Tundu Lissu: Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu

Aina ya Muungano wa Karume na Nyerere ni Tofauti na Muungano wa Sasa,kwani Muungano wa Sasa umejaa Magumashi,Ukiritimba,na Maujanja Mengi,Hata Zanzibar wametumia Fursa hiyo Kujigeuza Nchi Kinyemela na sasa Rais wao ni Amri jeshi anakagua Gwaride la vikosi vya Ulinzi nk,Waziri Mkuu Hana Sauti au mamulaka Zanzibar ,ni Kama hawamtambui,Nyerere alipenda mabadiliko Ndio Maana alianzisha mfumo wa Vyama vingi, Nina imani angekuwa Hai lazima angekubali kwenda na wakati , yaani kuirejesha Tanganyika na kumaliza Unyonyaji wa Zanzibar juu ya Pesa za Tanganyika kwa visingizio vya kumaliza Kero za Muungano.
 
Waarabu tuna usemi NI RAHISI SANA KUWADANG'ANYA WATU, LAKIN NI VIGUMU SANA KUWAAMBIA WATU KUWA MUMEDANG'ANYWA NA WAKAKUAMINI.

Ahsantum Tundu Lissu kwa kubainisha usemi wa Bob Marley katika album yake ya Uprising wimbo Redemption. alinena hivi
YOU CAN FOOL SOME PEOPLE SOMETIMES BUT YOU CAN'T FOOL ALL THE PEOPLE ALL THE TIME.

Hongera sana Tundu Liss
u
 

Nyerere ktk Hotuba zake alikubali Kuwa Wakati wa Utawala wake wa Miaka 26 Serikali yake ilitenda Mabaya na Mazuri ,lakini ikija Serikali mpya inachukua Mazuri hasa ya Msingi inayaendeleza na Yale mabaya wanaachana nayo , huenda Muungano kukosa Hati ni mojawapo ya Mabaya,lakini Tambua Nyerere alikiri Mapungufu Enzi ya Utawala wake , hapaswi kulaumiwa sana,Watawala wa sasa Ndio wa kulaumiwa kwa Kuiruhusu Zanzibar kujitangaza Kuwa ni Nchi huku Pesa za kuwahudumia zikitoka Tanganyika ambayo sasa imekuwa Koloni la Zanzibar inasaka uhuru wake.
 
Tindu lisu uliyesoma bure leo unaweza kumtukana Nyerere? Siasa imekupa kiburi? Nimekutemea mate usoni puuuuuu.
Amemtukanaje Nyerere?, hoja ipingwe kwa hoja, acheni ushabiki wa kipuuzi, kama vipi weka hayo matusi aliyotukana, jamaa ana vithibitisho kabisa, wewe unakuja na maneno matupu tena ya kijinga...
 
Jumbe alikuwa si Mzanzibari?

Wolfgang Dourado alikuwa si Mzanzibari?

Tundu Lissu anasema wote hao walipohoji kuhusu muungano Nyerere aliwaweka kizuizini.

Njoo na lingine.


Dada yangu Kigezo/vigezo ambavyo Nyerere aliviweka ni kuwa ukitaka kutilia qn mark muungano ni uwe na hoja zenye mashiko vinginevyo wewe ni mhaini tu.

kwa mfano ukiwa na ulevi au tamaa ya madaraka na ukaona muungano ni kikwazo kutimiza malego yako haya bac wewe ni mhaini.

Ukitumiwa na watu kutoka nje kutaka kuuvunja muungano kwa faida yako na wanaokutumia wewe ni mhaini.

Mkikaa kikao na watu wazima wenzako mkakubaliana mambo fulani fulani kuhusu muungano na ukitoka hapo ukawageuka wenzako wewe ni mhaini.

Ukifanya mambo ya muungano kwa siri siri bila uwazi kwa wenzako, hata kama nia yako ni njema juu ya muungano bac wewe ni mhaini. nk, nk, nk.

