Tundu Lissu: Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu

Tundu Lissu: Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu

Ng'wamapalala kwa kiasi fulani anaweza akawa sawa, lakini title aliyoamua kuitumia ana madhumuni fulani, yaani amelenga kitu fulani, yaani ametoka title kwa kufasiri na kuchambua...
Mkuu, hili siyo suala la kuwa "sawa kwa kiasi fulani". Maudhui ya Mh. Lissu ndiyo yanayotengeneza title ya kile alichokisema pale bungeni.

Ninadhani unasumbuliwa na kaugonjwa ketu watanzania wengu ambako ni kutokubali ukweli kwa jinsi ulivyojibainisha/unavyojibainisha.
 
Mkuu wangu ndiyo ninaingia kwa sasa. Kama unavyofahamu tena, watoto lazima wavae na wapate chakula mezani. Nilikuwa niko kwenye shughuri za kutafuta visenti ili watoto waishi.

Kwa sasa najaribu kuyapitia mawazo na maoni ya wachangiaji.


Tuko wote.

Shukran Mkuu nimekusoma!

Pamoja kwa saana tu Kaka!

Mpaka sasa hatujashuhudia yeyote aliekuja na hoja nzito zenye mantik hapa jamvini...wengi wao wanajitahidi tu kukubeza na kukulaumu weye mbeba ujumbe!? Daah!

Endelea kumwaga dose Kaka...Wazalendo wenzio tunakusoma!

Wee mtu unatisha! Duuh!

Pamoja kwa saana tu!

Ahsanta.
 
Lisu anawapatia sana magamba. Anawatia taratiiiibu!

Mkuu,

Mbona watuletea lugha za kibanati na makhanatha!?

Au umeamua kumchafulia hii thread yake Mkuu Ng'wamapalala!?

Sidhani hao uwaitao ati "magamba" wana appreciate lugha utumiayo dhidi yao!? Daah!

Ahsanta sana.
 
Tundu Lissu ni smart lawyer na very good mwanaharakati but he is a lousy politician....huwezi mtukana Nyerere na isi ku cost

Haaaahaaaa....hajagundua hilo miaka yote hii? Kuna game nyingine ndogo ndogo zinawatoa povu mpaka super strikers kwa ugumu wake wa kuzicheza. This is one of those games kwa mhe. Lissu,lol!
 
NI ukweli kuwa nyerere alifanya mambo mengi makubwa lakini ni ukweli kuwa alifanya pia makosa makubwa mojawapo ni hili la Zanzibar na muungano, Zidumu fikra sahhi za Nyerere
 
NI ukweli kuwa nyerere alifanya mambo mengi makubwa lakini ni ukweli kuwa alifanya pia makosa makubwa mojawapo ni hili la Zanzibar na muungano, Zidumu fikra sahhi za Nyerere


Mkuu wakupaswa kumlaumu Nyerere ni Watu Wa Nchi ya Zanzibari na sio sisi Watanganyika!

Kuna Kitu Nyerere alikona Zanzibari ambacho ni faida kwetu sisi watanganyika! Na ndiyo maana ikabidi tuwakalie tu wazanzibari kimabavu !

Nyerere hakufanya vile kwakuwa alijiskia tu bali ni faida kubwa aliyoiona kwa sisi watanganyika !
 
Mkuu,

Mbona watuletea lugha za kibanati na makhanatha!?

Au umeamua kumchafulia hii thread yake Mkuu Ng'wamapalala!?

Sidhani hao uwaitao ati "magamba" wana appreciate lugha utumiayo dhidi yao!? Daah!

Ahsanta sana.
Hii ngoma nzito sana hakuna Bavicha yeyote atakaeweza kuingia humu.

Nyerere, ni role model wa Dr.Slaa, Lema, Mnyika, Mbowe, na Bavicha, sasa Tundu Lissu, anawambia Nyerere alizoea kuishi kwa uongo.

Na Bavicha wanamuogopa Tundu Lissu unaona kazi hiyo.
 
Mkuu wakupaswa kumlaumu Nyerere ni Watu Wa Nchi ya Zanzibari na sio sisi Watanganyika!

Kuna Kitu Nyerere alikona Zanzibari ambacho ni faida kwetu sisi watanganyika! Na ndiyo maana ikabidi tuwakalie tu wazanzibari kimabavu !

Nyerere hakufanya vile kwakuwa alijiskia tu bali ni faida kubwa aliyoiona kwa sisi watanganyika !
Andiko lako linachagiza kuwa Mwl. Nyerere na Watanganyika waliihujumu Zanzibar kwa maslahi yao!. Are you serious?.

Hebu nisaidie kwa kudadavua zaidi.
 
Muunganooooo .hivi pemba na unguja viliungani vipi....Maana naona tanganyika na zanzibar tu.
 
