Gombesugu,kuna wengi walipoteza maisha kwenye utawala wa mkono wa chuma wa awamu ya kwanza,unayefikiri kavuliwa nguo ujue kasamehewa tu ana damu nyingi zisizo na hatia kichwani mwake!mwombee rehema za mungu huko aliko!na wewe usifanye aliyoyafanya hata kwa familia,ni uovu unaonuka!
Nyerere alikuwa binadamu kwa sehemu mjanja,kwa sehemu mbabe,kwa sehemu muumini wa ukristo kwa sehemu nyingine mshirikina-angalia mwenge na kadhia hizo.sasa kama hati ya muungano haipo un wala ikulu ya znz wala magogoni,tukisema huyu mzee alikuwa tapeli ila tu alikuwa si hatari kama hawa aliowaachia nchi,hatujatukana.mazuri anayotenda mtu anakwenda nayo kaburini,yale maovu yanabaki yakinuka na kumsuta!tunapoishi tuwe makini lissu huna kosa kweli itatuweka huru! Tusijetetea muungano kama ndege kasuku wakati hauna uhalali kisheria!
- Tundu Lissu si amezaa mtoto na mbunge wa viti maaalum wa Chadema na kumuwachilia mbali sasa kweli anaweza kumtupia mawe Baba wa Taifa kuwa ni mnafiki kuliko yeye? jamani chonde chonde na hiyo Rasimu yenu na UKAWA yaani katiba mpya ndio mtukane hata muasisi wa Taifa kisa UKAWA tu? DUH
Le Mutuz System
Mkuu gombesugu mleta mada ameleta mada ya uchonganishi kwa sababu ametia fitina kuna mada nyingi zimeongelea alichosema Tundu Lissu ila huu ni uchambuzi wa mleta mada, kwa sababu kama kumsikia Tundu Lissu wote tulimsikiliza wala sio alisikia yeye mwenyewe sasa yeye amekuja na uchambuzi wake yaani amefasiri alivyoelewa yeye na lengo la mleta mada limefanikiwa, anajua lengo lakeMkuu wa Chuo,
Kwa context ya hiyo bayana yako dhaifu hapo juu...je unaamisha yakua Bwana mleta mada,Mkuu Ng'wamapalala...ndie mrongo na mfitinishi!? Na sio yule Julius Nyerere,kama tulivyoaminishwa na Tundu Lissu!? Duuh!
Hapana sio kwamba tumekuja kumchafua mleta mada licha ya hivyo mleta mada hajulikani ukiongelea Ng'wamapalala wapo wengi sasa hapo sijajua mleta mada atakuwa amechafuka vipi!?Weye na wenzio nakhis hoja zenu ni muflis...na labda mmeamua kuja hapa na kumbughudhi/kumchafua tu Mkuu Ngw'amapalala,au!?
Tundu Lissu hakusema Nyerere amezoea kuishi kwa uongo na udanganyifu kama kichwa cha habari cha mleta mada kinavyosemaKipi alichoongeza au kutia chumvi...ambacho yule Tundu Lissu hakukisema dhidi ya Nyerere!?
Sio kwamba Tundu Lissu aliongelea hivyo vitu mafichoni ina maana wote wanaokataa wameangalia ufafanuzi wa Lissu na wala sio kwamba mleta mada alisikia yeye mwenyewe tu...Si amejaribu kukuwekeeni mpaka link ya mumsikize neno kwa neno,au!?
Vilaza gani tena hao mkuu gombesugu?Mbona Mkuu wa Chuo nawewe unataka kuwa wale vilaza wangine!? Daah!
Sawa mkuu ila hapa tunajaribu kuwa objective na mleta mada pia anatakiwa kuwa objective piaMie nakustahi mno Mkuu na pia nathamini baadhi ya michango yako...kwa hiyo jaribu kuwa objective!
Kama vipi mkuu gombesugu uwe unatembelea pia jukwaa la great Thinkers uone michango ya watu imeenda shule, utakutana pia na duru za siasa kule na michango mingi iliyonenepa, hapo kwa Yericko Nyerere nadhani una kitu unakitafuta maana nyote wawili mnafahamiana wenyewe, halafu una hoja za kichokozi sana...Mbona mwenyewe Yericko Nyerere...ambae ndo mtoto wa damu/wa kumzaa mwenyewe Nyerere,haonekani kushughulishwa saana
kama weye Kamanda,inakuwaje hii!?
nyerere ndio role model wa dr.slaa, mbowe , yericko nyerere,bensaanane halafu tundu lisu anamtukana.. lisu hana adabu kwa viongozi wake wa chama
Mkuu, nani amesema hapa kuwa Mwl. Nyerere hakuwa mwanadamu?.
