Pre GE2025 Tundu Lissu: Ili CHADEMA iaminike, ipendwe na kuthaminiwa tena na Wananchi ni lazima ipate Nahodha Mpya, kwa sasa haiaminiki na Jamii!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Aliondolewa kwenye Chama automatically ila yeye mwenyewe alishakuwa hana kumbukumbu tena 🐼
Hakuondolewa bali hakugombea nafasi ya chama baada ya kuondolewa kwenye urais. Shida mnafananisha scenario mbili tofauti.
 
CDM itapotea kabisa kuwa na mtu kama huyo - wajumbe malizeni kazi mapema mkinusuru chama chenu kutekwa na watu wa ajabu ajabu.
Jamaa anatuaminisha watanzania kwamba CDM haipendwi na haiaminiwi tena na wamanchi na Tanzania.

Huyu jamaa hana nia njema na chama chenu.
 
Ujinga walioifanya akina Ntobi na Yeriko Nyerere kumvua nguo Mbowe Kijasusi zaidi ndio umeiua kabisa Chadema

Hata mwendawazimu hawezi kuiamini Chadema ya Mbowe πŸ˜‚

View: https://www.youtube.com/watch?v=RyC-0pblLsE&t=329s
Tumsikilize huyu mpiga debe na rafiki mkubwa wa Lissu. Yuko kwenye mkutano wa CCM, anazungumzia CDM na kumpigia chepuo rafiki yake huku amevaa kijani. Mbowe aliwastukia mapema ama sivyo ingekuwa shida tupu.

Amandla...
 
Makamu mwenyekiti wa Chadema mh Tundu Lissu amesema kwa sasa chama chao kimepoteza Imani kwa Wananchi

Lissu amesema ili Chadema iaminike ppendwe na kuthaminiwa tena na Wananchi ni Lazima ipate Nahodha mpya

Mlale Unono πŸ˜„
Ni kweli. Sasa hivi haina mvuto tena
 
Makamu mwenyekiti wa Chadema mh Tundu Lissu amesema kwa sasa chama chao kimepoteza Imani kwa Wananchi

Lissu amesema ili Chadema iaminike ppendwe na kuthaminiwa tena na Wananchi ni Lazima ipate Nahodha mpya

Mlale Unono πŸ˜„
Kuna kaukweli
 
Lissu ni punguani.
Lisu siyo punguwani, wanaharakati malipo yao wanapokea kutoka kwa mabeberu.

Wanaharakati nchi ikipowa hawana raha na wala hawawezi kupokea fund yoyote.

Lisu ana hamu ya damu za Watanzania, ukitaka siasa radical na serikali inakuwa radical pia.

Pale Msumbiji yule anayepinga matokeo amekimbia nchi uku amewaacha vijana wajitowe sadaka damu yao, nadhani hiki ndicho kosa kubwa la Mbowe hataki kuwatowa Watanzania sadaka ya damu.

Ukiwa umemsikiliza Lisu vizuri anataka siasa za nginjanginja ambazo kwa Africa unakwenda kuuwa watu wasionufaika na chochote kwa maslahi ya watu wachache.
 
Kwa mtu mwenye akili timamu ukimsikiliza Lisu ni Magufuli mtupu ingawa mwenzake alikuwa na kautulivu kidogo na kujifanya anamuweka Mungu mbele.

Mimi mtu yeyote anayejiona yeye ndio muarobaini wa kila jambo au jambo huwa namuona ni mpuuzi tu.

Lisu hana sifa za kuwa kiongozi wa ngazi ya juu kabisa hana uwezo wa kuunganisha zaidi ya kujaza chuki tu na yakimzidi atakimbilia kwa Amsterdam ulaya.
 
Makamu mwenyekiti wa Chadema mh Tundu Lissu amesema kwa sasa chama chao kimepoteza Imani kwa Wananchi

Lissu amesema ili Chadema iaminike ppendwe na kuthaminiwa tena na Wananchi ni Lazima ipate Nahodha mpya

Mlale Unono πŸ˜„
Kwa hiyo Chadema haikuibiwa uchaguzi uliopita bali watu walikikataa kwa sababu wamemchoka Mbowe?

Amandla...
 
Huyu ndie Lisu alisema alikuwa hajawahi kuingia shule ya msingi muda uliopangwa na waalimu!!.Alikuwa anachelewa kwa ujeuri wake.Na bado anaendelea kukiuka katiba ya chama chake,hii ni shida ya kujitafutia.Bora Heche ana hekima ila huyu mjiandae
 
Lissu yupo sana Chadema na baada ya uchaguzi Chadema itakuwa moja na imara zaidi najua hamtaki lakini ndiyo hivyo Lissu Mwenyekiti ajaye.
Inawezekana kabisa kuwa Lissu atashinda uchaguzi na hivyo kuwa Mwenyekiti ajae wa Chadema. Lakini kusema kuwa baada ya uchaguzi CDM itakuwa moja ni kujidanganya. Hata kama Mbowe atapata kura 10 tu lakini kuna wengi watakuwa wamekwazika na jinsi alivyotendewa. Na patakuwa na kulipa visasi, hawata waacha watu kama Ntobi, Yericko salama. Watu hawatahama chama lakini watakaa pembeni.

Amandla...
 
Anaweza kushinda. Akishinda nchi italipuka kwa furaha. Shughuli itaanza baads ya hangover ya uchaguzi.

Amandla...
Na wakimuibia kura zake, watamkuta ACT kwenye kinyang'anyiro cha urais na atakomba wabunge wa kutosha.
 
Aondoke yeye Lisu, aiache chadema ikitamalaki. nani kamdanganya yeye anaaminika? Katudanganya juzi hapa kuhusu Tigo na kashambulia watu kisa kasoma gazeti la The gurdians.

Yeye akamsaidie Mwabukusu kule kwenye Samia leagal aide,siasa haziwezi.
 

..tusilaumu wanaharakati na wapinzani kwa makosa ya watawala.

..mgombea wa upinzani wa Msumbiji amekimbia kwasababu ya kuogopa kuumizwa na vyombo vya dola vinavyothibitiwa na chama tawala ikiwa atapinga matokeo.

..Waafrika na Watanzania tujiulize kwanini kuwe na siasa za nginjanginja? Nini kinatuzuia kuweka mifumo wezeshi kufanya siasa za haki, amani, na utulivu?

..Kwanini Watanzania tunazungumzia damu kumwagika wakati Raisi ameshasema kwamba kuna 4R? Nani anazuia 4R wakati bunge ni la CCM, serikali kuu, na za mitaa zote ni CCM?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…