Sasa ilikuwa ni juu ya lissu na wewe unaye mshadadia mtueleze na kutuhakikishia kuwa hao waliokutana na dhahama hizo hawa kufanya mambo kama hayo au yanayo fanana na hayo? Na baada ya hapo ndio mtuhumu Nyerere kwa uongo.

Vinginevyo lissu kakosea sana na nafasi atakoyopewa kesho aitumie kuwaomba radhi Watanganyika.

Na asipofanya hivyo kauli yake hii dhidi ya Nyerere itamwandama katika maisha yake yote kama mwanasiasa mark my words.

Ukitaka kuhakikisha hilo subiri uone hii kauli yake kwa kuanzia, itakavyo tumiwa kumuandama na pro ccm katika hili bmk.
 
Nyerere alikubali kitambo Kuwa kipindi cha utawala wake walikuwa na mapungufu Yao,walitenda mabaya na Mazuri, lakini Nyerere alisisitiza ikija Serikali mpya inachukua Mazuri hasa ya Msingi inayaendeleza na Yale mabaya inayatupa kapuni,pitia Hotuba zake utabaini Hilo,huenda hili la muungano kukosa Hati likawa mojawapo wa mabaya Ndio Maana Zanzibar wakatumia Fursa hiyo kujibadili Kuwa Nchi kinyemela na kuendeleza ulalamishi ili muungano Ufariki kila mmoja akae kwake.
 

Mimi sikutaka hata kuwajengea hoja kina Dkt. Mwakyembe na Prof. Shibji kwa sababu machapisho yao ni matokeo ya msingi uliowekwa na Mwl. Nyerere. (Muungano).

Kama tunayoambiwa na Tundu Lissu ni kweli, basi hata machapisho yao mengi yatakuwa ni kaput.

Kama katika misingi ya sheria, hakukuwepo na Muungano, basi hata machapisho yao ambayo yalikuwa yamejikita kwenye Muungano wa Watanzania ambao kiuhalisia kisheria haupo basi, matokeo ya kutokuwepo huo muungano yanayafanya hata machapisho yao kuwa useless.

wajubi wa misemo wanasema, ni bora kuongea na mwenye mbwa kuliko kuongea na mbwa!.

Hiki nilichofanya ndiyo ku-balance hoja badala ya kuwawekea political blanket wakati wao siyo waasisi wa Muungano.

Kama ni ku-balance issue kwa jinsi unavyotaka wewe, kwa nini hujahoji katika suala la Muungano, Mh. Lissu katika hoja zake hakutaja jina la Abeid Amani Karume badala yake akanukuuu maandiko ya Mwl. Nyerere pekee.

La mwisho, Mambo ya vyama yanaimgiaje hapa?. Hivi ni kigezo gani unatumia kufahamu kama mwanaJf fulani ni CHADEMA , CUF, CCM, NCCR-Mageuzi, TLP na UDP wakati mtu mwenyewe amejificha kwenye unverified ID?.

Kwani wewe ni chama gani kama mimi ni CCM?.
 
Wewe unadai aina ya Muungano wa Abeid Amani Karume na Mwl. Nyerere wakati wenzako wanakuambia, kisheria hakukuwa na Muungano!.

Hujasikia watu bungeni wanahoji cheti halisi cha Muungano?.
 
Kwa hiyo unaulibali uwongo na udanganyifu wa Mwl. Nyerere kuhusu Muungano?. Mh. Lissu amesema, Mwl. Nyerere alikuwa muongo na mdanganyifu kama alivyobainisha kwenye maandiko yake na vitendo vyake.
Mbona mimi nilisikiliza hotuba ya Tundu Lissu hayo maneno kwenye bold sikuyasikia au we runinga yako inasikikaje au ina fasiri kabisa, halafu mbona unanukuu kana kwamba runinga unayo mwenyewe humu jf, acha upotoshaji basi, au TBC walipokata akaendelea akatamka hivyo?
 

Nyerere ni mnafik tu. Mbona aliendelea kuutetea Muungano hata alipokwisha ng'atuka? hiyo ilikuwa Serikali ya nani mjomba'ke?
 
