Gerald .M Magembe
JF-Expert Member
- Jul 17, 2013
- 2,496
- 1,800
..hizo fedha hufika kwa mkurugenzi wa halmashauri.
..mbunge na madiwani hupanga matumizi ya fedha hizo.
..fedha hizo hazipiti hata siku moja ktk mikono ya mbunge.
..zaidi hizo fedha siyo nyingi, zinatosha kutatua shida ndogo-ndogo tu.
Asante kwa ufafanuzi.
Daah kuna mikoa itabakia kwenye lindi la ufukara.
Mfano hapo Singida anakotoka Lisu zaidi ya vitunguu na karanga sijui kuna nini pale jamani.
Lisu anaongea kama hajui alikotoka bwana.
Kura nyingi tu atapataSalamu kwako Tundu Antiphas Lissu, Shalom,
Leo napenda kukwambia rasmi kuwa , Kura yangu iko kwako! Na hii ndo sababu yangu kuu ya kukupa kura!
Katika maisha yangu nimekuwa nikifanya utafiti sana juu ya dhana ya umasikini wa watanzania na Tanzania kwa ujumla, Moja ya sababu ambayo niligundua kwenye utafiti wangu ni kuwa Tanzania tuna mfumo mbovu sana wa utawala ambao vyovyote vile hatuwezi kuendelea kwa mfumo huu!
Mfumo huu ninaousema ni mfumo kuwa fedha zote za watanzania zinakusanywa na kuwekwa chini ya mtu mmoja( raisi ambayo yeye ndo anayeamua kuwa hizo fedha zigawanywe kivipi)
Madhara ya mfumo huu ni kuwa umeondoa uwajibikaji kwa wananchi na viongozi, umeondoa ubunifu kwa wananchi na viongozi na mwisho umepelekea tabia ya ombaomba na unafiki kwa wananchi na viongozi
Mfumo huu pia umechochea ufisadi wa kiwango kikubwa sana kwa wananchi na viongozi na kama Kuna mtu anabisha Leo hii aniambie maisha ya ukwasi wanayoishi maraisi wastaafu yametokana na nini???
Hapa Tanzania hakuna raisi mstaafu mwenye maisha ya utajiri wa kuwaida. Wengi wana utajiri mkubwa wa real estate, kilimo kikubwa na hata pia makampuni makubwa ya uzalishaji. Na kibaya ni kuwa vyote hivi huwa wanavipata wakiwa maraisi. Sababu ya haya yote ni kuwa tumekuwa na mfumo wa kuziweka fedha zote za nchi chini ya mtu mmoja.
Leo hii raisi ni kama Mungu hapa Tanzania. Kila aendapo watu ni kulia shida, awafanyie hiki na awaletee hiki, haya yote ni kwa sababu ya mfumo mbovu tulionao ambao umeondoa uwajibikaji na ubunifu kwa watanzania na viongozi wetu
Kwa nini Mfumo wa Majimbo ndo suluhisho wa haya yote?
1. Mfumo wa majimbo utafanya hela zote zinazokusanywa kwenye sehemu husika zitumike kwa matakwa ya wananchi wa sehemu husika mf. Kujenga barabara , hospitali, shule bora na huduma bora za Maji na umeme!! Hili litafanya wananchi wasiwe wajinga kwa viongozi wao na kamwe was iwe ombaomba na watu wa kujipendekeza kwa viongozi wao.
2. Mfumo wa majimbo utachochea ubunifu kwa wananchi kufanya shughuli mbalimbali bora za uzalishaji ili majimbo yao yakusanye fedha za kutosha kwa ajili ya maendeleo yao.
Kama jimbo husika linategemea kilimo basi wananchi wa hilo jimbo watafanya kilimo bora na watakifanya cha biashara ili wapate mapato mazuri ya kuendeleza jimbo lao kimiundombinu na Pia kimaendeleo. Hakuna sehemu watu watalala au kuwa wazembe na watakuwa wakali kwa viongozi wao kuwahamasisha wawe agressive kwenye kubuni miradi bora ya maendeleo kwa maendeleo yao.
