Lambert alimuuliza Lissu swali la kushtukiza kuhusu msimamo wake kuhusiana na vita ya Drc na Ukraine kama angebahatika kuwa Raisi.
Lissu alijibu kwa kifupi kuhusu Drc kwamba suluhisho ni kuunganisha nguvu za nchi majirani ili kupata amani nchini humo.
Kuhusu vita vya Ukraine Lissu aliibua hoja ambazo nadhani Watanzania wengi hawana habari nazo. Lissu alirejea msimamo wa Tanzania au Mwalimu Nyerere kuhusu vita vya Soviet Union na Czechoslovakia mwaka 1968. Vilevile alielezea historia ya matishio ya usalama wa Russia tangu enzi za Napoleon, na kusisitiza kwamba suala la usalama wa Russia ni lazima lichukuliwe kwa umakini ktk kutatua mgogoro kati yake na Ukraine.
Kwa kifupi Lissu ana elimu[vijana wanaita madini] kubwa sana ambayo ili kuipata waandishi wa habari wanatakiwa waulize maswali sahihi, na sio maswali ambayo Lissu ameshayajibu mara kadhaa.
Lissu alijibu kwa kifupi kuhusu Drc kwamba suluhisho ni kuunganisha nguvu za nchi majirani ili kupata amani nchini humo.
Kuhusu vita vya Ukraine Lissu aliibua hoja ambazo nadhani Watanzania wengi hawana habari nazo. Lissu alirejea msimamo wa Tanzania au Mwalimu Nyerere kuhusu vita vya Soviet Union na Czechoslovakia mwaka 1968. Vilevile alielezea historia ya matishio ya usalama wa Russia tangu enzi za Napoleon, na kusisitiza kwamba suala la usalama wa Russia ni lazima lichukuliwe kwa umakini ktk kutatua mgogoro kati yake na Ukraine.
Kwa kifupi Lissu ana elimu[vijana wanaita madini] kubwa sana ambayo ili kuipata waandishi wa habari wanatakiwa waulize maswali sahihi, na sio maswali ambayo Lissu ameshayajibu mara kadhaa.