Lissu omba radhi. Kumtukana Nyerere ni kuwatukana watanzania

Nyerere ktk zile Hotuba zake alikiri Mapungufu wakati wa Utawala wake uliodumu kwa Miaka 26 alikubali Walitenda Mabaya na Mazuri , hawakuwa Malaika . Nyerere alisisitiza Serikali mpya ikiingia ikulu inayachukua Yale Mazuri yote na kuyaendeleza ,eti tena cha ajabu hata mazuri yanawekewa question mark? Na Yale mabaya yanatupwa kapuni,Nyerere alijua ipo siku Haya yatatokea Ndio Maana alikubali mapungufu mapema,na pengine mojawapo wa Mabaya ni muungano kutokuwa na Hati , lakini haipaswi kumlaumu sana Nyerere kuliko Hawa walioruhusu Zanzibar Kuwa Nchi kinyemela huku Tanganyika inataabika na pesa zake kutumila kuilisha Zanzibar na kuubembeleza muungano.
 

- Tundu Lissu si amezaa mtoto na mbunge wa viti maaalum wa Chadema na kumuwachilia mbali sasa kweli anaweza kumtupia mawe Baba wa Taifa kuwa ni mnafiki kuliko yeye? jamani chonde chonde na hiyo Rasimu yenu na UKAWA yaani katiba mpya ndio mtukane hata muasisi wa Taifa kisa UKAWA tu? DUH

Le Mutuz System
 
debe tupu ni wewe pamoja na Ng'wamapalala

Mkuu, mbona unatukia ghadhabu dhidi ya ndugu yetu mleta mada hapa jamvini!¿ Daah¡

Kama "kosa" la kusema ukweli juu ya yule Julius Nyerere...basi mlaumu yule MP wa Chadema Bwana Tundu Lissu!

Nyerere aliishi kwa urongo,unafiki,uzandiki,vitisho dhidi ya wenzie na kuwachafua kisiasa. Pia Nyerere alizoea vya kunyonga,ndo maana hakutamani vya kuchinja!? - By Tundu Lissu Chadema MP!

Wako wapi wale Chadema wafia Unyerere akina Mag3,Nguruvi3,Mwanakijiji na wafuasi wao/vilaza wenzi wao!? Daah!

Weye mfia Unyerere wa kambi ya CCM aka Chama wa Gongo la Mboto uko wapi!?

Mnaona sasa,mpaka Wabunge wenu wachovu,nao sasa wameanza kuamka na kupata Darsa za Mkuu FaizaFoxy...kukhusu unyama wa yule Dikteta Nyerere!? Daah!

Kikwete...tafadhali kamwombe radhi Rais Mzee Aboud Jumbe, kwa niaba ya Watanzania soote wapenda ukweli;haki na amani!

Ahsanta sana.
 
Last edited by a moderator:
Muungano wa Marekani ni Nchi 52 Hakuna kero za muungano wala Wizara ya muungano,Michango ya gharama za muungano hutolewa kwa wakati si Kama ZNZ wamekwepa kwa Miaka 47 ,muungano wao upo Digtal ,Uchoyo wa Ardhi,Udini,Ubaguzi,Ulalamishi nk ni Mwiko,Zile Nchi ndogo ngogo hazina Utitiri wa Wabunge,viongozi na Watumishi wa Umma kwa kutegemea Walipiwe Mishahara na Nchi zingine,kila Nchi inajitegemea ktk mahitaji ya kijamii ,wabunge hawachukui posho Mara 2 si kama Zanzibar wabunge wanavuna Posho Dodoma,na wanaweza Kuwa Mawazili hata ktk zile Wizara ambazo si za Muungano,lakini Wabunge wa Tanganyika hawaruhusiwi kuingia kule Baraza za Wakilishi wala Kuwa Mawaziri kwenye baraza la mawaziri la Zanzibar.
 
Ebu acheni kumkandia na kumtusi Nyerere kwani Karume alikuwa wapi kipindi hicho au yeye hakuhusika kwenye muungano.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…