mpaka sasa ananadaiwa 17,500,000 kwa nini riba iwe kubwa hivyo? Huko kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii waajiriwa wa sekta binafsi wanakumbana na adha kubwa ya kupata mafao yao. Kama upo Dar fanya survey kidogo Ofisi yeyote ya NSSF utajionea shida na dhuluma wanayofanyiwa hao watu, ni mwendo wa kukatishwa tamaa tu na mbaya zaidi unakuta mtu hana kazi muda huo.
 
Hela ya kujenga uwanja wa ndege Chato ingetosha kulipa wahanga wa bomoabomoa fidia.

Vile vile ukihusisha sekta binafsi katika ujenzi wa miundombinu unaweza kuoko fedha nyingi ukazielekeza katika maeneo mengine.

Kingine ni kufuta sitting allowance za wabunge na kuondoa mashangingi serikalini.

Serikali kuiokodisha ATCL au kuiendesha kwa ubia kutaokoa pia fedha nyingi zitatumika kuibeba ATCL.

Kufuta na kuondoa kabisa Bajeti ya kukimbiza mwenge na fedha hizi kuzielekeza katika maeneo mengine ya kipaumbele.

Vile vile ukiweka mazingira mzuri ya watu kufanya biashaara, utafanya watu wengi zaidi wafungue biashara na hivyo kupanua wigo wa kodi na matokeo yake ni kuongea makusanyo ya kodi.

Kwa kifupi,yote asemayo yanawezekana tukiachana na huu ujamaa uchwara na kupunguza matumizi makubwa na yasiyo ya lazima pamoja na kuwa na sera nzuri na rafiki za kikodi na watu kufanya biashara.

Na mwisho jiulize mmetumia fedha kiasi gani kugharamia chaguzi fake za kuunga mkono juhudi, fedha ambazo zingetosha kusomesha watoto wengi wa masikini katika vyuo vikuu vyetu.
 
Chapa kazi najua unapenda sana kutawaliwa na wazungu.Uhuru upi unataka?ndoa ya jinsia moja?kutembea uchi?
Huo utumwa "tuliutokamo" lini?
Kwa miaka 5 ya jiwe utumwa umeongezeka kwa kupoteza hata kale ka uhuru tulikokunako!, ...awamu hii hatitizami tukaona, hatuli tukashiba, hatulali tukasinzia,..sheria kandamizi zimekuwa nyingi mno, don't,.. don't,. Zimekuwa nyingi mno!.
 
Hakuna sheria inayoruhusu kulipa fidia eneo moja mara mbili.Hao waliobomolewa wengi waliuziwa na waliokwisha lipwa fidia
Hela ya kujenga uwanja wa ndege Chato ingetosha kulipa wahanga wa bomoabomoa fidia.
 
Usitufokee! Wewe endelea na aliyekuhifadhi ndo anakufaa. Hatutaki kuendelea na uchumi wa makaratasi huku pato la Taifa likiliwa na kikundi kidogo cha wanaCCM.
 
Kilipofikia chama pendwa kwa sasa!
Egmtp-WWoAE_XGt.jpg
 
Kamanda hivi ukiweka kwenye orodha ya vikwazo vya biashara kodi ni namba moja?unataka kusema leo ukifuta kodi zote viwanda vitajaa?

Hivi unajua ni viwanda vingapi vimeshindwa kujengwa sababu ya ukosefu wa umeme wa uhakika?siku zote kodi hulipwa kwenye faida mtu anayopata na kwa Tanzania kwa makampuni yaliyoorodheshwa kwenye soko la hisa la Dar ni hutozwa asilimia 25 wakati yaliyoorodheshwa hulipa asilimia 30.

Kwenye kujenga msingi wa kufuta,kupunguza au kuongeza kodi lazima Chadema watuambie wakifuta fedha ngapi zitapungua au kuongezeka na mikakati ya kuziba pengo na si maneno ya jumla jumla la sivyo nchi itakuwa ya kimafia kwa kuendeshwa na watu wachache badala ya serikali.

..Kodi ni moja ya vikwazo vinavyo-discourage ujenzi wa viwanda nchini.

..hivyo ni lazima tu-deal na tatizo hilo, na njia mojawapo ni kupunguza kodi hizo.

..nadhani hapa kuna kambi mbili za mitizamo kuhusu kodi. CCM wanaamini ktk kuongeza makusanyo kwa kutoza kodi kubwa. CDM wanaamini ktk kuongeza makusanyo kwa kuwa kodi ndogo na kuchochea watu wengi zaidi kuingia ktk biashara na uwekezaji.
 
Hela ya kujenga uwanja wa ndege Chato ingetosha kulipa wahanga wa bomoabomoa fidia.
Ingetoka wapi wakati hakusanyi kodi? kasema kodi atazifuta, hata za wafanyabiashara anazodai ziko 15 bila kuzitaja kasema atazifuta ili bidhaa kutoka nje zimwagike nchini bila kulipiwa ushuru, tunachagua afisa masoko wa mabeberu? katumwa na mabwana zake kuja kutafuta soko la bidhaa za viwanda vyao? Atatoa wapi pesa kuyafanya hayo anayoahidi? ATATUUZA HUYO.
 
Kuna kitu kinaitwa Debt/GDP ratio, kwa Tanzania bado deni la Taifa ni himilivu kwani ratio ipo chini ya asilimia 50.

Elewa,acha kupotoshwa bila maendeleo ya vitu (miundombinu) hakuna maendeleo ya watu
Wanachosahau au kujisahaulisha ni ukweli kuwa maendeleo ya vitu yanakwenda kurahisidha maendeleo ya watu.

Nchi kama Ujerumani imejaa miundo mbinu ya kisasa ya usafiri inayowezesha urahisi wa viwanda kuwa na ufanisi.
 
Back
Top Bottom