Mfumo huu utatengeneza wananchi wanaojiamini na Kuwajibika kweli katika kutunza rasilimali zao ili ziwasaidie wao na uzao wao. Wananchi hawatakuwa wazembe na watawawajibisha kweli viongozi wasio wabunifu kwenye kutengeneza vyanzo vya mapato kwa sababu watakuwa wanajua bila vyanzo vya mapato bora na vya uhakika kwenye maeneo yao basi watakuwa nyuma kimaendeleo na hawataweza kunsurvive.
Mfumo wa majimbo utafanya kama sehemu Kuna mbuga za wanyama basi wananchi wa maeneo husika wazitunze rasilimali kweli kwa sababu watajua kweli bila mbuga hizo utalii utakufa na hawatapata mapato ya kulipa mishahara wafanyakazi wao, kujenga barabara na mitaa bora, kuhudumia Bima za afya na madawa hospitali. Kwa iyo Kama jimbo litategemea utalii basi watautunza na kuuthamini kweli utalii.
Kama jimbo linategemea viwanda au biashara basi jimbo hilo litatunga Sera bora ili kuhamasisha uwekezaji mkubwa wa viwanda na biashara kwa sababu wananchi wa sehemu husika watajua bila hivyo basi hawawezi pata mapato ya kununulia dawa, kupata Maji safi na salama na kujenga barabara nzuri!
Kama jimbo husika linategemea kilimo na migodi basi wananchi wa viongozi wa maeneo husika wataumiza kichwa kuweka Sera bora katika hayo maeneo ili kuhakikisha zinawapatia mapato makubwa ya kufanya miradi ya maendeleo. Watu watajiona kweli kuwa wao ni sehemu sahihi ya maendeleo husika.
Imefika wakati watanzania lazima tuseme kuwa mfumo wa utawala wa Chama cha mapinduzi, umechochea sana ufisadi, umasikini, kujipendekeza, uzembe, ubabaishaji na kutowajibika kweli kwa Watanzania!!!
Mfumo huu wa sasa umefanya watanzania tudharauliwe na viongozi na kuendeshwa Kama watoto wadogo kuwa tusipowachagua watu wao basi tusahau maendeleo kwa sababu wao ndo wanaamua hela zetu wazigawe vipi!! Hii sio sawa kabisa
Mfumo huu wa sasa umesababisha watu kuwa ombaomba na watumwa kwenye nchi yao kuwa kila wakimuona Raisi basi wamnyenyekee kama Mungu n kumuomba hiki na kile. Kama Raisi tunaomba Maji, barabara, umeme na shule bora
Kwa maendeleo ya kweli ni lazima Watanzania tuamue kwenye uchaguzi huu kumchagua Tundu Antiphas Lissu ili atubadirishie mfumo.
Hamasisha watu wengi zaidi kumchagua Lissu na Chadema kwa maendeleo ya kweli ya Tanzania na Watanzania!
Sambaza kwa watu wengi zaidi waelimike pia!!
Asanteni!
Lord denning.
Bahati mbaya Lissu hakusanyi kodi inayotolewa na wananchi wa Singida, na anayekusanya anajua anakozipelekaDaah kuna mikoa itabakia kwenye lindi la ufukara. Mfano hapo Singida anakotoka Lisu zaidi ya vitunguu na karanga sijui kuna nini pale jamani. Lisu anaongea kama hajui alikotoka bwana.
Hujaelewa madaBahati mbaya Lissu hakusanyi kodi inayotolewa na wananchi wa Singida, na anayekusanya anajua anakozipeleka
Daah tatizo lenu hoja zenu ni za kufikirika na za kwenye makaratasi hazina uhalisia...Singida wanalima alizeti.
..utafiti uliofanyika hivi karibuni umebainisha kwamba Korosho inaweza kustawi Singida.
..Singida pia ni wafugaji wazuri wa kuku, mbuzi, na ng'ombe.
..hakuna eneo masikini ktk Tanzania yetu.