Tumekuwa tukisema kwa miaka mingi sana kwamba nyerere alikuwa bumunda tuu, tunaitwa waislamu. Miaka kadhaa iliyopita miongoni mwa waja wa nyerere wa hapa JF, mmoja wao alisema nyerere ni zaidi ya mandela. Nikamjibu kwa kumwambia kwamba tofauti ya nyerere na mandela ni kwamba, Mandela angezaliwa nchi yoyote duniani, basi angekuwa rais wa nchi hyo. Lakini nyerere asingeweza kuongoza nigeria hata kwa siku tano tuu.

Haya sasa, baba wenu wa taifa huyo.
 
Mkuu.
Mbona ya Shivji , Mwakyembe na ya ma Proff. Hukuyasema.
Wale wale ambao hamsomi bible nzima, mnarukia viji mistari tu ili kujenga hoja zenu mfu.
By the way Lissu kaongea uongo kwani ?
Mkataba wa Muungano ni lini Serikali ya Kuanzia Nyerere mpaka JK ulipelekwa UN ?
Kuanzia janq binafsi nimeanza kumtizama the late Julius kwa jicho la tatu.
No wonder all the Problems we have now source yake ni yeye.

Kumtazama nyerere kwa jicho la tatu ndiyo kwanza unaanza leo? "welcome to the reality son". Watu wakisema kwamba nyerere ni muongo, dictator, mwoga wa mapambano ya kimawazo;.... wathao mnawaita siasa kali.
Haya haya yaliyosemwa na tundu lisu kama yangesemwa na sheikh ponda au ustaadh bin jumaa; wote msingeyaamini.
 
Waswahili bwana wamezoea ukoloni wa kifikra...mtu akisema ukweli anaitwa mkorofi na mwenye kiburi..tena maneno yake yaukweli yanageuzwa kuwa matusi...acheni ukoloni wa kifikra..ni wapi palipoandikwa mtu akishafariki mabaya yake yasijadiliwe?kama ni dhambi basi pia acheni unafiki wa kuenzi mazuri ya marehemu..
 
Kina shekh Ponda,Ilunga,na wapambanuzi wengi includence of me...tulifaham kwa kina mbichi za mwl Nyerere kitamboooooo....Hongera Hon Lissu kwa kuungana nasi katika kuweka bayana ukweli pacna woga....
 
Katika mwendelezo wa kupinga mawazo na mfumo wa utawala wa Mwl. Nyerere. Tundu Lissu amepasua jibu ambalo wengi huwa wanaogopa kulipasua pale aliposema kuwa Mwl. Nyerere alikuwa ni "msanii wa kisiasa" kwa sababu aliyokuwa anayasema siyo yale aliyokuwa anayatenda kuhusiana na suala la Muungano. Haya ameyabainisha wakati akitoa hoja kwenye Bunge Maalum.

Mh. Tundu Lissu ameenda mbali na kusema, Mwl. Nyerere alizoea vya halamu na vya halali hakuviweza. Katika kuthibitisha maneno yake, Mh. Tundu Lissu alisema, mwaka 1968, Mwl. Nyerere aliudanganya ulimwengu pale aliposema kupitia gazeti la Observer la UK, “Iwapo umma wa Zanzibar bila ya ushawishi kutoka nje, na kwa sababu zao wenyewe, wataona kuwa Muungano una hasara kwa uhai wao, sitawapiga mabomu kuwalazimisha......Muungano utakuwa hauna tena sababu ya kuendelea iwapo washiriki wake wataamua kutathmini na kuthibitisha jambo hasa tukio la kihistoria kama Muungano'.

Mwaka 1984, Wazinzibari walipohoji Muungano, Alhaji Aboud Jumbe akafukuzwa kazi kwa amri ya Mwl. Nyerere na amewekwa kizuizini Mjimwema mpaka leo. Wolfgang Dourado akawekwa kizuizini, Bashiri Swanzy akapakiwa kwenye ndege ya kwanza akapelekwa Ghana.

Mh. Tundu Lissu aliendelea kusema, kwa vile Mwl. Nyerere alizoea vya kunyonga, kwenye Kitabu chake cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania, Mwl Nyerere alisema, 'huko nyuma baadhi ya viongozi wapinzani wa Muungano wameishawahi kusema tufanye referendum kwa Zanzibar kuhusu Muungano, tukakataa kwa sababu safi kabisa'.

Tundu Lissu anadai, Mwl. Nyerere hakukataa hoja ya Muungano kwa sababu safi kabisa, bali aliwaweka kizuizini wale waliohoji Muungano. Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uwongo na hakuweza kusema kweli.

Kitu muhimu kabisa cha kujiuliza na kufikiria. Kama kweli Mwl. Nyerere alikuwa anaishi kwa uwongo na udanganyifu, ina maana hata hati ya Muungano haipo na kama haipo, ina maana amewaingizwa 'mkenge' wananchi na hasa wanaCCM kwa kusimamia hoja ambayo kiuhalisia haipo. (Muungano wa serikali mbili).