Tukubaliane tu kuwa, Mh. Tundu Lissu amepasua jipu ambalo wengi waliogopa na wanaendelea kuogopa kulipasua. Kwa lugha inayoeleweka na wengi, amemchana chana Mwl. Nyerere na pamoja na kitabu chake cha Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania.
Tundu Lissu ni smart lawyer na very good mwanaharakati but he is a lousy politician....huwezi mtukana Nyerere na isi ku cost
Tupo pamoja rafiki hata mimi naamini kakosea vingi; ndipo sasa na uliza should we then seat down crying like babes to wait until it dawns? Should we not therefore rise and set a good course for our destiny as a country?
Nyerere is a history if we allow him to be our destiny we are doomed; blessed are we if we are to regain our conscious and do the proper and not the popular ways to reach our destiny!
Mkuu nimekusoma!
Takriban hayo yoote nakubaliana na weye!
Tatizo lililopo hata huyo kilaza Tundu Lissu pia anatumika tu kwa maslahi ya mmiliki wa Chadema!
Hakuna chochote/lolote jipya alilozungumza Tundu Lissu...ambalo sisi wangine hatujawahi kulizungumza humu-JF na kwingineko!
Unyama,uharamia na uzandiki wa Nyerere unafahamika kwa myaka yoote ya maisha yake yule Mzee wa Kizanaki!
Tatizo ni yakua huyo Lissu na Chadema yake...nao pia hawana credibility wala integrity ya kuzungumzia urongo,uzandiki,unafiki,kuchafuana kisiasa na uharamia mwangine...sababu hiyo pia ndo michezo ya hao Chadema,au!?
Ahsanta.
Mkuu, nani amesema hapa kuwa Mwl. Nyerere hakuwa mwanadamu?.
Tukubaliane tu kuwa, Mh. Tundu Lissu amepasua jipu ambalo wengi waliogopa na wanaendelea kuogopa kulipasua. Kwa lugha inayoeleweka na wengi, amemchana chana Mwl. Nyerere na pamoja na kitabu chake cha Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania.
Umeamua kuchagua hayo ya nyerere tu!? Je akina mwakyembe walioandika kitabu kuja kukana kwa midomo? Je kina Shifji na ukosefu wa uti wa mgongo kwa kupinga yale aliyoamini na kuwachechemua Zenji? Je wale wasomi wa vyuo vyote TZ waliokaa na kuandika andiko la serikali tatu sasa wanatumiwa kama magogo ya chooni kuandika tena serikali mbili!! MAGOGO YA CHOONI YAKO MENGI!! ukiwepo wewe mtoa mada uliyejikita kwenye sehemu moja ya Nyerere tu!! pole huna wafuasi!!! Wa kuantagonize na LISSU!!Katika mwendelezo wa kupinga mawazo na mfumo wa utawala wa Mwl. Nyerere. Tundu Lissu amepasua jibu ambalo wengi huwa wanaogopa kulipasua pale aliposema kuwa Mwl. Nyerere alikuwa ni "msanii wa kisiasa" kwa sababu aliyokuwa anayasema siyo yale aliyokuwa anayatenda kuhusiana na suala la Muungano. Haya ameyabainisha wakati akitoa hoja kwenye Bunge Maalum.
Mh. Tundu Lissu ameenda mbali na kusema, Mwl. Nyerere alizoea vya halamu na vya halali hakuviweza. Katika kuthibitisha maneno yake, Mh. Tundu Lissu alisema, mwaka 1968, Mwl. Nyerere aliudanganya ulimwengu pale aliposema kupitia gazeti la Observer la UK, Iwapo umma wa Zanzibar bila ya ushawishi kutoka nje, na kwa sababu zao wenyewe, wataona kuwa Muungano una hasara kwa uhai wao, sitawapiga mabomu kuwalazimisha......Muungano utakuwa hauna tena sababu ya kuendelea iwapo washiriki wake wataamua kutathmini na kuthibitisha jambo hasa tukio la kihistoria kama Muungano'.
Mwaka 1984, Wazinzibari walipohoji Muungano, Alhaji Aboud Jumbe akafukuzwa kazi kwa amri ya Mwl. Nyerere na amewekwa kizuizini Mjimwema mpaka leo. Wolfgang Dourado akawekwa kizuizini, Bashiri Swanzy akapakiwa kwenye ndege ya kwanza akapelekwa Ghana.
Mh. Tundu Lissu aliendelea kusema, kwa vile Mwl. Nyerere alizoea vya kunyonga, kwenye Kitabu chake cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania, Mwl Nyerere alisema, 'huko nyuma baadhi ya viongozi wapinzani wa Muungano wameishawahi kusema tufanye referendum kwa Zanzibar kuhusu Muungano, tukakataa kwa sababu safi kabisa'.
Tundu Lissu anadai, Mwl. Nyerere hakukataa hoja ya Muungano kwa sababu safi kabisa, bali aliwaweka kizuizini wale waliohoji Muungano. Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uwongo na hakuweza kusema kweli.