Magufuli anatosha mkuu
Ufisadi utahamia majimboni, Hapa jimbo la Hai kwa miaka 15 iliyopita pesa za mfuko wa jimbo umefanya kazi mwaka huu tuu, na pesa ziligawiwa kwenye miradi na Mkuu wa wilaya.
Kwa miaka 14 hizi pesa Mbowe alikuwa anapeleka wapi? jana aliulizwa hili swali Uswaa Machame, na mkutano ulivunjika na akaondoka kwa kuzomewa.
Labda sehemu zingine lakini Kilimanjaro labda jimbo la Same Kusini (mwana mama ) na Same Mashariki (katika vitu Mzee Cleopa Msuya amefanikiwa ni dicipline kwa kizazi chake )lakini maeneo yaliyo baki tumepigwa na wabunge ni kutoka Upinzani.
Daah tatizo lenu hoja zenu ni za kufikirika na za kwenye makaratasi hazina uhalisia.
Ona unavyotaka kudanganya watu hapa kuwa kuku wanaweza endesha maendeleo ya mkoa.
Tusaidie tu contribution kwa sasa kwa mkoa wa singida kwa pato la Taifa.
Mjiandae kulipa fidia mikoa ambayo kwa muda mrefu toka uhuru mchango wake katika pato la Taifa umetumika kuendeleza kwingine.
Salamu kwako Tundu Antiphas Lissu, Shalom,
Leo napenda kukwambia rasmi kuwa , Kura yangu iko kwako! Na hii ndo sababu yangu kuu ya kukupa kura!
Katika maisha yangu nimekuwa nikifanya utafiti sana juu ya dhana ya umasikini wa watanzania na Tanzania kwa ujumla, Moja ya sababu ambayo niligundua kwenye utafiti wangu ni kuwa Tanzania tuna mfumo mbovu sana wa utawala ambao vyovyote vile hatuwezi kuendelea kwa mfumo huu!
Mfumo huu ninaousema ni mfumo kuwa fedha zote za watanzania zinakusanywa na kuwekwa chini ya mtu mmoja( raisi ambayo yeye ndo anayeamua kuwa hizo fedha zigawanywe kivipi)
Madhara ya mfumo huu ni kuwa umeondoa uwajibikaji kwa wananchi na viongozi, umeondoa ubunifu kwa wananchi na viongozi na mwisho umepelekea tabia ya ombaomba na unafiki kwa wananchi na viongozi
Mfumo huu pia umechochea ufisadi wa kiwango kikubwa sana kwa wananchi na viongozi na kama Kuna mtu anabisha Leo hii aniambie maisha ya ukwasi wanayoishi maraisi wastaafu yametokana na nini???
Hapa Tanzania hakuna raisi mstaafu mwenye maisha ya utajiri wa kuwaida. Wengi wana utajiri mkubwa wa real estate, kilimo kikubwa na hata pia makampuni makubwa ya uzalishaji. Na kibaya ni kuwa vyote hivi huwa wanavipata wakiwa maraisi. Sababu ya haya yote ni kuwa tumekuwa na mfumo wa kuziweka fedha zote za nchi chini ya mtu mmoja.
Leo hii raisi ni kama Mungu hapa Tanzania. Kila aendapo watu ni kulia shida, awafanyie hiki na awaletee hiki, haya yote ni kwa sababu ya mfumo mbovu tulionao ambao umeondoa uwajibikaji na ubunifu kwa watanzania na viongozi wetu
Kwa nini Mfumo wa Majimbo ndo suluhisho wa haya yote?
1. Mfumo wa majimbo utafanya hela zote zinazokusanywa kwenye sehemu husika zitumike kwa matakwa ya wananchi wa sehemu husika mf. Kujenga barabara , hospitali, shule bora na huduma bora za Maji na umeme!! Hili litafanya wananchi wasiwe wajinga kwa viongozi wao na kamwe was iwe ombaomba na watu wa kujipendekeza kwa viongozi wao.
2. Mfumo wa majimbo utachochea ubunifu kwa wananchi kufanya shughuli mbalimbali bora za uzalishaji ili majimbo yao yakusanye fedha za kutosha kwa ajili ya maendeleo yao.