Tukikubaliana na hoja ya Tundu Lissu, inabidi tujiulize, Kwa nini Baba wa Taifa alikuwa anaishi maisha ya uwongo na udanganyifu?. Alikuwa anafanya hivyo kwa manufaa ya nani?.

Kama hoja ya Tundu Lissu ni kweli basi hatuna budi kusema, kweli uwongo hupanda lifti wakati ukweli hutumia ngazi kuwafikia walengwa!.

Hoja hii inanipeleka kwenye angalizo la sababu ya baadhi ya wajumbe wakiongozwa na Leticia Nyerere kushauri bunge kwa nguvu zote liweke mipaka kwenye kanuni za bunge zikiwataka wabunge kutowadharirisha waasisi wa Muungano. Kumbe nyuma ya hoja zao walikuwa wanaogopa ukweli usijulikane!.

Mpaka katiba mpya ipatikane, tutaona na kusikia mengi!.

Kauli mbiu ni serikali moja au kila nchi ichukue fito zake kwa sababu watu tuliowatuma kwenda kumalizia mchakato wa katiba kwa sasa wanahoji uharali wa Muungano huku wakitaka mpaka makaratasi yenye sahihi za waasisi wa Muungano. Hawa wabunge wameshindwa kufanya kazi ya kumalizia mchakato wa Katiba badala yake wanaanza kuuliza kama Muungano ni halali au batili. Yaani baada ya Miaka karibia 50 ndiyo tunaanza kuuliza Muungano kama ni halali huku waasisi wa Muungano tukiwasema ni waongo na wadanganyifu.

Ninadhani kuna kitu hakiko sawa kwenye baadhi ya hoja za Wabunge!.
[video=youtube_share;bB7BxxMepR8]http://youtu.be/bB7BxxMepR8[/video]
[video=youtube_share;jE7oTPXtpas]http://youtu.be/jE7oTPXtpas[/video]

Kila kitabu na zama yake! Mimi sioni dhambi ya watanzania kuhoji leo kama Muungano una uhalali , au kama una usawa, au kama kasoro zake zinatatulika! Kama Watanzania wa 1964 hawakuwa na uelewa huo, wa leo wanao. Kama wanao sioni kama ni dhambi kwao kuhoji.

Binafsi najua ni kweli kuna usanii mwingi umekuwa unafanywa. Historia ya nchi yetu imepotoshwa sana tu. kwa kiwango ambacho watoto wetu wanazaliwa wakiujua owongo huo. Wanakua wakiukulia uwongo huo! hii ni aibu.

Ni katika misingi hiyo ya uwongo na ubabaishaji ndipo ilipozaliwa serikali ya ovyo kama hii ya sasa. Ambapo wananchi wamekuwa wanadanganywa kila kukicha, mpaka wanakuwa wageni kwenye nchi yao.

Wanatakiwa wahoji. Naaam wahoji kila kinacholeta mashaka. Ni haki yao na wanawajibika kufanya hivyo.
 
Kuna uwezekano mkubwa kuwa wewe ndiyo hujafahamu kiini cha hoja achilia mbali kujitambua!.

Kiini cha hoja ni Mh. Tundu kudai kuwa Mwl. Nyerere alikuwa anafanya kazi zake tofauti na kile alichokuwa anakisema au kukiandika kuhusiana na Muungano.

Kama ni suala la kufikiri. Kuna uwezekano mkubwa watu wengi walioishi miaka 50 iliyopita waliokuwa wanafikiri vizuri zaidi ya watu wengi wanaoishi mwaka wa leo. Dunia ya sasa imejaa consumer only. Hata kufikiri tu wanategemea watu fulani wafikiri kwa niaba yao.

Hata bunge la Katiba lina akisi hoja ninayoisema. Wengi bungeni wamelishwa maneno ya wanasiasa wachache na kuyameza bila kuhoji.

Nyerere alishakiri si mara moja kuwa kuna mambo mazuri alifanya na mengine mabaya, kwanini sisi tunataka kumfanya yeye ni malaika hakukosea?
 
Tusubiri, ukweli ukidhihiri uongo hujitenga. Kumbuka juzi, Sitta ingawa yupo busy bungeni lakini kaitwa na Pengo na kaenda mbio-mbio, jiuliize kunani?

Na kwa Shehe Mkuu mbona husemi? ??
Acha udini wako Mtoto wa Kike...!
 
Tundu lisu anaona uwongo wa mwl.nyerere2...mbona hasemei uongo wa historia aliyosoma ya watu kutokea kwa nyani? Au wakisema wazungu siyo uongo? Wakat huyu mzee akiwapo hakuna hata paka mmoja aliyethubutu kusema kwa kuogopa kuumbuka, ni uongo huu huu ulitupatia ziwa nyasa, mt.kilimanjaro na kagera. Ule ulikuwa wakat wao yeye leo amefanya nn kama siyo porojo2 na kula pesa za walala hoi.
 
Back
Top Bottom