Ndio sampuli ya washabiki wa Lissu na mapoyoyo kama kina Mwabukusi (wanasheria uchwara).
Ndio maana mmeshindwa kuelewa IGA sehemu kubwa ilikuwa ni dispute resolution na investment conditions
(Contract offer).
Hayo mambo kama hayapo kwenye BIT au special investment kama IGA. Basi kwenye mkataba wowote wa kimataifa lazima privately yawepo kwenye ‘host nation’ agreement. It’s standard on FDI contacts to include ADR terms.
Hakuna upuuzi kama MIGA kwenye international FDI kuna isipokuwa kuna agreed terns of alternative dispute resolution (ADR) process. Those must be addressed in the contract up until arbitration; being the highest level of international decisions.
Hakuna upuuzi wa MIGA, kila siku nchi inashitakiwa unewahi kusikia mwekezaji anasema MIGA, if anything watatumia BIT.
Hana analolijua Lissu kuhusu Mikataba, same as Kabudi.
..ungewaelimisha wanajamvi MIGA ni nini wangeweza kuelewa hoja yako, na kuyafahamu madhaifu ya Lissu.
..ripoti za Mruma na Ossoro inaelekea hazikuwa za kweli. Kama zingekuwa za kweli serikali ilitakiwa ikashtaki ili Watanzania tulipwe mabilioni.
..kinyume chake serikali ndio imeshtakiwa, na Watanzania tutalazimika kulipa mabilioni kama sio matrilioni.
..wakati huohuo Prof.Kabudi aliyekuwa kinara na msemaji Mkuu wa serikali wakati wa vita na walioitwa mabeberu amejitokeza na kusema kodi ambayo serikali ilisema inawadai Acacia haikuwa ya kweli.
..kuongeza chumvi kwenye kidonda, Deo Mwanyika, aliyekuwa Afisa wa ngazi ya juu wa Acacia, na Barrick, amepewa ubunge na Ccm.
..Zaidi, Prof.Mruma ambaye aliongoza mojawapo ya Tume za Uchunguzi, na alilia machozi siku kuwasilisha ripoti mbele ya Raisi, ameonekana ktk luninga akishindwa kuitetea serikali iliposhtakiwa.
..Katika mazingira hayo, hivi utaiamini Serikali, au utawaamini waliokuwa wakitilia mashaka ripoti, na hatua za serikali?