Kama jimbo husika linategemea kilimo basi wananchi wa hilo jimbo watafanya kilimo bora na watakifanya cha biashara ili wapate mapato mazuri ya kuendeleza jimbo lao kimiundombinu na Pia kimaendeleo. Hakuna sehemu watu watalala au kuwa wazembe na watakuwa wakali kwa viongozi wao kuwahamasisha wawe agressive kwenye kubuni miradi bora ya maendeleo kwa maendeleo yao.
Mfumo huu utatengeneza wananchi wanaojiamini na Kuwajibika kweli katika kutunza rasilimali zao ili ziwasaidie wao na uzao wao. Wananchi hawatakuwa wazembe na watawawajibisha kweli viongozi wasio wabunifu kwenye kutengeneza vyanzo vya mapato kwa sababu watakuwa wanajua bila vyanzo vya mapato bora na vya uhakika kwenye maeneo yao basi watakuwa nyuma kimaendeleo na hawataweza kunsurvive.
Mfumo wa majimbo utafanya kama sehemu Kuna mbuga za wanyama basi wananchi wa maeneo husika wazitunze rasilimali kweli kwa sababu watajua kweli bila mbuga hizo utalii utakufa na hawatapata mapato ya kulipa mishahara wafanyakazi wao, kujenga barabara na mitaa bora, kuhudumia Bima za afya na madawa hospitali. Kwa iyo Kama jimbo litategemea utalii basi watautunza na kuuthamini kweli utalii.
Kama jimbo linategemea viwanda au biashara basi jimbo hilo litatunga Sera bora ili kuhamasisha uwekezaji mkubwa wa viwanda na biashara kwa sababu wananchi wa sehemu husika watajua bila hivyo basi hawawezi pata mapato ya kununulia dawa, kupata Maji safi na salama na kujenga barabara nzuri!
Kama jimbo husika linategemea kilimo na migodi basi wananchi wa viongozi wa maeneo husika wataumiza kichwa kuweka Sera bora katika hayo maeneo ili kuhakikisha zinawapatia mapato makubwa ya kufanya miradi ya maendeleo. Watu watajiona kweli kuwa wao ni sehemu sahihi ya maendeleo husika.
Imefika wakati watanzania lazima tuseme kuwa mfumo wa utawala wa Chama cha mapinduzi, umechochea sana ufisadi, umasikini, kujipendekeza, uzembe, ubabaishaji na kutowajibika kweli kwa Watanzania!!!
Mfumo huu wa sasa umefanya watanzania tudharauliwe na viongozi na kuendeshwa Kama watoto wadogo kuwa tusipowachagua watu wao basi tusahau maendeleo kwa sababu wao ndo wanaamua hela zetu wazigawe vipi!! Hii sio sawa kabisa
Mfumo huu wa sasa umesababisha watu kuwa ombaomba na watumwa kwenye nchi yao kuwa kila wakimuona Raisi basi wamnyenyekee kama Mungu n kumuomba hiki na kile. Kama Raisi tunaomba Maji, barabara, umeme na shule bora
Kwa maendeleo ya kweli ni lazima Watanzania tuamue kwenye uchaguzi huu kumchagua Tundu Antiphas Lissu ili atubadirishie mfumo.
Hamasisha watu wengi zaidi kumchagua Lissu na Chadema kwa maendeleo ya kweli ya Tanzania na Watanzania!
Sambaza kwa watu wengi zaidi waelimike pia!!
Asanteni!
Lord denning.
πππ[emoji3577]View attachment 1572872
Kuna kila haja ya kila mtanzania anaeipenda kweli nchi yake kuwa balozi wa Lissu, kumuombea kura Lissu kwa watu mbalimbali na kuhamasisha wamchague ili hatimaye watanzania tupate maendeleo ya kweli ya watu na vitu!
