Tundu Lissu: Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu

Hivi mtu ukiambiwa uliunda MUUNGANO kiharamu, kwa uongo, kwa kuzoea vya kunyonga haya sio matusi?

Je, ukiambiwa wewe sio Mungu wala Malaika bila ya kuambiwa wewe pia sio Shetani wala Luciferi haujatukanwa?

Ukiambiwa kile kilichosababisha uwepo na uhalali wa MUUNGANO hakipo kabisa hadi UN umesifiwa?

Hata pale unapoonyeshwa kwamba hati ipo bado unadai sahihi za marehemu hawa sizo utajisikiaje?
 
Teh teh....nadhani litakuwa kubwa sana...halitamkiki.
Hivi Warioba hawajamtukana au hayo matusi yanabagua mzungumzaji!!?
 
Mimi bado sijaona kosa la Mheshimiwa Lissu. Mambo yote aliyosema ni ya ukweli:
Tatizo Ntarahamwe hawapendi kusikia ukweli kwa sababu wanaishi kinafiki na kuchekacheka.

Bila Lissu hiyo hati ya kughushi isingetolewa. Na mpaka sasa hao wajumbe hawajagawiwa nakala yake.

Hatua gani imechukuliwa kwa yule aliyegushi saini ya Mwalimu katika "Acts of Union"?
 

Kutoka kamusi ya Kiswahili hapo hakuna tusi hata moja..sijajua nkuulize hivi Baba akiahidi kukuletea zawadi na asipoleta..ukimwambia baba umenidanganya..utakuw umemtukana..
 
mkuu watu wanalalamika tu lakin hawataji tusi pengine ni njia ya kututoa kwenye hoja za lisu
Utajisikiaje utakapoambiwa umezoea vya kunyonga, umezoea vitu haramu, kwamba MUUNGANO uliouasisi katika mazingira magumu namna ile hauna hati halali hadi UN, kwamba umezoea kuendesha mambo kwa uongo tu,...., na kejeli nyingi za huku mitandaoni unazihamishia Bungeni.

WaTanzania mmezoea matusi gani?
 
Mbona taifa linaharibiwa namna hii.
Kama kweli katukana c muhimili wa kutoa hukumu c upo, au ni umma?
Inawezekana hajaanza kutukanwa leo !
 

Hatukana bali aliongea kiswahili cha kiingereza, mfano mvulana /msichana wakiwa wakubwa. Huitwajie kwa kizungu kama si kuvunja ungo!
 

Wanatafuta hutuma ya wananchi..mi naona Lissu amesema ukweli ambao wengi hawapendi kuusikia..
Mtoto wako akikwambia baba we muongo.(baada ya kutomnunulia zawadi ulomuahidi)...utamchapa.? na kulalama kuwa amekutukana..!?
 
Kutoka kamusi ya Kiswahili hapo hakuna tusi hata moja..sijajua nkuulize hivi Baba akiahidi kukuletea zawadi na asipoleta..ukimwambia baba umenidanganya..utakuw umemtukana..
Mfano wako huu hauendani kabisa na alichokisema mjinga Lisu. Baba anakuwa hajaleta tu zawadi alioahidi. Mtoto mwenye malezi mema hathubutu kumwambia Baba yake mwongo, aliyezoea vya haramu, vya kuchinja haviwezi,...
 
kusema kwamba Nyerere hakuwa malaika.
ccm wanaamini kuwa nyerere alikuwa malaika
 
Mfano wako huu hauendani kabisa na alichokisema mjinga Lisu. Baba anakuwa hajaleta tu zawadi alioahidi. Mtoto mwenye malezi mema hathubutu kumwambia Baba yake mwongo, aliyezoea vya haramu, vya kuchinja haviwezi,...

neno uongo si tusi..
hayo mengine ni misemo ambayo hata kwenye kanga ipo..so hakuna cha ajabu..
mnatafuta huruma ya umma tu hakuna chochote
 
Kweli huwa haimpendezi muongo siku zote.

Sijaona makosa ya Lissu popote,ni uzushi na kashfa za kumpakazia tu.

Kama muungano haukuwa sahihi hakuwa na budi kuuita ni haramu.

Kwani unadhani Mwalimu Nyerere hakuwahi kufanya mambo haramu?Hakuwa malaika,kwahiyo ana dhambi zake pia.

*Mungu amrehemu,apumzike kwa amani.
 
kusema kwamba Nyerere hakuwa malaika.
ccm wanaamini kuwa nyerere alikuwa malaika
Mwalimu alikiri mara nyingi tu pale alipokosea kama binadamu tena hadharani. Mwalimu hakuwahi kujitukuza kwa lolote.

CCM ya sasa haimthamini kabisa Mwalimu. Ndio maana akina Jaji Warioba na SAS wakaona hata huu Muungano aliouacha Mwalimu ambao umechezewa kwa kiasi kikubwa ni bora uondolewe tu.
 

- tunawasamehe wenye akili lakini sio wendawazimu kama Tundu Lissu ametukana Mwalimu halafu amemtukana na Mzee Mtei, inaa maana kwao huyu mbunge wenu hakuna wazee wala watuwazima hivi amesoma nini hasa kinachomfanya ajione ana akili sana kuliko Mwalimu na Mtei?

- Chadema mnacheza siasa za self-destructions badala ya kuja kuo,mba radhi mnakuja na hizi? Subiri hii habari kwenye uchaguzi ujao mbona itakuwa super sana!!

Le Mutuz System
 
Wadau.,naomba kufahamishwa tusi ambalo Tundu Lissu amemtukana Mwalimu Nyerere,maana nimekuwa nikiskia watu wakilalama na kumlaumu Lissu.
Mod nsomba usiunganishe uzi huu..ili tupate ukweli..

- Mwalimu alikuwa na tabia ya kuishi kwa uongo uongo na ujanja ujanja, ndio maana hata huu muungano wake hauna hati, unasema haya sio matusi? kwa baba wa Taifa?

- Kaka soma Jambo Leo kesho uone hii habari nimeiweka vizuri sana kule!!

Le Mutuz System
 
Tundu Lissu mwenyewe amekiri sasa sijui wewe unakataa nini. Lissu amemwambia Nyerere ameisha kwa uwongo maisha yake yote. Alizoea vya haramu. Wewe bado huoni kwamba hayo ni matusi. Kubalini tu kwamba hapa jamaa alichemsha big time yaishe.
 
neno uongo si tusi..
hayo mengine ni misemo ambayo hata kwenye kanga ipo..so hakuna cha ajabu..
mnatafuta huruma ya umma tu hakuna chochote
Uongo linakuwa sio tusi kama kilichofanywa, kilichosemwa au kilichotendwa ni uongo kweli. Kipi katika MUUNGANO wa Tanganyika na Zanzibar ni uongo? Hati ya Makubaliano ya Muungano haipo kama alivyosema mjinga Tundu Lisu?

Unaikumbuka approach ya JJ Mnyika kwenye suala hili? Ulimsikiliza Evod Mmanda kwenye suala hili?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…