Kitu muhimu kabisa cha kujiuliza na kufikiria. Kama kweli Mwl. Nyerere alikuwa anaishi kwa uwongo na udanganyifu, ina maana hata hati ya Muungano haipo na kama haipo, ina maana amewaingizwa 'mkenge' wananchi na hasa wanaCCM kwa kusimamia hoja ambayo kiuhalisia haipo. (Muungano wa serikali mbili).
Tukikubaliana na hoja ya Tundu Lissu, inabidi tujiulize, Kwa nini Baba wa Taifa alikuwa anaishi maisha ya uwongo na udanganyifu?. Alikuwa anafanya hivyo kwa manufaa ya nani?.
Kama hoja ya Tundu Lissu ni kweli basi hatuna budi kusema, kweli uwongo hupanda lifti wakati ukweli hutumia ngazi kuwafikia walengwa!.
Hoja hii inanipeleka kwenye angalizo la sababu ya baadhi ya wajumbe wakiongozwa na Leticia Nyerere kushauri bunge kwa nguvu zote liweke mipaka kwenye kanuni za bunge zikiwataka wabunge kutowadharirisha waasisi wa Muungano. Kumbe nyuma ya hoja zao walikuwa wanaogopa ukweli usijulikane!.
Mpaka katiba mpya ipatikane, tutaona na kusikia mengi!.
Kauli mbiu ni serikali moja au kila nchi ichukue fito zake kwa sababu watu tuliowatuma kwenda kumalizia mchakato wa katiba kwa sasa wanahoji uharali wa Muungano huku wakitaka mpaka makaratasi yenye sahihi za waasisi wa Muungano. Hawa wabunge wameshindwa kufanya kazi ya kumalizia mchakato wa Katiba badala yake wanaanza kuuliza kama Muungano ni halali au batili. Yaani baada ya Miaka karibia 50 ndiyo tunaanza kuuliza Muungano kama ni halali huku waasisi wa Muungano tukiwasema ni waongo na wadanganyifu.
Ninadhani kuna kitu hakiko sawa kwenye baadhi ya hoja za Wabunge!.
[video=youtube_share;bB7BxxMepR8]http://youtu.be/bB7BxxMepR8[/video]
[video=youtube_share;jE7oTPXtpas]http://youtu.be/jE7oTPXtpas[/video]
hakuna ghadhabu hapa gombesugu dhidi ya mleta mada, sasa mtu anakuja anasema Tundu Lissu ni debe tupu bila ya uthibitisho wakati yeye Lissu anaongea kwa vithibitisho na haya yote anasababisha mleta mada kwa lengo lake hilo hilo ambalo watu wanaanza kutukana mtu bila ya hoja eti kisa amesoma title tu ya huyu mleta mada
Sasa nimlaumu vipi Tundu Lissu wakati alieleweka vizuri halafu alikuwa haropoki, tunaweza tukawa tunajadili kumbe hatuelewani tuna jadili kitu gani, yamkini pia unaweza ukawa unadandia treni kwa mbele
Dah! huu ni uongo sasa unaosema, umesikia wapi Tundu Lissu ametamka hayo maneno, ndio maana nakwambia mleta mada amewaingiza chaka na wewe kwa kuongozwa na chuki umeingia kingi yaani unacheza ngoma ambayo hauijui,wapi Tundu Lissu amesema Nyerere alizoea vya kunyonga ndo maana hakutamani vya kuchinja? eti FaizaFoxy unaweza kumsaidia nduguyo...
Mbona hueleweki unataka kujenga hoja gani hapo!?
cc chama
acha uongo mkuu gombesugu yaani Tundu Lissu amepata darsa kutoka kwa FaizaFoxy nadhani hapo unatania tu, sidhani kama huko sawa, misimamo ya Tundu Lissu inajulikana toka zamani sasa iweje leo awe mchovu, kipindi fulani aliongea kuhusiana na Zanzibar kukiuka au kuvunja Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alizomewa na kutukanwa tu bila hata ya hoja na ma ccm pamoja na wabunge kutoka Zanzibar, lakini yeye huwa anasimamia ukweli kwa maana yeye hajazoea vya kunyonga kama watu wa ccm, au kusema hasioyatenda kama kina Mwakyembe huku anaaandika hivi kule anapinga alichokiandika yaani ni ujanja ujanja tu, sasa unatudanganya eti Tundu Lissu kapata nondo kutoka kwa FaizaFoxy nadhani hapo umeongozwa na hisia bila ya uhalisia wowote...
Kwa hiyo hapo unamaanisha baada ya kumwomba radhi na yeye pia abadirishe misimamo yake? kwa hiyo inawezekana hata yeye mwenyewe alikuwa hajielewi mpaka nondo zilipotoka kwa Tundu Lissu!?
Ahsanta sana pia...