Asante sana kwa hoja makini!Haiwezekani kukawa na ufisadi sababu wananchi watakuwa na mamlaka ya kumuondoa madarakani kiongozi yeyote wa jimbo tofauti na sasa hata kukiwa na ufisadi mahali hadi kiongozi mkubwa ambaye hakushirikishwa kwenye huo ugisadi aje atembelee hapo nfipo utasikia kuna ufisadi, lakini wananchi wanakuwa wanafahamu ila hawana uwezo sababu viongozi wao ni wateule. Huu utawala wa majimbo ni mwisho wa mafisadi wanaiba pesa sababu wanakuwa na uamuzi wa kuzitumia kwa chochote kile sasa zikiwa jimboni zitakuwa na matumizi ya jimbo.
Hebu fikitia hivi geita lingekuwa jimbo linajitegenea kweli wangetumia pesa za kodi zao kujenga uwanja wa Ndege wa kimataifa chato na je wangekuwa kweli wanafikiria kujenga uwanja wa michezo kwa ajiri ya kuja kutembelea watalii. Haya matumizi mabaya ya pesa ndiyo yanasababisha umasikini kwa watanzania na utajiri kwa watu wachache kutokana na ufisadi.
Kama unataka kuendekea kuwa masikini na kutoa nafasi kwa viongozi kuwa mafisadi utapigia kura CCM lakini kama umechoshwa na umasikini na ufisadi utapigia kura CHADEMA. Mimi kura yangu nitampa Tundu Lissu sababu najuwa anayo agenda ya kweli ya kutuonfoa katika huu umasikini ambao CCM wameshindwa kuondoa miaka 59 sasa.
Acheni kupotosha watu kwa akili zenu mgando? Kwani Singida hakuna migodi ya dhahabu? Hakuna mapori ya akiba???Hujui kuwa Singida ndo wanaongoza kwa uzalishaji wa alizeti???Daah tatizo lenu hoja zenu ni za kufikirika na za kwenye makaratasi hazina uhalisia.
Ona unavyotaka kudanganya watu hapa kuwa kuku wanaweza endesha maendeleo ya mkoa.
Tusaidie tu contribution kwa sasa kwa mkoa wa singida kwa pato la Taifa.
Mjiandae kulipa fidia mikoa ambayo kwa muda mrefu toka uhuru mchango wake katika pato la Taifa umetumika kuendeleza kwingine.
Itoshe kusema tu kuwa hiyo sera ni mbovu itabomoa umoja wa kitaifa tuliokuwa nao tangia tunapata uhuru, itazua taharuri na migongano baina ya jamii zetu bila ulazima wowote.Acheni kupotosha watu kwa akili zenu mgando??? Kwani Singida hakuna migodi ya dhahabu? Hakuna mapori ya akiba???Hujui kuwa Singida ndo wanaongoza kwa uzalishaji wa alizeti???
Alafu unafikiri jimbo la kati litakuwa na Mkoa wa Singida peke yake?? Kwa taarifa yako Jimbo la kati linaweza kuwa na sehemu ya Mkoa wa Morogoro, Sehemu ya Mkoa wa Manyara, na mikoa ya Dodoma na Singida. Hujui mikoa yote hiyo ina kilimo kikubwa kinachowezwa kuboreshwa na kufanywa cha biashara ya kuingiza mapato makubwa??? Hujui kuwa kuna mapori ya akiba yenye wanyamapori wa kutosha yanayoweza kitumika vizuri kiutalii na kuingiza mapato mengi sana??? Hujui kuna viwanda pia ambavyo vitazalisha vidhaa na kuingiza mapato mengi sana???
Tatizo CCM mmenyimwa sana akili. Ndo mana kila siku watanzania wanazidi kuwa mafukara
Unaitaji kuelimika. Inaonekana elimu ya CCM imekupumbaza sana akili!Itoshe kusema tu kuwa hiyo sera ni mbovu itabomoa umoja wa kitaifa tuliokuwa nao tangia tunapata uhuru, itazua taharuri na migongano baina ya jamii zetu bila ulazima wowote.
Tafuteni jambo jingine la kudanganya watu ila sio hili.
Mwafaaa mwaka huu ,mungu Alisha kataa tangu 4 7 siku zilizo pitaMagufuli anatosha mkuu